Kenya ilipigania uhuru wake. Tanzania ilipewa uhuru bure na Mbeberu

Kenya ilipigania uhuru wake. Tanzania ilipewa uhuru bure na Mbeberu

Ndio, vita vya Mau Mau ndio viliipa Kenya Uhuru. Mkoloni alilazimika kuwakubalia waafrika weusi wajipange kisiasa kupitia vyama vyao kwasababu ya vita vya Mau. Chama cha KADU kiliamrishwa kitengeneze serikali kabla ya Uhuru. Kama njia ya mkoloni kujaribu kuingiza migawanyiko na usaliti kwa chama cha KANU ila wakaibuka na kauli kwamba lazima Kenyatta na wenzake(Kapenguria Six) waachiwe huru kwanza. Vita vya Mau Mau vilikuwa 'Guerilla War', yaani kama vya waasi ambao huwa wanampiga adui yao kisha wanarudi mafichoni. Harasa ilikuwa ni kwa mkoloni, kihali, kimali, kiraslimali kupitia usumbufu ambao ulifanya koloni lake liendeshwe kijeshi, bila mpangilio, bila amani, bila faida.
blablaablaablaa.....why 63 and not 56?
 
View attachment 1639768

HAPA NDIO UJUE NYIE MLIKUWA WATUMWA NA MNAENDELEA KUWA WATUMWA TU KWA MABEBERU

NJOO TZ KAMA UTAPATA HII UJINGA???
Unajua kwanini mkoloni alilazimisha kwa fujo kwamba waafrika lazima wabebe hizo pass? Kwasababu ya wasiwasi wake kuhusu usalama wake. Maanake walidai kwamba wakenya ambao walikuwa na nia ya fujo za kumfurusha mkoloni hawakustahili kukubaliwa kusafiri watakavyo ndani ya koloni lao. Yaani kwa ufupi mkoloni alikuwa na uoga mkubwa sana kuhusu majasusi na wapiganaji wa Mau Mau.
 
Kwani hiyo Vita ya Mau Mau ilitoa uhuru kwa Kenya?!

Au unatakiwa kukumbushwa kwamba Mau Mau Uprising iliisha somewhere in 1956-1957 wakati Kenya Ilipata uhuru wake 1963?!
Mwaka wa 1958 mzungu aliweka timetable ya independence. Alianza kulegeza kamba baada ya vita vya mau mau. Akakubali wabunge waafrika kuchaguliwa. Akakubali political parties kuundwa. Akakubali mikusanyiko ya kisiasa.

Halafu baadaye akakubali kuachilia wafungwa wa kisiasa kama Jomo Kenyatta. Halafu mwisho kabisa akakubali waafrika waende Uingereza kuunda katiba mpya katika Lancaster conference. Haya yote yalifanyika baada ya vita vya mau mau.
 
Hata Kenya ilipewa pia acheni kujidanganya, Muzungu aliondoka Kenya na Afrika kwa hiari, ...
Mzungu hangeondoka Kenya bila vita vya MauMau. Churchill mwenyewe alipokuwa UK prime minister alisema kwamba hatatupa uhuru kamwe. Na akaamrisha jeshi zaidi liletwe Kenya kupambana na Maumau. Mabomu yakatupwa kwenye maficho ya Maumau. Sasa baada ya vita kuisha ndio mzungu akakubali vyama vya kisiasa kuundwa. Akakubali wabunge waafrika kuchaguliwa. Akakubali mchakato wa kisiasa kuanza.
 
blablaablaablaa.....
why 63 and not 56?
Uhuru tungepewa vipi 56 kama hata vyama vya kisiasa vilikuwa vimepigwa marufuku na viongozi wa kisiasa kutiwa korokoroni? Ilibidi mzungu aanze kufungua political space polepole kwa kuruhusu vyama vya kisiasa kuanzishwa. Kuruhusu uchaguzi kufanyika na wabunge wa kiafrika kama Tom Mboya, Jaramogi Odinga na Moi kuchaguliwa katika Legco. Mwishowe akawachilia Viongozi kama Mzee Kenyatta ambaye alikuwa amefungwa kwa miaka karibu kumi.

