Kenya Election 2007: Outcomes

Ustaarabu gani wa kupigana kiberiti, haya nimauaji ya kimbari. Lazima Ban apeleke resolution UN, kibaki lazima aungane na charles tayler huko uholanzi. Raila na ECK waungane na jean minani ICTR, gakaka ziundwe maramoja.
 

....jamani mbona mnasahau wakenya wanapiga kura kwa line za ukabila na sidhani kama kikuyu wanafikiria wao ndio watawala wa Kenya au sasa wote ni guilty kwa sababu Kibaki ni kikuyu lakini kumbuka hata ODM kuna wakikuyu ,ni kweli Kikuyu ndio wameshika njia za uchumi na utajiri mwingi kutokana na tabia zao lakini sio serikali imewapa utajiri,Kenya ukabila ni order of the day na wanachukiana waziwazi ila hii fraud ya kibaki ndio imewapatia sababu ya kuchapa kikuyu lakini sabau kubwa kwa wengi ni chuki za kikabila na wala sio wizi wa kura maana kura kaiba Kibaki na cronies wake anakuja kuuawa mama na mtoto kule Eldoret,ndugu wakenya nawaonya mkianza kuua kikuyus msifikiri kikuyu watakaa kimya na wao watawaua tuu tena sana maana watakuwa na hasira ya revenge mmewaua ndugu zao and they will kill you with a passion na sasa hivi wana serikali na wengi wao wana pesa sana,bora sasa mgundue mbaya sio kikuyu ila ni serikali ya Kibaki na muungane mumtoe ila mkiua kikuyu tuu mjue kitakachofuata is a full scale war!
 

mimi kwa maoni yangu nadhani viongozi wa Africa hawana lolote they were behind Mugabe wakati they very well know that he is a dictator. Na marais wa EAC wana neutral stand hawataki kuonekana wanampendelea mtu yeyote, Tz ilikuwa kama vile wanashabikia ushindi wa kibaki kuitia maripota wa TVT ila pressure ya opposition ilipobana wakaona mambo yanaweza kubadilika sasa kuna neutral stand.
 
"Many Kenyans have been taking refuge from armed mobs and looters as fears mount of further attacks and reprisals."

"The African Union chairman is due in Kenya, as the US and UK add their voices to AU calls to end the violence."

Mh, yaani mpaka Rice na Brown waseme ndio AU wachangamke, Siamini kuwa Condoleeza Rice is more concern kuliko AU. Mbona viongozi wote africa wameduwaa, kweli kichaa huyu wengi walikuwa wanamzini sasa kichaa mwenzie kawaona nae anataka kumzini atamkataza nani?
 

Hayo ni mambo yanayoenezwa zaidi na wageni wa magharibi. Ukiangalia kwenye uchaguzi huo utagua kuna wakikuyu wengu tu na makabila mengine waliompigia kura Odinga, sio waluo peke yao. ndio majority, if it was in tribal lines for sure Odinga would have lost, and if Kibaki would have won he wold have had a landslide. Kuuana ni ujinga kabisa whether mkikuyu anaua mluo au mluo anaua mkikuyu, lakini sio vizuri kushughulikia symptoms na kuacha mzizi wa tatizo. Hiyo ni stupid way of postponing a problem inayotumiwa na viongozi wetu wa nchi nyingi kama Zimbabwe, sasa Kenya, Somalia etc.
 
Mzee Bongolander,
Naona huifahamu historia ya Kenya tangu 1963. Ukabila ulianzia huko na kundi lililomzunguka Kenyata. Matunda yake miaka yoote hii ndiyo tunayavuna sasa.
 
Mimi mawazo yangu ni kwamba tatizo hapo naliona kwenye electoral law inayoruhusu simple majority.Kwa uchaguzi huu wa Kenya,ilitakiwa first na second wachuane kwenye round ya pili baada ya siku 21. Hali hii wangeweza kumpata mshindi halali ambaye ana mandate ya watu wengi kama alivyopatikana rais wa Liberia Madame Hellen Sirleaf. Kwa mfano Liberia wangetumia mfumo wa Kenya,George Weah angekuwa Rais. Naomba waafrika wenzangu kuboresha katiba zetu,ili kupunguza nguvu ya taasisi ya Urais ili kuepusha wanasiasa waroho kusababisha machafuko.
 
Mimi mawazo yangu ni kwamba tatizo hapo naliona kwenye electoral law inayoruhusu simple majority.Kwa uchaguzi huu wa Kenya,ilitakiwa first na second wachuane kwenye round ya pili baada ya siku 21. Hali hii wangeweza kumpata mshindi halali ambaye ana mandate ya watu wengi kama alivyopatikana rais wa Liberia Madame Hellen Sirleaf. Kwa mfano Liberia wangetumia mfumo wa Kenya,George Weah angekuwa Rais. Naomba waafrika wenzangu kuboresha katiba zetu,ili kupunguza nguvu ya taasisi ya Urais ili kuepusha wanasiasa waroho kusababisha machafuko.
 
