Wana lumumba mpogo?
Kazi nyingi asifiwazo Rais mtukufu wetu mama Samia, mmezipima mkaona hazitoshi kuwashawishi wananchi kumrudisha Ikulu siyo?
Hizo pikipiki mamia kwa mamia zilizoandikwa kwa jina la Samia 2025, wazalendo watumie jina gani kuziita
Ni zawadi au nini?
Ni rushwa kwa wapiga kura au takirima na au nini hasa?
Kwa nini isitoshe kuziamini kazi zake mnazozisifia kwamba zimewagusa wananchi na zitoshe kumpa kura tena?
Kwani mnamashaka tena na kazi zake mnazotuorodheshea kila leo hapa jf, kwamba mama kawazidi marais wote kwa kazi zilizotukuka na kwamba anaupiga mwingi?