Yaani kwa sababu mzungu alikuwa ameangamiza uhuru wa kufanya siasa kabisa, ilibidi aanze kututayarisha pole pole kupata uhuru. Kama angetupatia uhuru 1957 basi Kenya hatukuwa na kiongozi yeyote ambaye angeweza kuutwa madaraka. Wengi walikuwa korokoroni na wengine kama Moi na Odinga hawakuwa na umaarufu sana kwa sababu hawakuwa wameruhusiwa kugombea kiti cha ubunge.

Lakini baada ya wao kuchaguliwa kuwa wabunge ndio umaarufu wao ukaongezeka na mzungu akapanga Jaramogi Odinga ndiye awe Rais wa kwanza wa Kenya 1961 lakini Odinga akasema Kenya haitapata Uhuru hadi Kenyatta aachiliwe kutoka gerezani.
 
Uhuru tungepewa vipi 56 kama hata vyama vya kisiasa vilikuwa vimepigwa marufuku na viongozi wa kisiasa kutiwa korokoroni? Ilibidi mzungu aanze kufungua political space polepole kwa kuruhusu vyama vya kisiasa kuanzishwa. Kuruhusu uchaguzi kufanyika na wabunge wa kiafrika kama Tom Mboya, Jaramogi Odinga na Moi kuchaguliwa katika Legco. Mwishowe akawachilia Viongozi kama Mzee Kenyatta ambaye alikuwa amefungwa kwa miaka karibu kumi.

Yaani kwa sababu mzungu alikuwa ameangamiza uhuru wa kufanya siasa kabisa, ilibidi aanze kututayarisha pole pole kupata uhuru. Kama angetupatia uhuru 1957 basi Kenya hatukuwa na kiongozi yeyote ambaye angeweza kuutwa madaraka. Wengi walikuwa korokoroni na wengine kama Moi na Odinga hawakuwa na umaarufu sana kwa sababu hawakuwa wameruhusiwa kugombea kiti cha ubunge.

Lakini baada ya wao kuchaguliwa kuwa wabunge ndio umaarufu wao ukaongezeka na mzungu akapanga Jaramogi Odinga ndiye awe Rais wa kwanza wa Kenya 1961 lakini Odinga akasema Kenya haitapata Uhuru hadi Kenyatta aachiliwe kutoka gerezani.
So tukubaliane nyie pia mlipewa uhuru wa bure, maana mlkua hamna ubavu wa kupambana nae wenyewe kama kenya alone?

Wivu tu, kwan mltakaje labda?
 
Ninarudia tena. Tanzania haikusaidia Kenya kupata Uhuru. Tuliunyakua uhuru wenyewe kutoka kwa mikono ya beberu kwa kupigana hadi kufa. Tulimwaga damu ili tupate uhuru wetu. Nyie hamkutusaidia kwa lolote.
ah ah mlivyomtoa mkoloni mweupe mkaja mweka mkoloni mweusi mama ngina na kenyata...akimiliki robo ya ardhi na wengine toka enzi za maumau bado wanaishi kwe squarters.
 
so tukubaliane nyie pia mlipewa uhuru wa bure.
maana mlkua hamna ubavu wa kupambana nae wenyewe kama kenya alone?

wivu tuu kwan mltakaje labda?
Tulimlazimisha kutupatia uhuru. Mwaka wa 1952 mzungu alisema kuwa atatawala Kenya milele. Prime minister Churchill alituma jeshi Kenya ili kuangamiza mchakato wa waafrika kutafuta Uhuru. Baada ya vita mzungu ndiye aliyebadilisha msimamo wake na akakubali kutupatia uhuru.

Kwenye vita mshindi ni yule ambaye anapata kitu ambacho alikuwa anakipigania. Sisi tulipigana kwa sababu tulitaka uhuru na mwishowe mzungu akakubali kutupatia. Mzungu naye alipigana ili aendelee kutawala Kenya milele ila mwishowe yeye mwenyewe aligundua kuwa hawezi kuitawala Kenya milele na akakubali kutupatia uhuru.
 
