Kidagaa kimemwozea
JF-Expert Member
- Jul 13, 2018
- 3,680
- 6,554
Ufaulu wa kukariri darasani ungetakiwa kuonyesha hapa kwa kutoa na kujenga Hoja.Kwanza yakiwekwa matokeo yangu na Yako kuanzia primary Hadi chuo kikuu nauhakika hakuna mahali utanikaribia Kwa ufaulu.
Wapi nimekwepa au nimesema mwanaume asihudumie Mkewe au familia yake. Bado unasema unaufaulu wa juu. Labda kama uliiba Papers. Lakini mtu yeyote ambaye hata hajaenda shule lakini zinachaji hawezi kufikiri kwa namna yako.Sitaki kuongea mengi.
Ni kwamba wewe hauna hela, na hoja zako hizi zinadhihirisha huna Hela na unakwepa jukumu la kumhudumia mke Kwa 100%. Mke ambaye manufacturer wetu kamuumba kama Kiumbe Cha kupokea tu, Leo unataka awe wa kutoa.
Mahari ni Mila potofu. Sio kwa mwanamke wala mwanaume ambaye anatakiwa kupewa wala kutoa.Unakoelekea utadai Wanawake wawe wanatoa MAHARI.
Hakuna raha ya Mama wa nyumbani zaidi ya kumgeuza mwanamke mtumwa na kumnyanyasa, akutegemee na ashindwe kuwa Huru kisa hana uwezo wa kujitegemea.Tafuta Hela Robert uwe tajiri utakuja KUJUA Raha ya mama wa nyumbani.
Hakuna Mwanamke anayefanya kazi huko kazini akawa salama.
Ukiona MTU anaongelea anawazidi wengine matokeo ya darasani mahali ambapo sio shule ujue huyo Ni kilaza namba 1 anatumia hiyo kujiwekea kinga
Umaskini kwenye nchi Yako hausababishwi na kina Mama wa Nyumbani.Mwanamke sio kiumbe Cha kupokea tu , Bali anapaswa ajitegemee. MTU asiyeweza kujitegemea Ni mtumwa. Na ndio wanasababisha umaskini katika nchi yetu. Je mwanamke asipoolewa atapokea wapi? Je mine wake akifa atapokea wapi?
Kwanini hukumshambulia wakati akiniita Mjinga?Ukiona MTU anaongelea anawazidi wengine matokeo ya darasani mahali ambapo sio shule ujue huyo Ni kilaza namba 1 anatumia hiyo kujiwekea kinga
Hamna mtu anayeingiza mshaahara mwenye hela , hela zipo kwa wafanyabiashara brotherUmaskini kwenye nchi Yako hausababishwi na kina Mama wa Nyumbani.
Hiyo ni mada nyingine.
Mme wake akifa anapokea kutoka Kwa vitega uchumi vya mume wake.
Ukweli ni kuwa Mleta mada Hana Hela Sasa anatafuta namna ya kujifariji.
Muulize kama anaingiza mshahara wa milioni 5 Kwa mwezi.
Mwanamke sio kiumbe Cha kupokea tu , Bali anapaswa ajitegemee. MTU asiyeweza kujitegemea Ni mtumwa. Na ndio wanasababisha umaskini katika nchi yetu. Je mwanamke asipoolewa atapokea wapi? Je mine wake akifa atapokea wapi?
Cha kufanya Robert tafuta Hela, hauna hela ndio sababu unawaza mke afanyie kazi.Hayo matokeo yake ndio aonyeshe uwezo wake wa kujenga Hoja hapa.
Wakina Kishimba hawajasoma na Bado wanaweza kujenga Hoja
Lakini Kuna jitu limemaliza Kodi za nchi na kusomeshwa mpaka chuo na Bado hata kujenga Hoja haliwezi.
Unamuuliza ikiwa mwanamke ni mtu kwa NINI asifanye kazi ya uzalishaji, anapuyanga.
Swali ambalo hata kijana wa darasa la Saba ambaye ana umeme wa kutosha kichwani anajibu vizuri tuu
Cha kufanya Robert tafuta Hela, hauna hela ndio sababu unawaza mke afanyie kazi.
HAUNA HELA NINA UHAKIKA.
Ukishaanza kuingiza milioni 5 Kwa mwezi ndio utaelewa Mwanaume Huwa anamchukuliaje mke wake.
Huna Hela kijana...
Umaskini kwenye nchi Yako hausababishwi na kina Mama wa Nyumbani.
Hiyo ni mada nyingine.
Mme wake akifa anapokea kutoka Kwa vitega uchumi vya mume wake.
