Kenya Abdallah Hassan, Katibu Mkuu wa kwanza Muislam Wizara ya Elimu, amefariki

Kenya Abdallah Hassan, Katibu Mkuu wa kwanza Muislam Wizara ya Elimu, amefariki

BlackPanther,
Mwenyezi Mungu amuongoze afanye kazi yake kwa uadilifu nchi ineemeka kutokana na elimu na ujuzi wake.

Black Panther hili jina umenikumbusha maisha yangu ya udogoni niko St. Joseph's Convent School hapa Dar es Salaam.

Miaka ile tukiwausudu sana Wamarekani na ilikuwa sisi ni watu wa kusoma magazeti ya Kimarekani Time na Newsweek, Ebony nk.

Wamarekani ni hodari sana kwa propaganda na wanajua kukamata bongo za vijana.

Sisi ilikuwa watu wa kusikiliza Soul Music - Wilson Picket, James Brown, Areth Franklin kwa kuwataja wachache.

Zile zilikuwa nyakati za wazimu khasa.

Tukiwausudu sana akina Huey Newton na Stokley Carmichael.
Na mengine mengi.

Umenigusa kidogo nilipoona umetumia hili jina.

Una memory kali haswaa mzee wangu 👏🏻👏🏻👏🏻tuko pamoja 😀
 
Back
Top Bottom