Kazi kama Ufundi Selemara, Uashi sio za watu ambao hawajaenda shule kama tunavyo amini

Kazi kama Ufundi Selemara, Uashi sio za watu ambao hawajaenda shule kama tunavyo amini

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2020
Posts
4,548
Reaction score
11,901
Bongo kuna Kasumba na iko hivyo kwamba kazi za Ufundu Mbao au Uwashi ni za watu ambao hawakubahatika kwenda shule.

Na hata wao wenyewe wanaamini hivyo na hawataki watoto wao waje kurithi hizo kazi.Ingawa ni kazi ambazo jamii inazihitaji sana almost kila siku.

Hizi ni mindset za kijinga sana na kwa karine hii mindset za aina hii hazitakiwi, Hizi kazi tunazo zidharau ndizo hizo Wageni wanakuja wanakamata kwa kasi make hakuna ushindani, sisi na elimu zetu tushindane kufanya application za kazi.

Kama Fundi Selemara anaweza pata tenda ya kutengeneza milango ya mininga ya Hoteli ya million 500 anawezaje kuwa ni kazi ya waty ambao hawajaenda shule?Kuna Jamaa angu ni Fundu mbao na juzi kati kapewa hio tenda na ni moja ya mafundi wanao komaaa sana watoto wake waje kurith kazi zake.

Shida haiko kwenye hio kazi shida kuu ni mindset zilizo jengeka na ni mindset za kijinga sana, haya hizo za tai zinapotea tutaona.

Juzi nilitembelea Mzungu mmoja ni fundi selemara na anatengeneza fenicha very expensive sana, masikini kama sisi hatuwezi nunua hizo fanicha,nilicho furahi kutoka kwake ni kukuta binti yake na yeye ni fundi na wanasaidiana. Hii Bongo haiwezekani kabisa make kazi kama hizo ni za kijidhalilisha.

Hizi kazi tunazo ona ni za watu ambao hawajaenda shule ndizo zinalipa, hizo za kukaaa kwenye AC zinaisha au kupotea au kupungua sana. Time will tell
 
VETA ilidharaulika sana kuwa wanaojiunga huko ni wale waliofeli kuendelea na sekondari kumbe kwa sasa ni hot cake. Wahitimu wake wanatengeneza hela zisizo na ukomo. Kazi ni nyingi kila siku watu wanahitaji huduma
 
Ni ujinga tu wa baadhi ya WATZ wenzetu,kuna mafundi pale Keko wanauza fenicha hadi Comoro
 
Back
Top Bottom