Wakuu
Huku Mbweni Mpiji maeneo ya Ungindoni wakiwa na sherehe zao za vigodoro ni kero kubwa, wanakesha usiku kucha na mziki ni mkubwa kiasi kwamba ni changamoto hata kupata usingizi. Mbali na hili ni hatari kwa watoto pia, ukienda kuchungulia mida ya saa tano sita usiku hukosi watoto, kwa watu wazima hamna tabu lakini hawa watoto wanakuwa exposed kwenye mambo ya ajabu sana, waliowahi kuona yanayofanyika huko wakati wa usiku wataelewa ninachosema.
Mbali na hilo, kuna pup ambayo ipo karibu na kanisa, jamani ni balaa, ni kero kwakweli. Kwenye pub wanasema wana kibali cha polisi kukesha. Polisi wanatoa vipi kibali cha watu kukesha kwenye makazi ya watu usiku kucha na hawana sound proof?
Nikaenda kupeleka malalamiko yangu katika ofisi ya serikali ya mtaa wakasema watalishughulikia lakini chochote walichofanya, weekend ni kama sikulala kwa makelele yale. Nadhani kuna rushwa inatolewa ili wafanye sherehe zao mpaka asubuhi, maana hatusikilizwi kabisa.
Soma Pia: Kelele usiku kucha Mtaa wa Alesika, Mbezi Beach kutoka Amigos Pub na Kanisa la Angels Ministry ni kero kubwa, tumechoka!
Sasa pata picha pub inapiga mziki, huku kigodoro kimechanganya, saa saba usiku kuna makelele utafikiri saa sabab mchana. NEMC mje mtupie jicho na huku na uongozi wa serikali ya mtaa uwajibike.