Kwa kadri siku zinavyozidi kusonga mbele ndivyo mambo yanazidi kujiweka wazi zaidi na labda kutoa picha halisi ya wizi wa kura.

Makamishina 4 wamekiri kwamba kulikuwa na kasoro ambazo zilitolewa na vyama husika, lakini wakaweka pamba masikioni.

Mzee Kivuitu hatimaye jana kaongea na huku akiwa anasikika kama mtu mwenye jazba na woga, akasema wao kama ECK hawana kosa, walisoma kile walicholetewa kutoka kwenye majimbo. Lakini akakiri kwamba kuna baadhi ya majimbo ambayo yalikuwa na utata na hasa watu wa EU waliposema kwamba mbona figure iliyosomwa kwenye jimbo iko tofauti na ile ambayo imesomwa na wao ECK. Huyu jamaa hakusikiliza hiyo hoja, bali jana ndiyo kaiongelea eti ilimshitua, kwanini hakushituka tangu siku alipotangaza matokeo?

Kulikuwa na dalili zote za ukora wa kura na hasa baada ya kucheleweshwa kura kutoka majimboni na wahusika kuzima simu. Hizo zilikuwa dalili tosha kwamba watu walikuwa wanatengeneza matokeo, na hata yeye alisema kwamba labda wanaweza kuwa wanatengeneza matokeo! Kwanini hakuchukua hatua za haraka ili ajiridhishe kwamba data alizopewa zilikuwa ni sahihi kwa kuomba masanduku ya kura yahesabiwe upya ili kujua ukweli wa mambo? Pamoja na kelele zote za wapinzani pale KICC huyu mzee hakutaka kuwasikiliza na akaja kufanya alichojua yeye.

Amesema alishinikizwa kutangaza matokeo, lakini nakumbuka pia alishinikizwa asitangaze matokeo pale KICC lakini kwa jeuri aliyo nayo aliendelea kutangaza pamoja na makelele ya watu. Iweje akubali kushinikizwa na PNU lakini asikubali kushinikizwa na ODM? Huyu jamaa kweli yuko fair? Above all EU na watu wa human rights wa Kenya waliomba aahirishe kutangaza matokeo, lakini bado akaendelea kufanya hivyo! Je, jamii ya wakenya iendelee kuwa na imani na mtu kama huyu aliyeahidi kuacha legacy nzuri? Ninadhani ataondoka na aibu yake kwa kushindwa kutenda haki huku akijua wazi kwamba hakutimiza wajibu wake, may be alikuwa anasema kwamba kwa kuwa jamaa ni wapinzani hawawezi kufanya lolote zaidi ya kulalamika.

Swala jingine, hivi ni kwanini kila mara alikuwa akisema kwamba mtu asiporidhika na matokeo, aende Mahakamani ambako ni upande wa pili wa barabara, huko ndiyo haki itatendeka. Jana kasema ECK ikigundua kuna tatizo kubwa itaenda yenyewe mahakamani, swali ni kwenda kufanya nini? Kwenda kujishitaki wenyewe kwamba hawakutenda haki? Hata kama akienda mahakamani naona ni sawa na kesi ya nyani kuipeleka kwa nyani mwingine!

Kwa aliye na ufahamu wa wazo la wale makamishina 4, kwamba iundwe Judicial Commission of Inquiry, inaundwa na idara ya mahakama ama na watu gani? Ni nani anateua hao watakao unda hiyo tume? Ni Kibaki ambaye ni mtuhumiwa au ni nani anateua hiyo tume?

Naona mwisho wa siku Raila ataishia kupoteza kwa jinsi mazingaombwe ninavyoona yanaendelea kujitokeza. Ngoja tusubiri akina Tutu, JK, M7, Kufour na wengineo watafikia muafaka gani kwenye hii kadhia.
 
Naomba waafrika wenzangu kuboresha katiba zetu,ili kupunguza nguvu ya taasisi ya Urais ili kuepusha wanasiasa waroho kusababisha machafuko.

Tutarekebishaje katiba wakati walio madarakani hawataki katiba zirekebishwe, maana zikirekebishwa ndiyo utakuwa mwisho wa utawala wa kurithishana. Mojawapo ya sababu zilizomfanya Raila atofautiane na Kibaki ni hilo swala la katiba.
 
Hivi Kalonzo kapotelea wapi? Ni kama yeye ana nafasi kubwa ya kusaidia kwenye hili suala.

Nasikia Kalonzo ni mlokole? Jamaa inaelekea alikuwa anataka kuwa makamu wa rais.
 
Hivi Kalonzo kapotelea wapi? Ni kama yeye ana nafasi kubwa ya kusaidia kwenye hili suala.

