Uchaguzi 2020 Kawe ya Halima Mdee, Halima Mdee na Kawe yake atosha

Uchaguzi 2020 Kawe ya Halima Mdee, Halima Mdee na Kawe yake atosha

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Wanakawe wote kwa umoja wetu bila kujadi itikadi zetu tujitokeze kwa wingi wetu tarehe 28.10.2020 tuendelee na sauti adimu ya Zege. Tunahitaji mtu wa kwenda kutusemea na siyo mtu wa kwenda kupiga meza.

Anayeitwa askofu hata kura za maoni alishika nafasi ya 3, maana yake hakubaliki hata ndani ya CCM.

Zipo sababu zaidi ya 200 za kumchagua Halima Mdee lakini hapa naweka baadhi yake 10 tu.

1. Ni mwanamke shupavu
Kwanza Halima ni mwanamke asiyeogopa,jasiri asiyeangalia uso wa mtu. Mfano wa kuigwa na jamii yote. Haisemei KAWE tu huyu ni mbunge wa taifa.

2. Halima Mdee ni msomi na mchapa kazi
Elimu ya Mdee ni ya sheria na siyo ya mambo ya kawaida kama ya yule jamaa. Anao uwezo mkubwa wa sheria na amekua mchango mkubwa katika miswaada mbali mbali ya kisheria inayoenda bungeni.

3. Ana maono
Halima Mdee amekua mbunge mwenye maoni katika kuibadili KAWE, amepita katika wakati mgumu sana wa kusimamishwa bunge kwa sababu ya misimamo yake isiyoyumba.

4. Halima Mdee siyo mbaguzi
Halima Mdee siyo mbaguzi wa Kabila,Rangi, dini wala kanda anakotoka mtu, huyu ni mwakilishi wa wananchi wote na amekua akiishi hivyo.

5. Msemakweli
Halima Mdee kwake nyeusi ni nyeusi tu haiwezi kubadilika ikawa nyeupe.Atakuambia ukweli bila kupepesa macho

6. Mzoefu katika siasa za Tanzania
Halima Mdee ni mzoefu sana katika siasa za Tanzania, ameingia bungeni tangu mdogo sana. Haendi kujaribu ubunge,huyu ni mwakilishi tayari.

7. Amekua msemaji wa wananchi
Wa wanakawe na taifa kwa ujumla. Halima Mdee amekua msemaji wa shida za wananchi na siyo mtu wa kupiga meza tu.

8. Mtetezi wa Mtoto wa Kike
Halima Mdee kama utakumbuka vizuri akiwa na kadhi kadhi ya kutiwa ndani na kupelekwa mahakamani akitetea haki ya mtoto wa kike kurudi shule akipata ujauzito. Hili suala lilichukuliwa simple sana hasa na watu wa CCM lakini wengi walikua wakimfuata Halima Mdee nyuma ya pazia awatetee.

9. Anajiamini sana
Halima Mdee ni aina ya wanasiasa vijana wasiotumia. Anafanya kazi kwa kufuata anayoyaamini, hana usanii kama wengine.

10. Mwadilifu
Halima Mdee ni nembo ya wanawake waadilifu wasiokua na shaka. Hana kashfa za rushwa wala wala kutumia vibaya rasilimali za jimbo zikiwemo pesa za mfuko wa jimbo.

Kwa ujumla kumwelezea huyu dada hadi kumaliza utaweza kujaza kitabu kizima kumuandika. Huyu ndiye mwakilishi sahihi wa wananchi wa jimbo la KAWE.
 
Huyo Asikofu Tapeli atafute kazi ya kufanya baada ya uchaguzi,maana hata kondoo wake wameshamsitikia walivyoona ni mzizi na Malaya, wamesha mkimbia na sadaka hakuna ndiyo mama kakimbilia kwenye mleko ya siasa nako kwa moto.
 
