Kenya bado kidogo itakuwa nchi ya mfano kwa demokrasia katika Afrika

Kenya bado kidogo itakuwa nchi ya mfano kwa demokrasia katika Afrika

Alex Mbwilo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2013
Posts
351
Reaction score
290
Nimefuatilia siasa za Kenya toka wameanza kampeni za kupata viongozi katika 2017, kwa hakika hawa jamaa ukiondoa kitendo kimoja kibaya cha kuuawa kwa mfanyakazi wa tume ya uchaguzi nimewakubali wakenya.Hawa jamaa wanashindana kwa hoja. na mtazamaji ukiwasikiliza wagombea unawatofautisha bila shida yoyote. Kwamba unajua yupi anatete na yupi anataka kuingia.

Hapa kwetu huwa lazima ufanye kazi ya ziada ili ujue yupi anatetea na yupi anataka kuingia, na hii inachagizwa na kila mmoja kusema "nita". Katika kampeni za Kenya Uhuru anasema "nime" na hata wale wa ngazi za chini waliokuwepo madarakani wanasema "nime" wanaotaka madaraka wanasema "nita". Kitu kingine sijaona upande fulani kutumia dola kuhujumu upande mwingine na hata kulipo tokea rabsha za kuzomeana kwa kulipa kisasi walipogundua shida inayo wanyemelea viongozi wote walilizima hilo, jambo ambalo ni tofauti na nchi nyingine za Africa pale ambapo aliyekuwepo madarakani akiona anazidiwa hutumia dola kuhujumu upande shindani. Hii ni sawa na pale watu wawili wanapigana ngumi mmoja akiona anazidiwa anakimbilia kuchukua panga kwa matumizi dhidi ya mgomvi wake.

Siku Kenya wakiondoa jinamizi la ukabila wataziacha mbali nchi nyingi za Afrika kisiasa lakini pia kiuchumi.Uhuru ni mwanasiasa wa kweli pamoja na ushindani mkubwa kutoka kwa Raila huoni dhahiri kutumia dola na unamuona anaminyana kweli kweli arudi ofisini ingawa Raila amekomaa naye anataka kuingia ofisini.

Kenya wakirekebisha hizo kasoro kiduchu hatuwakuti, nawaombea wamalize kampeni kesho kutwa na wachaguane salama na waendelee na maisha. matokeo yasiwagombanishe na kwa mwelekeo kura zikipigwa, hesabiwa na kutangazwa washindi katika hali uhuru na haki wakenya watatoka wakiwa imara sana safari hii.TUWAOMBEEE
 
Siasa za kutegemea vyombo vya usalama ili usalie madarakani zilishawaghalimu, nasi tusipende mteremko kila kizuri kina gharama zake.
 
Kwa mauaj ya yule jamaa wa TUME YA UCHAGUZ

May Allah bless Me and You
 
Kwa hili la ukomavu wa kisiasa Kenya wametuacha mbali sana, kwetu unashindwa tofautisha chama kilichopo madarakani na dola
 
Kenya wako na Independent candidate ambao Tz hakuna licha ya marehemu Mch Mtikila kushinda kesi mahakamani. - -- Kenya wana Tume huru ya Uchaguzi, uundwaji wa tume upo huru. Haichaguliwi na Rais.
Matokeo ya chaguzi zote hutangazwa kituo cha kupiga kura. Tume hufanya majumuisho tu, pia vyombo vya habari vinaruhusiwa kufanya majumuisho.
Matokeo ya Uraisi na mengine yote yanahojiwa mahakamani.
Kenya ina mahakama iliyo huru kwasababu ya mchakato wa kuunda mahakama upo huru.
Wakuu wa mikoa {governers), na wilaya huchaguliwa na wananchi.
Kenya kuna mabunge mawili kama zilivyo nchi nyingi zenye ustawi.
Wabunge wanafanya kazi zao za kibunge za kusimamia serikali, hawaingizwi serikalini yaani kufanywa mawaziri.
Serikali kwa maana ya mawaziri hawatokani na wabunge na waziri akiteuliwa ni lazima apate confirmation ya bunge.
Raisi hana madaraka ya kifalme.
Wabunge wa viti maalum vya wananawake huchaguliwa na wananchi.
Na mambo mengi, hayo ni machache tu ya kujifunza.
 
Kenya wanatabia za kimagharibi waliwahi sana kujua maana ya freedom.
 
Kenya wako na Independent candidate ambao Tz hakuna licha ya marehemu Mch Mtikila kushinda kesi mahakamani. - -- Kenya wana Tume huru ya Uchaguzi, uundwaji wa tume upo huru. Haichaguliwi na Rais.
Matokeo ya chaguzi zote hutangazwa kituo cha kupiga kura. Tume hufanya majumuisho tu, pia vyombo vya habari vinaruhusiwa kufanya majumuisho.
Matokeo ya Uraisi na mengine yote yanahojiwa mahakamani.
Kenya ina mahakama iliyo huru kwasababu ya mchakato wa kuunda mahakama upo huru.
Wakuu wa mikoa {governers), na wilaya huchaguliwa na wananchi.
Kenya kuna mabunge mawili kama zilivyo nchi nyingi zenye ustawi.
Wabunge wanafanya kazi zao za kibunge za kusimamia serikali, hawaingizwi serikalini yaani kufanywa mawaziri.
Serikali kwa maana ya mawaziri hawatokani na wabunge na waziri akiteuliwa ni lazima apate confirmation ya bunge.
Raisi hana madaraka ya kifalme.
Wabunge wa viti maalum vya wananawake huchaguliwa na wananchi.
Na mambo mengi, hayo ni machache tu ya kujifunza.

