Kenya: Jaji Mkuu amjibu Kenyatta. Nendeni mkashindane kwenye uchaguzi

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Jaji Mkuu nchini Kenya, David Maraga aliudhihirishia ulimwengu kuwa kuna uhuru wa mahakama katika bara la Afrika ambako agharabu majaji wanaonekana kutetea walio madarakani.

Lakini kwa wanaofahamu vizuri Jaji huyo, hawakushangazwa na uamuzi wake wa kubatilisha uchaguzi wa nchi hiyo.

Jaji Maraga, amemjibu Rais Uhuru Kenyatta baada ya kuwashambulia majaji wa mahakama ya juu ya nchini humo.

"Mimi siyo Mwanasiasa na nafanya kazi kulingana na misingi ya kiapo cha utii nilichochukua ili kuwatumikia Wakenya, siungi mkono JUBILEE wala NASA au mtu yeyote.

Nasimamia Katiba ya Kenya. Nendeni mkashindane kwenye uchaguzi na kama yeyote hataridhishwa na matokeo ni kiasi tu cha kuleta shauri/malalamiko yenye ushahidi mzuri/wa kutosha na mimi na wenzangu tutafanyia kazi bila kusita.

Kumbuka kwamba namuogopa Mungu peke yake".


Jaji Mkuu David Maraga.
 
Huyu ndio jaji. Sio wale wengine anatoa hukumu huku mfukoni ana kadi ya chama ambaye kwa vyovyote atai-favor mamlaka iliyompa hicho cheo tuache kufanyana wajinga.

Kuna mmoja alifikia hadi hatua ya kugombea uongozi kupitia chama chake mara baada ya kustaafu. This is truly separation of power among the state organs.
 
Hatari sana mkuu
 
Huyo unayemsema alipata wapi kadi ya chama na kisha yeyw kugombea uongozi (RAIS) km yeye alikuwa JAJI?

HAYA NI MAAJABU YA 10 YA DUNIA HII

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lubuva...ccm
Tulia....ccm
Augustin... Ccm
Mtungi...ccm
Kanali shimbo...ccm
Mawazri wote...ccm
Wakuu wa mikoa...ccm
Wakuu wa wilaya...ccm

Nknk
Tanzania...mali ya ccm

Hata Viongozi wa Upinzani wote ni CCM ama kwa kujijua au kutojijua!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…