Ukweli ni kuwa Mleta mada Hana Hela Sasa anatafuta namna ya kujifariji.
Muulize kama anaingiza mshahara wa milioni 5 Kwa mwezi.
Kwanini hukumshambulia wakati akiniita Mjinga?
Nimemjibu kuwa katika ujinga sipo Kwa ufaulu wangu tatizo liko wapi.
Sisi wengine ni chuma ulete hatuwezi kugonganisha vyanzo vya maokoto.KAZI NI ILE INAYOKUINGIZIA KIPATO. MAMA AU BABA WA NYUMBANI SIÔ KAZI KWANI HAKUNA KIPATO KINACHOZALISHWA.
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli
Amri ya Mungu ya kufanya Kazi. Inahusu kufanya Kazi za uzalishaji Mali, kujipatia kipato ili uweze kuishi.
Yàani Mûngu anapokuambia Fanya Kazi anamaanisha Fanya uzalishaji ili uweze kuishi. Kwani Asiyefanya Kazi Kula na asile.
Amri ya Kazi Ipo Kwa Wanadamu wote. Wakike na wakiume. Kwèñye jamii nyingi hasa zile Ambazo zîpo gizani kûna kasumba mbaya kuwa Mwanaume ndiye anatakiwa kufanya Kazi. Ilhali ukweli na Haki NI kuwa Watu wôte wanalazimishwa kufanya Kazi Bila kujali jinsia zào. Kazi za uzalishaji Mali, mapato.
Kwa nini lazima ufanye Kazi hata kama wewe ni Mwanamke;
1. Wewe ni MTU, ili Kulinda Ûtu wako
Mtu Asiyefanya Kazi z uzalishaji lazima utu wake uathirike. Lazima anyanyasike Kwa sababu atakuwa tegemezi.
Unaposikia Wanawake wananyanyaswa Moja Kwa Moja lazima uelewa ni kwèñye jamii na wale Wanawake wasiofanya Kazi. Huwezi mnyanyasa MTU anayejitegemea.
Hivyo unafanya Kazi ili uheshimike kama MTU.
Asiyefanya Kazi Kwa namna yoyote lazima adharaulike Bila kujali NI Mwanaume au Mwanamke.
2. ILI UMUABUDU MUNGU WAKO.
Kama hufanyi Kazi Huwezi kuwa unaabudu. Mungu anataka Zaka na Sadaka. Na elewa Zaka ni sehemu ya Kumi ya mapato yako siô mapato ya Mumeo. Mapato ya Mtu Mwingine (akiwepo Mumeo) akikupa ukayapeleka Kwa Mungu hayo huchukuliwa kama Sadaka na sio Zaka.
Elewa Mungu anabariki Kazi za mikono yako. Hapa inamaanisha Kazi za uzalishaji wako ili akupe riziki.
Unafanya Kazi ili usiende Kwa Mungu Mikono mitupu.
Kuonyesha kuwa Mungu aliibariki Kazi ya Mikono yako.
Mwanaume naye akienda atatoa Kulingana na alivyobarikiwa.
Kûna MTU atasema Ukiolewa au ûkioa mnakuwa Mwili Mmoja. Siô kwèli.
Kwa Mungu kîla MTU hulipwa yeye kama yeye na siô kimafungu. Kwamba Mungu hawezi kukuadhibu Kwa Makosa ya Mumeo au Mkeo. Pia Mungu hawezi kukubariki Kwa matendo ya Mkeo au Mumeo hiyo haipo.
Kushika Amri za Mungu NI Kwa Mtu mmoja mmoja.
3. ILI KUWA NA HAKI YA KUMILIKI MALI.
Nje ya Urithi na zawadi ambazo utolewa Kwa utashi wa Mtu. Sehemu pekee àmbayo MTU anahaki ya KUMILIKI Mali NI Kwa kufanya Kazi.
Mali yoyote àmbayo hujaifanyia Kazi na kuitolea jasho na haitokani na kipato chako siô Haki yako kisheria.
Kama NI Mali za Wazazi wako hizô siô zako.
Kama NI Mali za Mumeo au Mkeo hizô siô zako linapokuja suala la HAKI.
Zitakuwa zako Kama mwenye Mali Kwa hiyari Yake akaamua kukupatia akiwa yupo hai(zawadi) au akiwa amekufa(Urithi).
Kwèñye Ndoa zinakuwa Mali Zenu Kwa Sababu ya Ndoa ila nje ya Ndoa kîla mmoja atapewa alichochuma. Na hiyo ndîo HAKI.
