KENYA: Mahakama yatengua matokeo ya Uchaguzi wa Rais. Kurudiwa upya ndani ya siku Sitini(60)

Wanajukwaa kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu, mahakama ya juu nchini Kenya imeamuru time ya uchaguzi IEBC kuandaa uchaguzi mwingine ndani ya siku 60.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuna watu wanaobadilishiwa gia vichwani na viongozi wao watachanganyikiwa...
 
Majaji wametoa reason gani hadi wamefuta huko hebu tupe habari kamili
 
Mahakama imeufuta uchaguzi wa kenya kwa kua ulikua na dosari kubwa muda mfupi uliopita naamini kuna la kujifunza kwa hawa jirani zetu haswa serkali na mahakama zetu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpaka pale wanasiasa wa Tanzania na wananchi kwa ujumla watakapofahamu kuwa democrasia ndio yaleta maendeleo katika nchi hapo ndipo tutakuwa tumejitawala,lakini haya yanayoendelea hivi sasa Tanzania ni sawa na utawala wa kikoloni wenye sura ya mwafrika..

Wakenya wako mbele kiuchumi,kimawazo na sasa wametuonyesha mpaka kwa demokrasia wametupita,hii nchi tuiangalie kwa mbali,hii nchi ni ya kupigiwa mfano Afrika Mashariki.

Mungu ibariki Kenya
 
Hongera kenya kwa demokrasia ya juuu Africa..hapa kwetu hadi katiba ya warioba ipitishwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…