Kenya yapunguza viingilio vya utalii ili kufufua sekta ya utalii iliyoathiriwa sana na Corona

Kenya yapunguza viingilio vya utalii ili kufufua sekta ya utalii iliyoathiriwa sana na Corona

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Kenya jana imetangaza kupunguza ada za kuingia mbuga kuu za wanyama pori kwa watalii kutoka ndani na nje ya nchi hiyo ili kuhimiza sekta ya utalii iliyoathiriwa sana na janga la COVID-19.

Taarifa iliyotolewa na Shirika la huduma za Wanyamapori nchini Kenya (KWS) limesema hatua hiyo itadumu kwa mwaka mmoja.

Pia shirika hilo limewaruhusu wamiliki wa nyumba za kulala wageni kwenye hifadhi za wanyama pori wasitishe kulipa kodi kwa mwaka mmoja kuanzia tarehe Mosi mwezi Julai hadi tarehe 30 mwezi Juni mwaka ujao.

Waziri wa utalii na wanyama pori wa Kenya Najib Balala amewataka wamiliki hao kuboresha huduma za watalii na kukuza biashara zao kwa kutumia akiba inayotokana na usitishaji wa kodi.
 
Wanafanya hivyo coz wanajua hakutakuwa na idadi kubwa ya watalii katika nchi ambayo kila siku takwimu za maambukizi ya corona zinazidi kuongezeka kuliko kinyume chake.
 
Safi sana hawa ndo wanajua namna ya kuweka mazingira mazuri ili hela ikufuate uliko bila jasho kubwa.
Mbinu za kipimbi hizi ila Kwa mtalii wa Africa utampata ila c mzungu, mzungu mpaka anakuja huku haangali saana kuhusu gharama anaangalia nini anataka na usalama , Kenya kila kaunti imefungwa halafu unaweka mazingira ya utalii mgeni huyo anakuja na ungo?
 
Afya muhimu zaidi , mtalii gani ataenda Kenya ikiwa ni kitovu cha Corona ukanda huu?.
Wanafanya hivyo coz wanajua hakutakuwa na idadi kubwa ya watalii katika nchi ambayo kila siku takwimu za maambukizi ya corona zinazidi kuongezeka kuliko kinyume chake.
Kwa taarifa yenu Kenya ni kati ya nchi tatu za Afrika ambazo zimepata idhini na muhuri, 'safe travel stamp', ya WTTC(World Travel and Tourism Council) shirika la kimataifa la utalii na usafiri. Nchi zingine ni Tunisia na Egypt, hiyo travel stamp inahusisha serikali na wadau wengine kwenye sekta ya utalii kama hoteli na kampuni za usafiri kwenye protokali mpya za utalii na usafiri wakati wa janga la Corona. Mambo yanafanywa kitaaluma zaidi nchini Kenya, sio ubabe ubabe na siasa za peni mbili, kila nchi ifate sera zake na kila mtu apambane na hali yake. Matokeo tutayajua baadaye mwakani. #SafeTravels: Global Protocols & Stamp for the New Normal | World Travel & Tourism Council (WTTC)
 
Kwa taarifa yenu Kenya ni kati ya nchi tatu za Afrika ambazo zimepata idhini na muhuri, 'safe travel stamp', ya WTTC(World Travel and Tourism Council) shirika la kimataifa la utalii na usafiri. Nchi zingine ni Tunisia na Egypt, hiyo travel stamp inahusisha serikali na wadau wengine kwenye sekta ya utalii kama hoteli na kampuni za usafiri kwenye protokali mpya za utalii na usafiri wakati wa janga la Corona. Mambo yanafanywa kitaaluma zaidi nchini Kenya, sio ubabe ubabe na siasa za peni mbili, kila nchi ifate sera zake na kila mtu apambane na hali yake. Matokeo tutayajua baadaye mwakani. #SafeTravels: Global Protocols & Stamp for the New Normal | World Travel & Tourism Council (WTTC)
Hakuna mtalii mtoto watu waelewa na dunia sasa hv kijiji sasa we baki na karatasi yako ya cheti cha mzungu watu wanajua kama Kenya ipo kwenye hali mbaya
 
Hali mbaya aje na wanajua vitu hazifichwi
Nani ataeza Kwa nchi wanaoficha Kila kitu,mybe watali vichwamaji
Wakati medege yashaanza kushuka na watu mahotelini washaanza kuchukuliwa tena , we baki hapo hapo na nadharia yako
 
hongera zetu mazeee dah!...pale wizarani kuna vichwa hatari si mchezo!!!😂
utalii ni mikakati....
kule uswahilini majuzi tuliona waziri ameenda na kukita kambi uwanja wa ndege ategeetegee wageni ! aiseeee!
Ukiona hivyo usiseme mna vichwa! Jua uchumi unapumulia mashine.
 
Wakifika bure mnishitue...

Sisi huku tunaweka mkazo zaidi watalii waje kwa direct fly mpaka bongo. Watalii watakao tokea nchi jirani tutawapiga kodi na pia waongoza watalii wa nchi jirani na magari yao ni kuyaongezea kodi tu yakitaka kuvuka kuja huku. Na ni marufuku kwa watu wa utalii wa nchi nuyingine kufanya ikazi za utalii ndanmi ya nchio yetu. Tuko na expert wa kutosha huku.
 
hongera zetu mazeee dah!...pale wizarani kuna vichwa hatari si mchezo!!! utalii ni mikakati.... kule uswahilini majuzi tuliona waziri ameenda na kukita kambi uwanja wa ndege ategeetegee wageni ! aiseeee!
Vichwa kweli sio mchezo. Anaitwa Waziri Najib Balala, mikakati na sera za kueleweka kwanza, hata sekta ya usafiri wa anga bado hajaifunguliwa. Jirani walianza kwa kufungua anga yao ili wawakomeshe wapinzani. 😁 Kisha waziri wao wa utalii akaanza kukesha kwenye uwanja wa ndege. Ona waziri mwenyewe alivojichokea akiwangoja watalii. [emoji1][emoji1][emoji1]
2419332_Screenshot_20200606-100106_Twitter.jpg
 
Hakuna nchi inayoweza kushindana na tz afrika mashariki kwenye utalii ndo maana tunaingiza hela nyingi kuliko nchi yoyote.
 
Imetoka bei gani now iko bei gani nataka kuja kutalii huko nipeni taarifa kamili majirani.
 
Back
Top Bottom