Kauli za sasa za Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kuhusu CORONA zimeshaanza Kuzua 'taharuki' nchini, hivyo ama adhibitiwe au ajiuzuru upesi

Kauli za sasa za Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kuhusu CORONA zimeshaanza Kuzua 'taharuki' nchini, hivyo ama adhibitiwe au ajiuzuru upesi

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Tunajua na hakuna Mtanzania hasa mfuatiliaji wa Mambo asiyejua kuwa kiukweli COVID-19 ni hatari na ' inapukutisha ' Watu kweli kweli kuanzia Mataifa ya Kitajiri (Ulaya na Marekani) na hata katika baadhi ya nchi zetu za Afrika na kwa Majirani zetu wakubwa Kijiografia Kenya, Uganda na Rwanda.

Nimekuwa nikifuatilia hasa kwa baadhi ya nchi zenye Maambukizi na hata Vifo jinsi Mawaziri wao wa Afya wanavyokuwa ' Smart ' kama kutoa Taarifa kwa Wananchi Wao katika njia ya Kiumakini na iliyojaa zaidi Saikolojia ya Kimawasiliano kiasi kwamba haiwezi Kuwashtua.

Hakuna asiyejua (labda awe Mpumbavu tu) kuwa karibia 85% ya Wananchi wa hizi nchi zetu Masikini (za Kingumbaru) Tanzania ikiwemo upataji Wao wa Kipato unategemea mno Kutoka na Kutafuta katika sehemu mbalimbali hivyo ikitokea tu wakapewa Taarifa kwa Kitisho itawatesa zaidi Kisaikolojia.

Muda si mrefu Waziri wa Afya wa Tanzania Mheshimiwa Ummy Mwalimu ametoka Kutoa Kauli ambayo kwa tulio Mtaani sasa (katika Jamii) tunaanza Kuona jinsi Watu wakianza Kuchanganyikiwa na Kupata ' taharuki ' ukizingatia tayari harakati za Sikukuu ya Pasaka zimeshaanza kwa wengi.

Kauli yake Waziri ya kuwataka Watanzania wajiandae kwa Maambukizi Makubwa zaidi ya COVID-19 ndani ya Siku chache zijazo kutoka sasa mwenyewe akiyaita ' Community Transmission ' ilipaswa itolewe Kiumakini na ikiwezekana awahusishe Wataalam wa Mawasiliano na sivyo alivyofanya.

Tayari huku Mitaani naanza Kushuhudia Watu wakitishana kuwa sijui kuanzia Wiki ijayo Watanzania wengi hasa wana Dar es Salaam watakufa sana kwa CORONA. Kuna Watu nimewasikia wakisema kuwa wanataka Kulikimbia Jiji la Dar es Salaam ili Wasife na tufe Sisi tu Mapopoma wa Jiji hili.

Na asichokijua huyu Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ni kwamba hii Kauli yake inaweza ikapelekea hata hali ya Maisha na ya Kibiashara (hasa kwa Bidhaa na Huduma) kuanza kuwa ngumu na Watu Kuteseka. Na kuna Uwezekano hata Uhalifu ukaongezeka na hali kuwa mbaya zaidi.

Kwa ' Udhaifu ' huu wa utoaji wake Taarifa na hasa hii ya leo kuwa Watanzania wajiandae kwa ' Dhahama ' kubwa ya CORONA na Mwenendo wake mzima katika Kukabiliana na hili Janga sasa ni rasmi huyu Mwamama na Dada yetu ' ajiuzuru ' tu upesi awapishe wenye uwezo zaidi yake.

Nimesikitika sana!

Nawasilisha.
 
Hangaikeni wee ila tambueni hakuna mtu anayeweza kulinda uhai wake duniani. Hakuna aliye na mamla na uhai wake..Muda ukifika utakufa kama bado huwezi kufa kamwe!
.....Bwana asipoulinda mji waulindao wanakesha
 
Ummy alikuwa anaendekeza usanii na sasa usanii umefikia hatua ya kulipuka hivyo hana ujanja tena. Tulipiga kelele sana tukaambiwa na ma superstitious wa Jf kuwa walikuwa wanaugua vicorona vidogo vidogo kuanzia december mwaka jana hivyo Corona kwao siyo ishu.
 
Ummy alikuwa anaendekeza usanii na sasa usanii umefikia hatua ya kulipuka hivyo hana ujanja tena. Tulipiga kelele sana tukaambiwa na ma superstitious wa Jf kuwa walikuwa wanaugua vicorona vidogo vidogo kuanzia december mwaka jana hivyo Corona kwao siyo ishu.

Yawezekana kuna Kitu Watanzania tunafichwa na nimekuwa nikijiuliza Maswali mengi sana kwamba kwanini Serikali ya China iko ' busy ' mno Kuisadia Tanzania kwa hii COVID-19 ambayo haina Kiwango hicho Kikubwa cha Maambukizi na hawafanyi hivyo kwa nchi kama ya Kenya ambayo kila Uchwao ina Maambukizi mengi.

Ukiangalia kwa umakini huu ukaribu wa Kimsaada wa Wachina na hivi leo Waziri wa Afya anasema anaangalia uwezekano wa Kuwaambia Watanzania wawe wanatumia Barakoa ( Mask ) yawezekana kuna lililojificha zaidi juu ya COVID-19 hapa Tanzania pengine hata huko Kenya, Uganda na Rwanda. Naanza Kuogopa sasa!
 
Kauli yake Waziri ya kuwataka Watanzania wajiandae kwa Maambukizi Makubwa zaidi ya COVID-19 ndani ya Siku chache zijazo kutoka sasa mwenyewe akiyaita ' Community Transmission ' ilipaswa itolewe Kiumakini na ikiwezekana awahusishe Wataalam wa Mawasiliano na sivyo alivyofanya.
Kwa mawazo yako unadhani waziri kakurupuka tu bila ya kupewa data na wataalamu?
Jaribuni kufuata maelekezo ya serikali na wataalam,tatizo nilioliona ni kwa nini waziri katoa tamko wakati wa pasaka!
Una hiyari kufuata wataalam, au akili yako
 
Mkuu inaelkea wewe ulisomea historia na kiswahili darasani, na hujui A toZ za sayansi.
Tumekuwa tukionya humu mtandaoni juu ya maambukizi ya huu ugonjwa na wengi wenu mmeamua kuwaamini wanasiasa.

Maambukizi kama ilivyo huko Ulaya hayaepukiki na dawa yake si sanitizer na kunawa maji ya kutiririka na sabuni tu.

Tunaposema total lockdown watu hamuelewi, ngoja watu waanze kuanguka kama nzi.
 
Back
Top Bottom