Mzungu hangeondoka Kenya bila vita vya MauMau. Churchill mwenyewe alipokuwa UK prime minister alisema kwamba hatatupa uhuru kamwe. Na akaamrisha jeshi zaidi liletwe Kenya kupambana na Maumau. Mabomu yakatupwa kwenye maficho ya Maumau. Sasa baada ya vita kuisha ndio mzungu akakubali vyama vya kisiasa kuundwa. Akakubali wabunge waafrika kuchaguliwa. Akakubali mchakato wa kisiasa kuanza.

Blah blah, Muzungu aliondoka Afrika kwa sababu muda ulikuwa umefika, na kulikuwa na sababu za kiuchumi kwanza ilikuwa ni expensive sana kwa Muzungu kuendesha haya Makoloni kwani tayari Muzungu (Europe ) alikuwa bankrupt, hizo infrastructure zote zilizo Nairobi, Mombasa na kwingineko ni Muzungu alijenga kwa kutumia pesa yake na ilikuwa ni expensive projects ambazo ilikuwa hailipi, sababu ya pili USA kama global power mpya baada ya WW 2 alishasema no more colonies pamoja na kuanzishwa kwa UN 1945, hiyo ndiyo sababu lkn siyo ujinga wa sijui Mau mau, mau mau ilikuwa ni uprising tu ambayo kama Muzungu angetaka kuendelea kubakia angeizima mara moja.

Labda ungejiuliza kwa nini nchi za Kiafrika (Kusini mwa Sahara ) karibia zote zimepata Uhuru wake wakati mmoja in the 1960 's ? Kwa nini siyo kabla ya hapo ? Na kwa nini zote kwa karibia wakati mmoja ? Unafkiri imetokea tu ? Kama Muzungu aliondoshwa na Maua Mau kwa nini itokee miaka ya 60 ambapo nchi zote zilipata Uhuru wake ?

BTW Muzungu ameondoka China (Hong Kong ) mwaka 1997, sasa unafikiri kwa nini amechelewa hivyo ?
 
Na hapo ndo uone tofauti kati ya Tanganyika na Kenya!!!

A moment colonists set their feet in Tanganyika, Mababu zetu waka-react!!
Hujui lolote kuhusu historia ya Kenya na vita dhidi ya mkoloni. 'Earliest resistance' dhidi ya mkoloni Afrika mashariki ilikuwa kutoka kwa shujaa Chifu Waiyaki wa Hinga(Southern Kikuyus), mwaka wa 1898. Ambapo alitia moto makao makuu ya mkoloni maeneo ya Kiambu.

Unajua kuhusu vita vya Mekatilili Wa Menza(Giriama Resistance) dhidi ya mkoloni? Hiyo ilikuwa miaka ya 1870-1920(zaidi ya miongo mitano). Nandi Resistance ya Koitalel Arap Samoei(1890-1906)? Mloloni alitumia ugonjwa wa Small Pox ili kuzima moto wa Koitalel baada ya kuchoshwa na vita vya miaka zaidi ya 15. Soma historia kabla ya kukurupuka na kutuimba chorus za mchawi Kinjeketile Ngwale na maji yake 'bullet proof'.
 
Blah blah, Muzungu aliondoka Afrika kwa sababu muda ulikuwa umefika, na kulikuwa na sababu za kiuchumi kwanza ilikuwa ni expensive sana kwa Muzungu kuendesha haya Makoloni kwani tayari Muzungu (Europe ) alikuwa bankrupt, hizo infrastructure zote zilizo Nairobi, Mombasa na kwingineko ni Muzungu alijenga kwa kutumia pesa yake na ilikuwa ni expensive projects ambazo ilikuwa hailipi, sababu ya pili USA kama global power mpya baada ya WW 2 alishasema no more colonies pamoja na kuanzishwa kwa UN 1945, hiyo ndiyo sababu lkn siyo ujinga wa sijui Mau mau, mau mau ilikuwa ni uprising tu ambayo kama Muzungu angetaka kuendelea kubakia angeizima mara moja.

Labda ungejiuliza kwa nini nchi za Kiafrika (Kusini mwa Sahara ) karibia zote zimepata Uhuru wake wakati mmoja in the 1960 's ? Kwa nini siyo kabla ya hapo ? Na kwa nini zote kwa karibia wakati mmoja ? Unafkiri imetokea tu ? Kama Muzungu aliondoshwa na Maua Mau kwa nini itokee miaka ya 60 ambapo nchi zote zilipata Uhuru wake ?

