Kauziwa rice cooker Tsh. 300,000 na Waturuki, kaikuta inauzwa Tsh. 140,000 Mlimani City. Anawaza amalizie hela yao ama?

Mikopo ina riba hasaa. Kuna hawa wakopesha simu simu ya lak mbili mtu analipa lak 5. Kuna sehemu kuna atm ya crdb pembeni wana kiofisi chao kila nikienda atm wananiita bro bro njoo ukope simu. Mimi jibu langu nawambia kwani nyie hamwoni nimeshika simu mkononi.
Sema wabongo si waaminifu lazima.uweke riba kubwa kulipia watakaokutapeli
 
Vitakutukana kituruki mpaka utaomba poo

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Ilaa wanaibiwaaa hatareeee....kuna mdada.mmoja tegeta alichukua vituvya kama.laki nane akatanguliza lak3 kumbe anahama duka ndani ya huo mwezi aisee nilijisikia vibaya sema nkawaza nawao siwanapiga mwosha huoshwa
Safi aliwanyoosha. Majamaa ni matapeli sana yale unamuuzia mtu kitu cha 60,000 kwa laki 300,000. Hiyo kwanza ni kusababisha inflation nashangaa serikali why ipo kimya kuchekea aina hii ya ulanguzi wa bei kwa raia wake.
 
Mkopo lazima umalizie japo Ukiwa mtata unadinda na ukienda kwenye sheria unaweza shinda.

Kikubwa ni kuwa mtata maana huo ni Utapeli
 
Riba ipi ya 120% Kwa mwezi? Kuna sheria ipi inaruhusu riba ya hivyo?
Wapumbavu hao achana nao. Watu hawana hata elimu ya uchumi basi japo wajue maana ya interest rates limits allowed by law, wajue effects za overpriced products kwenye uchumi na money inflation, wajue hata fraudulent activity kwenye biashara, hakuna wanalojua ni kubungua tu maneno wasiyojua yanawapeleka wapi.
 
Hatari huduma mpaka mlangoni kwako!
 
Mkataba unamfunga!Amalizetuu kuwalipa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…