Aise kama uliyoyaandika ni kweli basi wako vizuri...walifikaje huko.?Hata vyombo vyao vya habari utadhani vya mataifa ya magahribi.Yaani ukiangalia presenters wa kwenye TV zao tofauti kabisa na TV za Kitanzania.Wanachambua kweli mambo.
 
Wakenya walioishi nje wakarudi ni wengi mno. Washakua exposed na the free world sio hapa kwetu kuanzia juu tu jamaa hataki kusafiri hata mara moja, exposure zero, kunyima watu uhuru anaona ndiyo njia sahihi.

Kenya ni moja ya nchi chacha Afrika zinazoongoza kwa freedom, wanatumia reasoning na sio mazoea kwenye kuamua mambo, utaona wanafungua debates kwenye tv kubishana. Bongo hata debate watu waliitwa wakakwepa. Kazi kweli tunayo.
 
Subir uchaguz uishe ndio uje na uchambuz wako
 
Nimefuatilia siasa za Kenya toka wameanza kampeni za kupata viongozi katika 2017, kwa hakika hawa jamaa ukiondoa kitendo kimoja kibaya cha kuuawa kwa mfanyakazi wa tume ya uchaguzi nimewakubali wakenya.Hawa jamaa wanashindana kwa hoja. na mtazamaji ukiwasikiliza wagombea unawatofautisha bila shida yoyote. Kwamba unajua yupi anatete na yupi anataka kuingia.

Hapa kwetu huwa lazima ufanye kazi ya ziada ili ujue yupi anatetea na yupi anataka kuingia, na hii inachagizwa na kila mmoja kusema "nita". Katika kampeni za Kenya Uhuru anasema "nime" na hata wale wa ngazi za chini waliokuwepo madarakani wanasema "nime" wanaotaka madaraka wanasema "nita". Kitu kingine sijaona upande fulani kutumia dola kuhujumu upande mwingine na hata kulipo tokea rabsha za kuzomeana kwa kulipa kisasi walipogundua shida inayo wanyemelea viongozi wote walilizima hilo, jambo ambalo ni tofauti na nchi nyingine za Africa pale ambapo aliyekuwepo madarakani akiona anazidiwa hutumia dola kuhujumu upande shindani. Hii ni sawa na pale watu wawili wanapigana ngumi mmoja akiona anazidiwa anakimbilia kuchukua panga kwa matumizi dhidi ya mgomvi wake.

Siku Kenya wakiondoa jinamizi la ukabila wataziacha mbali nchi nyingi za Afrika kisiasa lakini pia kiuchumi.Uhuru ni mwanasiasa wa kweli pamoja na ushindani mkubwa kutoka kwa Raila huoni dhahiri kutumia dola na unamuona anaminyana kweli kweli arudi ofisini ingawa Raila amekomaa naye anataka kuingia ofisini.

Kenya wakirekebisha hizo kasoro kiduchu hatuwakuti, nawaombea wamalize kampeni kesho kutwa na wachaguane salama na waendelee na maisha. matokeo yasiwagombanishe na kwa mwelekeo kura zikipigwa, hesabiwa na kutangazwa washindi katika hali uhuru na haki wakenya watatoka wakiwa imara sana safari hii.TUWAOMBEEE
umetumwa kuisafisha kenya dhidi ya madudu yake ya uchaguzi, unajua kuwa kuna kikundi cha wagombea kilitangaza kuwa msemaji wa jeshi hajulikani alipo?nini maana yake?
 
Wakenya walioishi nje wakarudi ni wengi mno. Washakua exposed na the free world sio hapa kwetu kuanzia juu tu jamaa hataki kusafiri hata mara moja, exposure zero, kunyima watu uhuru anaona ndiyo njia sahihi.

Kenya ni moja ya nchi chacha Afrika zinazoongoza kwa freedom, wanatumia reasoning na sio mazoea kwenye kuamua mambo, utaona wanafungua debates kwenye tv kubishana. Bongo hata debate watu waliitwa wakakwepa. Kazi kweli tunayo.
kwa uchaguzi huu kenya wamefanya debate ngapi?
 
We jamaa bhaana.... mtu anakufa we unasema wanabishana kwa hoja...

Haujaijua kenya bado ...... wait uchaguzi uanze ndo utaleta mrejesho hapa... utaelewa wakikuyu... jaluo... kamba wana tabia gani....

Ni misenge iyo jamaaa..... muulize kofi anan na mkapa...

Sent from "La -Vista"
 
Back
Top Bottom