Kazi nyingi serikalini zinahitaji elimu ya form 4 na training ya miezi 6 tu, ndio maana wapo waliochakachua vyeti huwezi kuwagundua

round kick

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2025
Posts
345
Reaction score
1,145
Ndio maana hapo zamani watu walihitaji kuishia form 4 unaenda kupiga mzigo, vigezo vya elimu kubwa vinazdi kadri miaka inavyoenda lakini kazi nyingi zinahitaji training miezi 6 tu.

Mwanafunzi wa field yupo diploma anaweza kumpokeza kazi mfanyakazi mwenye mwenye masters, ila akiajiriwa elimu itambana afanye kazi za chini, sio kwamba hawezi kufanya kazi za degee / masters.

Kwenye majeshi hali inaweza kuwa mbaya zaidi tungeona mengi sana kama wangekaguliwa vyeti kipindi cha Magu
 
Hata Dunia haihitaji mavyeti mengi na madigrii Bali maarifa na ujuzi na upumbavu kiasi tuu
 
Huwezi kuwagundua vipi wakati vyeti vya miaka hii ni ngumu kuvichakachua? Vyeti huhakikiwa NECTA kama ni original or fake
 
Huwezi kuwagundua vipi wakati vyeti vya miaka hii ni ngumu kuvichakachua? Vyeti huhakikiwa NECTA kama ni original or fake
Wachakuachuaji nao wanaenda na muda, vyeti bado vinachakachulika.

Sehemu nyingi wanazoajiri wanaangalia cheti ulichonacho mkononi hawana mazoea ya kuhakiki.

Waliofukuzwa kazi kwa kuchakachua vyeti wamerudishwa upya makazini, watu wamepata morali ya kutumia vyeti vya kuchakachua, Ulinzi upo hakuna adhabu
 
Mwalimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam atakuwaje na elimu ya form four na training ya miezi sita halafu aje kumfudisha mwanafunzi wa shahada ya awali, shahada ya umahiri na shahada ya uzamivu?
 
Mwalimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam atakuwaje na elimu ya form four na training ya miezi sita halafu aje kumfudisha mwanafunzi wa shahada ya awali, shahada ya umahiri na shahada ya uzamivu?
Hio kazi ipo directly propotional na kusoma sana darasani

Ndio maana sijasema kazi zote, soma upya kichwa cha post
 
Hio kazi ipo directly propotional na kusoma sana darasani

Ndio maana sijasema kazi zote, soma upya kichwa cha post
Ukisema kazi nyingi unakuwa too general, maana utatajiwa kazi zinazohotaji walau shahada ya awali, utasema sijamaanisha hiyo. Labda ungeziorodhesha ili tukuonyeshe ni kwa nini zinahitaji shahada
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…