Kenya wanajivunia generation Z, Tanzania tunajivunia uchawa!

Kenya wanajivunia generation Z, Tanzania tunajivunia uchawa!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Bila shaka watu wote tumeona namna vijana wa Kenya maarufu kama generation Z walivyoitisha mtiti mzito kwa kupiga maandamano mazito mitaani ya kupinga mswada wa bajeti uliolenga kuwakamua zaidi kupitia kodi na tozo mbalimbali. Vijana wale kupitia mitandao ya kijamii pasipo msukumo wa wanasiasa wameweza kuhamasishana na kujipanga vyema, wamepiga kunji zito mtaani pasipo kujali vitisho, risasi, maji ya kuwasha, mabomu ya machozi, virungu vya mamia ya polisi katili wa Kenya waliomwagwa mitaani kuwadhibiti. Hamasa na mtindo wao wa kupiga maandamano umekuwa wa kipekee mnoo kiasi cha kuitisha serikali ya Kenya na kuiamsha dunia.

Huo ndio upande wa vijana wa Kenya, ukija upande wa Tanzania, upande wenye vijana watumiaji wengi zaidi wa mitandao huenda kuliko nchi yoyote ile katika ukanda wa Afrika mashariki na kati, vijana wake wako busy mnoo mitandaoni kusaka connection za ngono na umbeya, kubet, kuchambua soka, kupost picha zao zilizohaririwa, kudanga na kusaka madanga na kubwa kuliko yote kuupigia debe uchawa.

Leo hii hapa Tanzania, vijana machawa ndio kizazi cha dhahabu, machawa wanapewa mpaka mialiko rasmi bungeni na Ikulu. Uchawa umepewa hadhi ya kipekee, vijana wanajivunia uchawa, vijana wanatamani kuwa machawa na serikali inaupigia debe uchawa kama ndio njia bora ya kujiajiri.

Maskini vijana wa Tanzania!
 
Kuandamana ili kupata mabadiliko sio tatizo! Shida ni hiz pumba za Gen-z huu ni uwendawazimu.
 
Hamieni huko kwa Ruto, maana wenyewe mnapiga kelele humu ndani tu
 
Kwani Chadema si waliandama ila nini kilitokea? Utofauti na wenzetu si kwa wao kuweza kuandamana bali na aina ya serikali yao pia.
 
inamaana kuandama nayo ni ustaarabu au ni sehemu ya maendeleo? , ufahamu na ufikiri wenu ni.....
Uliwahi Kusoma Chochote Kuhusu Kuhusu Karl marx Theory of Development? Au uliwahi kusoma Ruling class au Marx Class theory?? Au uliwahi kusoma Marxian Economic?? Au uliwahi kusoma Marx module on Ideology??

Kama Hizi Theory chache (Japo Ziko nyingi) uliwahi kuzisoma then sitaki kuamini unashangaa kuona Tabaka Tawaliwa Likidai haki kutoka Tabaka Tawala..Ambayo ni haki yao kabisa...
 
Kwani Chadema si waliandama ila nini kilitokea? Utofauti na wenzetu si kwa wao kuweza kuandamana bali na aina ya serikali yao pia.
Hahah Chadema Hawakuandamana ila walisaidiwa na Serkali kufufua Chama 😅😅
Ili watangaze chama Chao..
Yale sio maandamano 🤣🤣
 
WE CAN'T MOVES IN SAME WAY, WACHA WAO WAENDE NA GENERATION, Z, SISI NA RAIS WETU, TUKAZANIE KUJAKIKISHA TUNA VIWANDA VINGI, KILIMO SAFI, UONGOZI SAFI, TUBORESHE HUDUMA SAFI ZA KIJAMII, INATOSHA, HATUWEZI KUWAIGA WEHU NA MATAHAIRA.
 
Back
Top Bottom