Kenya yafaulu kuuza maparachichi kwa mataifa 42, mwendo wa mbele kwa mbele, wakulima wetu hoyee

Serikali yetu ya Tanzania imelala usingizi wa pono kwasababu nawajua wakulima wa TZ wanaowauzia wakenya Parachichi shambani alafu wakenya wanaenda kuuza Ulaya, na hii ni kwasababu serikali ya Kenya imetengeneza mazingira husika.

Sisi tuko busy kucheza na Chuchu sijui Zuchu.
 
Ajabu ni kuwa malori mengi yaliyokwama kwa sakata la corona Namanga na Horiri kutokea Moshi na Arusha yalikua na maparachichi

Si ndio inatakiwa tuwashukuru majirani kwa kutafuta soko la nje ili na wao wakija kununua kwetu wakulima wafaidike?

Ikiwa sie tumeshindwa kutafuta masoko kimataifa, acha wanaoweza wafanye kazi yao tunufaike wote.
 
Hahaha unajitahidi kweli kukwepa ukweli ila ukweli hauhitaji approval yako kuwa valid.

Hamna wala hamtakaa muwe na ardhi ya kulima Parachichi kuzidi Tanzania, kaeneo mnakokalimia Parachichi Kenya yote ni kama garden ya kitalu ya mkulima mmoja wa Parachichi Iringa.
 
Si ndio inatakiwa tuwashukuru majirani kwa kutafuta soko la nje ili na wao wakija kununua kwetu wakulima wafaidike?

Ikiwa sie tumeshindwa kutafuta masoko kimataifa, acha wanaoweza wafanye kazi yao tunufaike wote.
Tatizo jirani ameshindwa kutambua mchango wa Tanzania katika hii biashara.
 
hahaha asilimia 90 ya Parachichi wanazoexport wanazitoa Tanzania

Tanzania inaongoza Africa kwa uzalishaji wa Parachichi SA wenyewe wanakuja kuchukua Parachichi za exports kutoka Tanzania


Kuzalisha jambo moja, kutafuta masoko ni jambo jingine.

Tukubali wakenya wametuzidi ujanja kwenye uchakarikaji.

Kuna taasisi, wizara au watu hawafanyi kazi yao ipasavyo au wanaenda kwa mazoea.

Kuna kipindi tujifunze kwa hawa majirani.

Kuliko mazao yaozee shambani, bora tuwauzie wakenya wenyewe wapeleke kwa mabeberu ikiwa sie hatuwezi kujiongeza kutafuta masoko nje.
 
Tatizo jirani ameshindwa kutambua mchango wa Tanzania katika hii biashara.

Jirani alikua anapambana na Covid 19, usisahau huo ugonjwa siasa zimetawala sana kuliko utaalam. Ni janga jipya hata hivyo kila watu wanaogelea kivyao. Hadi sasa hakuna mwenye suluhu moja inayoaminika kwa wote. Trump juzi katupia barakoa.

Tukirudi kwenye hoja, sisi inabidi tuwashukuru majirani kwa kuokoa parachichi za wakulima wetu zisiozee shambani. Mambo ya shukrani au kutambua mchango si tija sana.

Chapati bado zipo nije kuchukua?
 
Ninyi si mlikua mnapinga ununuzi wa ndege na kusema hamtaki maendeleo ya vitu bali watu na kwamba bibi yako analima Parachichi pale njombe hizo ndege zitamsaidia nini?

Ndio akili iwakae sasa
 
Hata hapa arusha maparachichi hupelekwa EU na sijaelewa dhumuni la hii topic yako maana hata hayo huku TZ tunafanya cnt brag about its skiddish
 
Neno asante ni dogo lakini kina maana kubwa sana. Unapomwambia asante hata mfanyakazi kazi wako ingawa unamlipa mshahara anazidisha ufanisi. Ni njia ya kumfahamisha kuwa unatambua mchango wake au mchango wake ni muhimu kwako.

Chapati zippo karibu.
 
Hata sisi kwetu njombe tunalima Hass kwa wingi sana na wanunuzi wakubwa wanatoka Kenya.
 
MK254 hayo makatapera Wakenya wanayanunua Mbeya, Iringa na Njombe Kisha huyaleta Kenya na kusema wameyazalisha wao.
CCM imesababisha Taifa zima tuonekane mazuzu.
Dah jombaa, hata wewe pia ni miongoni mwa hawa matomaso ambao hawaamini kwamba maparachichi ya export yanakuzwa kwa wingi nchini Kenya? Naona baada ya wenzako kukosa takwimu za kuhalalisha madai yao kwamba Tz ndio mnazalisha zaidi wameanza kutupia video. Haya basi ndio hizi video, ukulima wa maparachichi nchini Kenya upo kwenye level nyingine.