Hovyooo!
10 years kakaa Kawe kama mbunge, hana cha kuonyesha!.
Anatuletea ngonjera

Anayepaswa kuonesha alichokifanya ni nani kati ya serikali na mbunge? Serikali inaongozwa na chama gani na Rais gani?

Kama Tanzania iko kwenye the so called "UCHUMI WA KATI", hivi hiyo Kawe iko Uganda au Burundi?

Si anaweza kukuonesha " uchumi wa kati", mandege ya Dreamliners na Bombardier, Stiglaz Goji na Reli ya SGR?

Au haya hayawahusu wana Kawe?

I thought kuwa una akili za kuelewa haya kuwa Tanzania inaongozwa na serikali inayoundwa na CCM. Ndiyo maana wilaya na manispaa lilipo jimbo la Kawe;

å Mkuu wa wilaya - DC ni wa CCM....!!
å Mkuu wa mkoa - RC ni wa CCM....!!
å Mkurugenzi wa manispaa mwenyewe mafungu yote ya pesa za maendeleo na miradi mbalimbali ni CCM..!!
å Watendaji wote wa Tarafa, kata na mitaa ni CCM....!!

SASA, kama hawa wameshindwa kuleta na kusimamia shughuli za maendeleo katika manispaa ya Kinondoni yote kwa usawa pasipo upendeleo wa kimaeneo, Halima Mdee (MB) anaingiaje kwenye lawama??

Je, huu si utakuwa ni uzembe na kushindwa kwa CCM yenyewe?

Tatizo ni moja tu mlilonalo nyie wana CCM. Nalo ni hili....

Mnadhani watu wote ni wajinga na hawaelewi kwa viwango vya ujinga na kutokuekewa kwenu...!!
 
Yule mgombea wa ccm analaana ya kutifua tope kondoo wake ndio Kawe amekataliwa Mpaka na mbuzi .
IMG_20200919_183733.jpg
IMG_20200920_151758.jpg
 
Kawe ni jimbo la uchaguzi lenye wakazi wanaojielewa ; hili sio kama Kilosa mnakowapeleka watu mliowaokota jalalani na kuwalazimisha watu wawachague!!
 
Siwezi kumchagua huyu mama sjui wanamuita bibi i don't know,miaka 10 is enough,we want another person.

Kwaanza ana hulka yakijinga yakutuona sisi wapiga kura kuwa ni watu wa kitaa,no!

Awamu hii Itabidi umfate mnyika aliko mkapige zogo hko mtakutana na wakata umeme wawavunje mikono kama hamtaacha fyokofyoko
 
Wewe siyo mkaz wa kawe, au la umeamia juz huijui Kawe.
Si ajabu unaishi Nanjilinji huko Mtwara
Hata hujui kwa nini kuna sehemu zinaitwa Tangi Bovu, Aly Sykes au Goig, Miti Mirefu kwa Lukuvi, Barabara ya Makonde NSSF!
Siujui kama ulisha muona mzee Maranda wa Makonde na barabara zake!
Barabara zote nilizozitaja isipokuwa ya Aly Sykes ni mitaro ya maji ya mvua miaka nenda rudi-juhudi hafifu za Halima.

Nyie pusi wa juzi mnajifanya wajuaji kuliko.

Barabara ya Salasala imejengwa kwa juhudi za Makonda, Halima alikuwa kalala selo, hana maana kabisa.

Halima must go.
 
Wana KAWE tusijidanganye tukaharibu jimbo letu.
Dini na siasa vitu 2 tofauti. Isitoshe huyu Gwajiboy anaeleweka. Tutaharibu kila kitu.

Vyema tukajielewa. Maendeleo yanaletwa na Serikali iliyoko madarakani na sio mbunge pekee.

Mbunge ni kuwawakilisha wananchi. Na Tunaona alivyoyafanya mbunge wetu.
Sasa tujitambue kuwa isishangaze ukaja Serikali mbadala na tukayaona maendeleo lukuki. VIVA Haki na maendeleo yetu.
 
Back
Top Bottom