NI dhulma kutaka KUMILIKI Mali isiyoyako. NI dhulma kama zilivyo dhulma ñyiñgine.
Kûna Amri inasema usitamani Mali ya jirani yako.
Unapotengana na Mkeo au Mumeo Mali zote Ambazo hukuzichuma siô Mali zako NI Mali ya jirani yako. Usizitamani.
Hakuwa jirani Kwa sababu alikuwa Mumeo au Mkeo lakini nje ya Ndoa huyo NI jirani kama walivyojirani Wengine.
Sheria kandamizi, Sheria nyonyaji, Sheria dhulmati zilizotungwa na Watu wasio na uelewa na mambo ya Haki huweza kumpa umiliki wa Mali MTU asiyestahili.
Kwa ujumla MTU anafanya Kazi ili ajitegemee na asipate Laana y kumtegemea MTU Mwingine.
Kwèñye jamii yetu kûna kasumba mbaya kuwa Mwanamke kuwa Mama WA nyumbani NI Kazi Jambo ambalo NI dhana potofu.
Dhana hiyo imeundwa kimakusudi kwa lengo la kukandamiza Haki hasa Kazi za Wanawake kujitegemea na kuishi Maisha halisi kama Nature inavyotaka.
Baadhi ya Wanaume huitumia dhana hiyo kama silaha ya kumuangamiza Mwanamke ili awe tegemezi na kumfanya awe mtumwa milele. Wanaume wanaotaka kuabudiwa kama mîungu. Kwa sababu anayekulea na kukulisha NI kama mungu wako.
Kwa mfano NI jamii àmbayo Wanawake ni tegemezi àmbayo Wanawake huweza kuolewa kimafungu(wake wengi) lakini jamii ya Wanawake wanaojitegemea hiyo NI ngumu.
KUoa Wake wengi NI unyanyasaji Mkubwa ikiwa Itafanywa pasipo hiyari ya Mwanamke husika.
Na Mwanamke tegemezi Hana hiyari Kwa sababu siô Mtu na Hana UTU.
Kupika chàkula chako au kwaajili ya familia yako haipo kwèñye orodha ya Kazi Kwa sababu unajitumikia mwenyewe.
Huwezi kupata kipato Kwa kujitumikia wewe mwenyewe.
Kufanya Kazi maana yake kutumikia Wengine ili wakulipe.
Huwezi kujifulia nguo zako au kumfulia Mtoto wako mdogo alafu ukaiita Kazi ilhali unajitumikia mwenyewe.
Huwezi kujipikia au kusafisha Vyombo au Nyumba unayoishi ukasema unafanya Kazi ya uzalishaji labda úwe na upeo mdogo..
Unaweza kufanya miradi ya familia na ukazalisha kipato Kwa kuwauzia Wengine.
Mfano unafuga Kuku WA familia lakini unauza mayai na Kuku Kwa Watu. Hiyo inaitwa Kazi.
Unalima shamba lako Kisha mazao unauzia Watu Wengine. Unajipatia kipato. Hiyo NI Kazi.
Kusema kuita majukumu ya Nyumbani NI Kazi ni matumizi Mabaya ya msamiati.
Ndîo maana ukikua Hapo kwèñu kama Huna Kazi hata kama unajishughulisha kuosha Vyombo lazima uambiwe utafute Kazi ya kufanya
Yàani Kazi ya kukufanya uishi. KAZI ya kukupa mahitaji yako.
Ndoa siô Kazi. Kuolewa siô KAZI
Kuzaa siô KAZI.
Kulea siô Kazi labda kulea Watoto wasiowako Kwa mkataba WA malipo yàani kuwa Yaya(babysitter) hiyo itaitwa Kazi
Na Huwezi kutaka ulipwe Kwa kujitumikia wewe mwenyewe.
Mfano ati kusafisha nyumba unayoishi au kulea Watoto wako alafu utake kulipwa hiyo siô Kazi.
Kama Huwezi ajiri MTU akulelee Mtoto mumlipe wewe na Mumeo.
Kûna wale wanasema Wanaume wanaotafuta Wanawake wanaofanya Kazi wamebweteka, au wavivu au mario. Wengine wanafika Mbali zaidi kuwaita mashoga.
Lakini hiyo NI mihemko ya Watu weñye upeo mdogo.