Cc. vulcan
 
Ninyi si mlikua mnapinga ununuzi wa ndege na kusema hamtaki maendeleo ya vitu bali watu na kwamba bibi yako analima Parachichi pale njombe hizo ndege zitamsaidia nini?

Ndio akili iwakae sasa

Kuna vitu ukijadili jaribu kutuliza akili na kuweka ushabiki pembeni. Hata nikikwambia uthibitishe madai yako dhidi yangu hauwezi.

Hapa unaambiwa habari ya ku export wewe unaibuka na mambo ya ndege, mbona sasa hivi zipo na Samaki wanapelekwa nje kwa ndege ya Rwanda?

Kama suala ni usafiri na sio utafitaji wa masoko si mngepeleka ndege zikapakie parachichi Kenya kupeleka huko kwenye masoko yao waliyotafuta wao? Ikiwa hatuwezi kubuni basi tujaribu japo kuiga tu.

Haujasikia juzi wanasema serikali ina mpango wa kununu ndege ya mizigo ipeleke mazao nje?

Haya mambo yanahitaji mikakati sio ukurupukaji. Lakini hizi harakati huenda zikatupeleka kwenye njia sahihi tukituliza akili na kufikiria kwa umakini, matokeo ya maamuzi yatakua na tija mbeleni.
 
Kuna vijana wamejitahidi Sana kuitambulisha parachichi ya Tanzania (njombe) lakini wanachokutana nacho toka kwa maafisa wetu wa biashara na kilimo, utashangaa. Ni kupigwa vita na kukatishwa tamaa.
 
Neno asante ni dogo lakini kina maana kubwa sana. Unapomwambia asante hata mfanyakazi kazi wako ingawa unamlipa mshahara anazidisha ufanisi. Ni njia ya kumfahamisha kuwa unatambua mchango wake au mchango wake ni muhimu kwako.

Chapati zippo karibu.

Usisahau wakenya ni mabepari!

Nifungie na mihogo ya kukaanga uweke chachandu nyingi ntapitia muda si mrefu. Ahsante
 
Hii habari nimeiona pia kwenye media ya CRI ya China. Hongereni sana jirani zetu wa Kenya
 
Aiseee umenikumbusha wimbo wa Mgosi Maliki Mkoloni ft Mr Ebbo unaitwa - Sifa za Kijinga ebu usikilize chini.

 
Reactions: Oii
Tanzania tunayo kila sababu ya kuiga mbinu za majirani kukuza uzalishaji na soko la ovacado.
 
Ninyi si mlikua mnapinga ununuzi wa ndege na kusema hamtaki maendeleo ya vitu bali watu na kwamba bibi yako analima Parachichi pale njombe hizo ndege zitamsaidia nini?

Ndio akili iwakae sasa
rudi shule mataga, hapa ni swala la wizara ya biashara kutengeneza mazingira ya wakulima kupata masoko ya parachichi nje ya nchi,
swala la umiliki wa ndege halihusiki hapa kwasababu hata sasa kuna madege mliyoyapokea kwa kukata viuno ila madege yapo tu parking na tunatuma minofu ya samaki ulaya kwa kutumia Rwanda Air.
kwa hiyo funga bakuli lako kabisaaa wewe Chuchu sijui Zuchu.
 
Hata sisi kwetu njombe tunalima Hass kwa wingi sana na wanunuzi wakubwa wanatoka Kenya.
Hahaha unajitahidi kweli kukwepa ukweli ila ukweli hauhitaji approval yako kuwa valid Hamna wala hamtakaa muwe na ardhi ya kulima Parachichi kuzidi Tanzania.
Serikali yetu ya Tanzania imelala usingizi wa pono kwasababu nawajua wakulima wa TZ wanaowauzia wakenya Parachichi shambani alafu wakenya wanaenda kuuza Ulaya.
Nina maswali mawili. La kwanza, Kenya na S.A wanakuza na kuuza maparachichi kwa wingi, yaani 'exports'. Takwimu za Kenya na S.A zinasomeka vizuri tu. Mnasema Tz inakuza na kuuza kwa wingi zaidi, inakuwaje takwimu zenu za 'production' na 'exports' hazi'reflect' hayo mnayoyasema? Pili, inakuwaje kwamba wakulima wa Kenya wanapokea pesa taslimu moja kwa moja kutoka kwa exporters(KES 9B, Jan-June) wakati mazao ni ya watz kama mnavyodai?
 
Nyie muko na ujanja mwingi kutuzidi.
Sisi tunakabana wenyewe kwa wenyewe, mutu akijaribu kufurukuta anapigwa nyundo kwa kichwa hata asiweze....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…