BTW Muzungu ameondoka China (Hong Kong ) mwaka 1997, sasa unafikiri kwa nini amechelewa hivyo ?
Sasa unataka kulazimisha facts zako za uchwara?
 
Tanzania iliwekwa chini ya muingereza kwa mkataba maalumu.sisi tulikuwa koloni la mjermani
Halafu mjerumani alivyo fala akashindwa hata kukifanya kigermany kuwa ndio lugha rasmi kwa makoroni yake
 
Blah blah, Muzungu aliondoka Afrika kwa sababu muda ulikuwa umefika, na kulikuwa na sababu za kiuchumi kwanza ilikuwa ni expensive sana kwa Muzungu kuendesha haya Makoloni kwani tayari Muzungu (Europe ) alikuwa bankrupt, hizo infrastructure zote zilizo Nairobi, Mombasa na kwingineko ni Muzungu alijenga kwa kutumia pesa yake na ilikuwa ni expensive projects ambazo ilikuwa hailipi, sababu ya pili USA kama global power mpya baada ya WW 2 alishasema no more colonies pamoja na kuanzishwa kwa UN 1945, hiyo ndiyo sababu lkn siyo ujinga wa sijui Mau mau, mau mau ilikuwa ni uprising tu ambayo kama Muzungu angetaka kuendelea kubakia angeizima mara moja.

Labda ungejiuliza kwa nini nchi za Kiafrika (Kusini mwa Sahara ) karibia zote zimepata Uhuru wake wakati mmoja in the 1960 's ? Kwa nini siyo kabla ya hapo ? Na kwa nini zote kwa karibia wakati mmoja ? Unafkiri imetokea tu ? Kama Muzungu aliondoshwa na Maua Mau kwa nini itokee miaka ya 60 ambapo nchi zote zilipata Uhuru wake ?

BTW Muzungu ameondoka China (Hong Kong ) mwaka 1997, sasa unafikiri kwa nini amechelewa hivyo ?
Muingereza alitia mkataba na China kuwa ataitawala Hongkong kwa miaka mia moja. Hii ni baada ya Muingereza kumshinda Mchina katika vita waliyokuwa wakipigana. Baada ya muda huu wa miaka mia moja kuisha Muingereza akairudisha Hong Kong kwa Uchina kama ambavyo mkataba ulivyosema. Muingereza hakuwa na option maana Mkataba aliotia saini ilisema lazima arudishe Hongkong baada ya muda fulani. Sasa huwezi kulinganisha Hong Kong na Kenya
 
Sasa unataka kulazimisha facts zako za uchwara?

Sijalazimisha popote ila nimeuliza maswali ambayo ungeyajibu kama ukipenda/weza, usiamini kila kitu unachoambiwa kirahisi hivyo tumia logic yako kufikiri, Dunia iko complicated zaidi, una amini kabisa wale wacheza reggae rastamen Mau Mau wenye mishale na mikuki walikuwa na uwezo wa kuishinda Royal British Army ? Siajabu pia unaamini kwamba Mandela aliondoa apartheid AK, au ?
 
Muingereza alitia mkataba na China kuwa ataitawala Hongkong kwa miaka mia moja. Hii ni baada ya Muingereza kumshinda Mchina katika vita waliyokuwa wakipigana. Baada ya muda huu wa miaka mia moja kuisha Muingereza akairudisha Hong Kong kwa Uchina kama ambavyo mkataba ulivyosema. Muingereza hakuwa na option maana Mkataba aliotia saini ilisema lazima arudishe Hongkong baada ya muda fulani. Sasa huwezi kulinganisha Hong Kong na Kenya

Kwa nini unafikiri Muzungu aliweka mkataba na China na siyo Kenya ? Au Kenya pia kulikuwa na Mkataba ?
 
Ni ukweli kabisa, kilichoipumbaza Tanzania ni uhuru wa kupewa bila kutumia nguvu

Kenya na nchi nyingine zilipigania uhuru kwa nguvu hata kama Tanzania ilienda kusaidia kijeshi lakini hakuna vita vya kidai uhuru Tanzania mwenye historia alete hapa.