Waislam, Wayahudi na Wakristo wanaotumia Biblia na Quran na Talmud hii NI orodha ya Manabii na mitume na watu weñye majina makubwa kukuliko ambao wake zào walikuwa wanafanya Kazi(yaani wazalishaji)
1. Mtume Muhammad
Huyu alimwoa Bi. Khadija, mfanyabiashara. Muhammad alishauri kijana WA kiislam aoe Mwanamke Kwa vigezo vitatu àmbavyo NI Dini yake, Uzuri wake na Mali. Sasa Mwanamke atakuwaje na Mali kama hafanyi Kazi
2. Suleiman
Ñdipo akaandika Mithali 31
3. Isaka aliyemwoa Rebecca aliyekuwa anachunga Mifugo ya Babaake.
4. Yakobo aliyemwoa Raheli na Recho. Yakobo alimkuta Raheli akiwa anachunga Mifugo
5. Musa aliyemwoa Sipora. Sipora alikuwa anachunga
Watu wafanye Kazi
Binti yako kama hutaki kuabudu Watu na unàtaka kumwabudu Mungu kikamilifu lazima ameivya kufanya Kazi uitekeleze.
Mwanaume anayekuzuia usifanye Kazi ya uzalishaji huku akikukwambia ufanye ujitumikie yàani ufanye majukumu ya kifamilia na kuziita NI Kazi ilhali hujui unaingiza kipato kiasi gani. Huyo hafai. Hana Upendo WA kwèli. Hana Haki na NI mlaghai. Anataka uvunje Amri ya kufanya Kazi àmbayo siô Amri tuliyopewa Sisi Wanaume pekee Bali NI Amri ya wôte.
Kûna hoja ya Mwanaume ndiye aliyeumbiwa Kula Kwa jasho.
NI Sahihi lakini hiyo siô hoja ya kumfanya mwanamke asifanye Kazi.
Mwanamke afanye Kazi za uzalishaji Ambazo hazitamfanya atoe jasho(yàani ahangaike kupita kiasi).
Kumbuka Kabla ya anguko, agizo la Mungu lilikuwa Kulima Bustani na Kûitunza, hiyo NI Kazi walipewa lakini Mungu hakuweka laana ya kudanya kazi hizo kwa jasho.
Hivyo ndivyo utakavyoishi Kwa HAKI na kuzifurahia Siku zako zote utakazoishi Hapa Duniani Binti yàngu.
Acha nipumzike sasa.
Ijumaa Kareem, ñawatakia maandalizi mema ya Sabato
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Unajua wewe unatoka nje ya mada Yako, usiumizwe sana na ufaulu wangu kwakuwa hiyo ni Mali yangu.Kikwete Hana pesa ndio maana Salma ni Mbunge sio.
Tulia Mumewe Hana pesa sio.
Tax Mumewe hana pesa ndio maana anafanya kazi.
Kina Ummy mwalimu,
Kina Kamara waume zao hawana pesa ndio maana wanafanya kazi sio?
Alafu unaufaulu mkubwa😂😂
Ufaulu mkubwa haupo kwenye vyeti Mkuu. Ufaulu mkubwa unaonekana kwa mtu mwenyewe.
Sasa kama unafikiri Mke kufanya kazi ni kwa wanaume wasio na pesa na ulifaulu vipi kama usingesoma ungekuwa unawaza kwa namna ipi?
Nilitegemea kwenye huu mjadala ungeleta changamoto na kutetea kwa hoja upande wako ili kuwapa moyo wenye mtizamo kama wako lakini umekuja kujiabisha na kuwaangusha wenzako.
Zaidi umekuja kuwatia aibu mpaka Wasomi waliofaulu😅
Kwa hapo uko sahihi maana hata Mimi sitegemei mshahara mkuu...Hamna mtu anayeingiza mshaahara mwenye hela , hela zipo kwa wafanyabiashara brother
Unajua dogo Robert unaleta Dharau Sasa masuala ya matusi wakati tunabadilishana hoja Kwa hoja, kuwa makini...Atapokeaje kutoka kwenye miradi ambayo Haina usimamizi baada ya Mumewe kufa?
Hivi Mkuu akili yako umeme upo wa kutosha kweli?
Sikiliza Robert humu Jamiiforums kuna nyuzi ndugu zetu wameachishwa kazi ghafla na Wanawake wakahudumia familia Kwa muda mfupi na kuanzisha migogoro.Umeonyesha ujinga katika kujenga Hoja Mkuu.
Hilo la ufaulu umejidhalilisha kwa sababu kama ungekuwa unaufaulu mkubwa ungejadili kwa hoja zenye nguvu kama mtu aliyefaulu kweli.
Sasa wewe unaleta porojo za watu wajinga waliogizani kuwa ooh mwanamke kaumbwa kupokea, sijui anatakiwa kukaa nyumbani hivi tangu umezaliwa mpaka unafikia umri huo uliwahi kumwona msomi au mtu mwenye akili zinazochaji akaongea jambo kama hilo?
