Kenya: Moto wazuka kwenye shamba linalomilikiwa na familia ya Kenyatta

Kenya: Moto wazuka kwenye shamba linalomilikiwa na familia ya Kenyatta

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
373
Reaction score
829
1679949951334.png

Moto mkubwa umezuka katika ardhi inayomilikiwa na familia ya Kenyatta karibu na barabara ya Eastern Bypass huko Ruiru, kaunti ya Kiambu.

Mlipuko huo wa moto unakuja saa chache baada ya mamia ya wahuni kuvamia shamba la Northlands na kuharibu mali ya thamani isiyojulikana.

Kulingana na ripoti, genge hilo liliingia katika ardhi hiyo kutoka upande wa Kamakis kupitia njia iliyo na shughuli nyingi na wengine walionekana wakiiba kondoo kutoka kwa mali hiyo.

Brookside Dairy, Shule ya Peponi iko ndani ya mali kubwa ambayo inaenea katika shamba hilo. Nia ya uvamizi huo haijulikani.

Sources Via Bbc Swahili.
 
Maridhiano yawepo, pamoja na uchaguzi ulioonekana hauna dosari watu watatu washauawa kupitia maandamano haya
Ni shidaaaaa...Mungu tuepushe na hili songombingo huku TZ, pia wasaidie Ndugu zetu Kenya wayajenge vyema.

Amani ni rahisi sana kuivunja, kimbembe ni kuirejesha upya kama ilivyokuwa awali ndipo penye kitendawili kigumu sana.

Case study [emoji117] Libya...[emoji30]
 
Back
Top Bottom