Machifu ndio walikua wanapigana na sio Tanzania kwa ujumla, watz tuache ushabiki mandazi, ndio maana mpaka leo CCM inatuona mabumbunda na hatuna cha kuwafanya
Watu wenye fikra kuwa Uhuru wa Tanganyika ulipatikana bila ya kumwaga damu, ni mazalia ya kizazi kipya ambacho kimejazwa historia potofu iliyotungwana jopo lililoongozwa na Pius Msekwa, baada ya Uhuru kwa kuagizwa kufanya hivyo na TANU, kwa madai kuwa historia iliyokuwepo iliandikwa na wakoloni kwa mtazamo wa kikoloni.

Kwa bahati mbaya, jopo hilo lilifanya jinai ya kusadikisha watu kuwa uhuru wa Tanganyika ulitokana na harakati za kudai uhuru zilizofanywa na TANU, chini ya Mwalimu Julius Nyerere, na kwamba haukupatikana kwa kumwaga damu.

Kwa utotofu huo wa maksudi Watanzania wa kizazi cha sasa wanasadikishwa, tena kwa maksudi, kuwa harakati za kujinasua na ukoloni Tanganyika, hazikuanza tangu zama za akina Mtemi Mirambo wa Unyanyembe, Mangi Mweri, Chief Mkwawa, Vita vya majimaji, kutaja kwa uchache!

Harakati hizo ambazo, wakoloni waliziita, 'native resistance or rebellion' zilisababisha umwagaji mkubwa wa damu za mashujaa wetu wazalendo, licha ya andiko rasmi la historia kutotambua umuhimu wa michango ya mashujaa huo, katika harakati za kupigania uhuru wa kujitawala, hata kama kila mwaka tunawakumbuka na kuadhimisha siku ya Mashujaa.

Bado tunahitaji wanahistoria makini waandike histori ya Tanzania anayoakisi harakati za kupigania uhuru tangu enzi za akina Abushiri, Chifu Chaburuma, nk, hadi enzi za T.A.A na TANU iliyotamatisha mchakato huo.
 
Watanzania huwa wana kiburi ya hali ya juu sana maana wanaamini kuwa wao ndio waliikomboa Afrika kutoka kwa Mabeberu. Ukiona waziri wao akifoka jinsi waliikomboa Afrika hadi mate inamtoka mdomoni na mishipa kuvimba kichwani ndio utajua kwamba hii propaganda ya CCM ni nzito sana.

Ukweli wa mambo ni kuwa nchi chache sana hapa Afrika zilipigania uhuru wao. Nchi zilizopigania uhuru kwa kumwaga damu hazijapita 12 hapa Afrika. Nitataja baadhi yao: Kenya, Guinea Bissau, Mozambique, Zimbabwe, South Africa, Angola, Algeria na zingine chache. Nchi nyingi za Afrika zilipewa uhuru wao bure bila vita. Tanzania ni mojawapo ya nchi zilizopewa uhuru bure kabisa na beberu bila Watanzania kuingia msituni kumenyana na Mzungu. Hamkumwaga damu ili kupigania uhuru wenu.

Kama nyie ni wakombozi wa Afrika mbona hamkuikomboa Kenya kutoka kwa mabeberu? Mabeberu waliua Wakenya karibia laki moja wakati wa state of emergency 1952 wakati wanapigana na Maumau. Wamama na watoto wakapelekwa kwenye concentration camp ambapo wengi walikufa kwa njaa. Wanaume walipelekwa gerezani na kuteswa na kuuawa.

Hata nchi ya Uingereza imeomba msamaha kwa ushetani waliotufanyia na kutoa pesa kama fidia. Mbona nyie hamkutusaidia? Mbona sisi tulijipigania uhuru wenyewe na kufa kwa wingi ili tupate uhuru wetu? Hakuna nchi yoyote ya Afrika iliyotusaidia kupata Uhuru. So nyamazeni. Hata hamkupigania uhuru wenu mlipewa bure. We don't owe you anything. Hatuna deni lenu maana nyie hamkutusaidia.
Hakuna mtu mwenye dhamana ya uhuru wa mtu mwengine.
So hiyo kupewa uhuru sijui ndiyo nini!
 
Back
Top Bottom