Watu wanaongea kitu kama hicho wapo makundi yafuatayo;
1. Wajinga wasio na elimu na Akili
2. Wenye mfumo dume Kandamizi
3. Wenye Mila Potofu
Sasa wewe hapo upo kundi gani?
Unajua wewe unatoka nje ya mada Yako, usiumizwe sana na ufaulu wangu kwakuwa hiyo ni Mali yangu.
Umesema mama wa nyumbani sio kazi.
Na ukaendelea kusema ni kwakuwa haiingizi Pesa.
Unaelewa ulichoandika?
Nikakuuliza mfanyakazi wa ndani unamlipa mshahara wa Nini ikiwa hiyo siyo kazi na haaingizi pesa?
Tofautisha watu kutafuta status kwenye jamii, ndiyo hayo mambo unayoongelea ya kina Kamala nk
Ni kwamba Mama wa Nyumbani ni kazi kubwa tu kama zilivyo kazi zingine, na inaingiza mapato ila kwakuwa wewe ni mvivu wa kufikiri, basi huoni...
Kaangalie CV ya Mke wake WA Kwanza na wapili uone analingana na huyo Mama WA nyumbani.Unajua dogo Robert unaleta Dharau Sasa masuala ya matusi wakati tunabadilishana hoja Kwa hoja, kuwa makini...
Nakutahadharidha....
Wewe hii post Yako nilokuquote ndio inathibitisha dhahiri hauna pesa mdogo wangu.
Wewe kama umeshindwa KUJUA biashara Huwa zinawekewa Mfumo wa kujiendesha utajuaje Mama wa Nyumbani ni kazi kama zingine?
Reginald Mengi alipofariki IPP imekufa?
Wewe huna Experience na maisha sio ajabu unatumia simu ya mkopo au mkeo amekupa zawadi.
Ni kwamba nimekwambia tafuta Hela ukishazipata utajua mentality ya Mume juu ya mke wake kuwa chini ya boss ikoje. Sawa?
Kama Mkeo umeme NI mdogo pia lazima akukubalie lakini Huwezi pata Mwanamke àmbaye kichwa kina gridi kûbwa ya taifa àmbaye anajielewa Akakubali awe mfuniko katika pipa lakoMimi siwezi ruhusu mke wangu kufanya kazi Kwa sababu Hilo jumba tunamoishi ndio kazi yake, na akiwa na tatizo lolote ama upande wa kwao ni jukumu langu.
Alafu tumia herufi rasmi katika maandishi yako maana huelewi.Wewe mwenyewe ndîo umeleta masuala ya kusema sikupati kwèñye ufaulu Sasa huo ufaulu wako ndîo uonyeshe Hapa na kujenga hoja.
Maswali yôte uliyouliza yanazidi kuonyesha hyo ufaulu wako unatoa Mashaka
Mfanyakazi wa Ndani unamlipa Kwa sababu anafanya majukumu yako wewe na hamna uhûsiano wowote.
Kufanya Kazi NI sehemu ya kujenga status ya Mtu yeyote íwe Mwanaume au Mwanamke.
Hadhi ya Mtu inajengqa na mambo meñgi mojawapo NI kufanya Kazi zinazoathiri jamii Kwa kuitumikia
Kwani ni Wanaume wangapi wanaofanya Kazi na wake zào hawafanyi Kazi na hao Wanaume wanawanyanyasa na kuanzisha migogoro kîla Siku Kwa Wake zào?Sikiliza Robert humu Jamiiforums kuna nyuzi ndugu zetu wameachishwa kazi ghafla na Wanawake wakahudumia familia Kwa muda mfupi na kuanzisha migogoro..
Embu naomba àndiko lolote kutoka Dini yoyote àmbayo muumbaji amesema Mwanamke asifanye Kazi. Àndiko Moja alafu Mimi nakuletea Mia Moja. Najua Hilo àndiko hutalipata kwèñye Dini yoyote hata Dini za zetu za kiafrika Huwezi Kuta hiyo kitu.Wewe unaleta ukinyume na maumbile Mimi nasimama upande wa muumbaji, ndivyo alivyoiweka Mwanamke Yuko upande wa upokeaji.
Sasa jambo dogo kama Hilo hujui utajuaje mengine?
Mimi Mila kweli wakati nasoma nilikuwa nazikataa ila ni miaka mi5 sasa nimezishika Mila kisawasawa.
Wewe furahia kuniita Mjinga hebu tuma cv Yako pm Jumatatu niikague nione kama inafaa kukuajiri maana naona njaa inakutesa sana kijana...