Nasikia Kalonzo ni mlokole? Jamaa inaelekea alikuwa anataka kuwa makamu wa rais.

Lazima ataukwaa tu, maana sina hakika kama anaweza kuingia kwenye coalition govt bila ya kuahidiwa nafasi nono (including u-VP).

Nimesikitishwa na kitu kimoja kwamba vile viti 12 vya wabunge wa kuteuliwa siyo sheria, bali yalikuwa ni makubaliano tu. Kwa hiyo kuna hisia kwamba kwa kuwa Kibaka amepata viti 35 tu, anaweza kuvichukua viti vyote 12 akateuwa watu wake ili awape nafasi za uwaziri.

Katiba za nchi za Afrika zina mambo! Niliwacheka Malawi wakati Bingu anaki-dump chama kilichomuingiza Ikulu na kuunda chama kipya. Katiba ya Malawi ilikuwa haiongelei lolote kama Rais akijivua uanachama, lakini mbunge akijivua na ubunge anapoteza. Sasa ndiyo haya ya Kenya!
 
Kibaka amewaalika wabunge waliochaguliwa kwenda Ikulu leo hii saa 9 alasiri.

Hili litakuwa ni jaribio la kwanza kuona ni wabunge wepi wa upinzani wanamuunga mkono na wepi hawamtambui. Kweli wezi huwa wana mikakati ya ajabu sana. Sasa Ikulu anawaita kwenda kufanya nini?????
 

Mawazo mazuri sana haya. katiba yetu (TZ) ndivyo ilivyokuwa siku zote, lakini katika utawala wa Mkapa wabunge wetu walibadilisha na sasa tunaruhusu simple majority. Ndio watu wengine wanauliza sisi tunaendelea au tunazidi kwenda nyuma? Waafrika tutaendelea kuishi kwa kudra za mwenyezi Mungu, ustaarabu inaonekana hatuuwezi kabisa!
 
Hivi Kalonzo kapotelea wapi? Ni kama yeye ana nafasi kubwa ya kusaidia kwenye hili suala.

Nasikia Kalonzo ni mlokole? Jamaa inaelekea alikuwa anataka kuwa makamu wa rais.

Tatizo moja la wenzetu wakenya wanapenda mno madaraka na vyeo at any expense; huyu kama ameadiwa u-VP atakuwa tayari ku-compromise kila principe. Isingekuwa kupenda kwao madarakani wangemtoa Kibaki kupitia bungeni kiulaini kabisa, lakini kwa kupenda kwao vyeo, Kibaki ana uwezo wa kuwahonga vyeo wabunge kibao kiasi kwamba mwisho wa siku ODM itakuwa haina majority, ni balaa sana. Wote tunapenda madarakani hata TZ, lakini hawa wenzetu wamezidi kwa kweli.
 
K-T Hivi huyu jamaa michuki minister wa security kenya does he really have that powers to be in office at this juncture maana. i find it ironical for him to be ordering while he was voted out in his constituency. does he have a scandal that he is protecting at any cost maana he is very active to ensure that everything settles.
 

Hata mimi nimesikia hivyo juu ya hili la viti 12. Hapo kuna kasheshe kubwa sana.

I hope watawala wetu wanaona na watajifunza kwamba ni muhimu kweli mwaka huu
tuiangalie upya katiba yetu kwa faida ya nchi yetu, sisi wenyewe na vizazi vyetu.
 
kuanzia leo mimi jina la kibaki nitaliandika kuanzia na herufi ndogo (small letters) maana simuheshimu tena.
 
Hata mimi nimesikia hivyo juu ya hili la viti 12. Hapo kuna kasheshe kubwa sana.

I hope watawala wetu wanaona na watajifunza kwamba ni muhimu kweli mwaka huu
tuiangalie upya katiba yetu kwa faida ya nchi yetu, sisi wenyewe na vizazi vyetu.

Hawa unaowaita watawala wetu si mpaka walione hili. Watu wengi kule home wanafikiri tatizo la Katiba na Tume ya Uchaguzi ni mambo yanayowahusu upinzania; ndio maana NGOs na taasisi zingine za kiraia hazijihusishi sana na madai ya haya mambo. Pengine kuna haja ya kuwahamasisha na kuwashnikiza taasisi kama hizi pamoja na za dini kushiriki kikamilifu kudai Katiba bora kwa nchi yetu
 
kuhusu katiba kwa nini tusitumie mfumo wa uingereza kwenye uchaguzi kuwa chama kinacho pata wabunge wengi ndio kinaunda serikali ili kuondoa utata ktk kumpata raisi.hii itasaidia ktk kudhibiti wizi wa kura,kwani kila jimbo litakuwa makini ktk kehesabu kura na kutoa matokeo yake kwa uhakika kuliko kusubiri kurazihesabiwe tz yote ilikumpata rais
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…