Kaulimbiu ya Muslim university of Morogoro imekosewa

Kaulimbiu ya Muslim university of Morogoro imekosewa

Malaika hawana hiyari
Majini yana hiyari kama binadamu

Malaika hawamuasi Muumba wao
Majini kwa kuwa wana hiyari wanaweza kuasi kama alivyoanza huyo lucifer aka ibilisi

Waislamu hawaabudu majini bali Mwenyezi Mungu

Baadhi ya majini nao huabudu Mwenyezi Mungu Mungu
Cha kushangaza malaika wa kiislamu wasiokuwa na hiari walimtahadharisha allah kwamba asiumbe binadamu.😂😂

Fundisho sahihi ni kwamba shetani alikuwa malaika (cherubim) na aliweza kupitisha ushawishi mpaka theluthi moja ya malaika wakaungana naye.

Wote kwa pamoja walipigwa na malaika Michael akiwa na malaika walio chini yake. Walifukuzwa mbinguni na kutupwa duniani. Ndio hao wengine wapo kifungoni na wengine wanazurula na kuwashawishi watu kufanya uovu. Wote hao ni waovu na hivyo hakuna malaika aliyefukuzwa mbinguni ambaye ni mwema. Wote wabaya.
 
@CAPO DELGADO jamaaa hata akili tu ya kufikiri sawa sawa unaonekana huna, sasa ww unayakataa majini wakati kuna majini ni bora kuliko wewe
Acha kueneza mafundisho potofu. Majini wote ni waovu. Ila waislam kwasababu mnapenda unajimu ndio mkajiwekea kwamba kuna ambao ni wema. Bado kitambo kidogo na wote mtaenda huko kwenye hayo majini yenu mnayoyaita mema.
 
Inategemeana na andiko lenyewe, mbona kituo kipo mwishoni na ulazima wa kuweka koma sijauona.
Chukua hii elimu, itakusaidia siku nyingine ukiwa unaandika proffesionally huko kazini.
Badala ya kuandika hivi,
Jinsi unavyoandika haitaji elimu kubwa kukutambua kuwa wewe ni kichwa boksi maana andiko lako lina makosa mengi ya kiuandishi kama mtoto wa chekechea.
Ungeandika hivi:
Kwa jinsi unavyoandika, haihitaji elimu kubwa kukutambua kuwa wewe ni kichwa boksi. Maana andiko lako lina makosa mengi ya kiuandishi kama mtoto wa chekechea.
 
sioni sababu ya kubishana kwenye misingi ya dini hapo hamna kilichokosewa kwakua wamenukuu kutoka kwenye maandiko yao matakatifu.
Muda mwingine hebu tujiulize itakuaje kama tutafika huko tukakuta ukristo ndio dini ya kweli au uislamu ndio dini ya kweli tusiwe wepesi sana w kukosoa vitu ambavyo hatujui undani wake.
Ni kweli kabisa palivyoandikwa ni makosa ila haiwez kuwa kosa kama ni nukuu toka kwenye vitabu vitakatifu
 
Chukua hii elimu, itakusaidia siku nyingine ukiwa unaandika proffesionally huko kazini.
Badala ya kuandika hivi,
Jinsi unavyoandika haitaji elimu kubwa kukutambua kuwa wewe ni kichwa boksi maana andiko lako lina makosa mengi ya kiuandishi kama mtoto wa chekechea.
Ungeandika hivi:
Kwa jinsi unavyoandika, haihitaji elimu kubwa kukutambua kuwa wewe ni kichwa boksi. Maana andiko lako lina makosa mengi ya kiuandishi kama mtoto wa chekechea.
Na wewe kama unaandika chagua kutumia lugha moja , haijakaa kisomi mtu kuchanganya lugha katika uandishi.
 
Muda mwingine hebu tujiulize itakuaje kama tutafika huko tukakuta ukristo ndio dini ya kweli au uislamu ndio dini ya kweli
Duniani hapa hakuna dini yoyote iliyosahihi na ndio maana Yesu Kristo alikuja kuleta wokovu. Dini ni jitihada za mwanadamu kumtafuta Mungu. Jitihada hizo zinakoma pale mtu anapompata Yesu Kristo maana anapata uzima wa milele na kujazwa Roho Mtakatifu ili aweze kuishi maisha ya kumpendeza Mungu.
 
Kila kitu kifanywe kwa ajili ya kutaka radhi za Allah na kuchunga mipaka yake .Ukiweka hilo akilini hatofanya udanganyifu , vilevile jitahada zitaongezeka kwa kuweka akilini kuwa anachokifanya ni ibada na ina malipo ndani yake.
Hapo aya inaongelea kusoma tu (reading)....wewe unaongelea kila kitu...Tumwamini yupi?
 
Hapo aya inaongelea kusoma tu (reading)....wewe unaongelea kila kitu...Tumwamini yupi?
Kusoma kunahusisha jitihada, uvumilivu, kufundisha nk.

Katika Qu'ran aya mbili panaweza kutolewa mada na vitabu kibao kutokana na maudhui na ujumbe wake katika engo tofauti tofauti.
 
Kusoma kunahusisha jitihada , uvumilivu ,kufundisha nk.

Katika Qu'ran aya mbili panaweza kutolowa mada na vitabu kibao kutakana na maudhui na ujumbe wake katika engo tofauti tofauti.
Kusoma hakuhusishi hayo yote.
Kusoma ni kusoma tu.
Kama kula ilivyo kula tu.
Kwani wewe unaposoma haya maandishi ya hii comment yangu hapa saivi umehusisha uvumilivu gani?Umefundisha nini?

Ukiona wanadamu wanaanza kuongezea mambo yao (shirk) kulingana na mawazo yao kwenye Qur'an, inakuwa kama wanamsaidia mungu hivi..Astaghfirullah
 
Kusoma hakuhusishi hayo yote.
Kusoma ni kusoma tu.
Kama kula ilivyo kula tu.
Kwani wewe unaposoma haya maandishi ya hii comment yangu hapa saivi umehusisha uvumilivu gani?Umefundisha nini?

Ukiona wanadamu wanaanza kuongezea mambo yao (shirk) kulingana na mawazo yao kwenye Qur'an, inakuwa kama wanamsaidia mungu hivi..Astaghfirullah
Unabishana na Khomenei?
Huna adabu kijana kafri🤣🤣
 
Back
Top Bottom