Kenya's Day of Pride; The Birth of a New Republic

Kenya's Day of Pride; The Birth of a New Republic

....daaah mpwa Kaizer.....umetuwakilisha vilivyo hapo Uhuru park.....pamoja na mkuu Shadow.....big up sana! Hongereni sana Wakenya.....! u have made a very importanty step kwenye maisha ya wakenya waleo, wakesho na vizazi vijavyo........!
 
Mwai Kibaki anaongea sasa...

Sasa naona tumewakilishwa na 'His Excellencey Aman Karume, President of Zanzibar'...hivi Tanzania Imekufa ? au haijawahi kuwepo

Hili ndio jibu zuri.... W'end imeanza huku, we endelea kupuliza vuvuzela....
 
Hili ndio jibu zuri.... W'end imeanza huku, we endelea kupuliza vuvuzela....


Dah, kwa comment hii yta Askofu, nalazimika kuchomoka niingie mtaani

Hotuba ya Kibaki watu wamekuwa makini sana iola haina kushangilia manake its just so technical....kama kawaida yake...ndo anamalizia

See you all guys
 
Anaongeza........"Utawala wa Imla na Kimabavu umewekwa kwenye kabiuri la sahau,, Mafirauni warudi kwao...."

Kitendawili!....yeye ni mnyama na yeye ni ndege, ni nani? wanajibu Popo" sijui anamaanisha nini LOL
Raila Odinga anajulikana sana kwa kupenda kutumia mafumbo na lugha ya majazi...nd'o maana
wananchi wa kawaida wanampenda. Si unaona anavoshangiliwa?...The man has been on the fore
front of this fight since day one na hajasita. Mpiganaji wa kikweli na sio ndumilakuwili. Kenya needs
him big time.
 
Dah, kwa comment hii yta Askofu, nalazimika kuchomoka niingie mtaani

Hotuba ya Kibaki watu wamekuwa makini sana iola haina kushangilia manake its just so technical....kama kawaida yake...ndo anamalizia

See you all guys

Kajichanganye mwaego...
 
There is no doubt that Kenya has moved forward a major step and they should be congratulated for this achievement. The Ugandans went through a similar exercise in 1996 but the only diffrence it was a no party type of constitution which has now been severely compromised by the removal of the clause limiting the Presidency to two terms.

Sisi Tanzania kusema kweli tuna katiba yenye viraka viraka hasa baada ya hayo mabadiliko ya katiba Zanzibar. At least as a matter of URGENCY kama hatuwezi kuibadili katiba kwa ujumla basi tuongeze hivyo viraka kwa kufanya mabadiliko mawili:

Kwanza wabunge wasiwe mawaziri - Rais achague mawaziri kutoka raia wenye ujuzi na wawe vetted na bunge - hili nafikiri ni badiliko la maana sana tutakaloweza kujifunza toka Kenya. Itapunguza namba za mawaziri etc. itaprofessionalize uongozi serikalini na kupunguza gharama za kuendesha serikali.

Pili kupunguza madaraka ya rais hasa katika ku wateua viongozi wa serikali na mashirika e.g. civil servants. This is one of the worst cancers eating our institutional framework and unless things change then I cannot see much progress occuring in Tanzania.
God bless Africa; God bless Tanzania.
 
Moja ya mambo kwenye mabadiliko ya Katiba mpya ya Kenya ni kufutwa kwa kifungu cha Mahakama ya Kadhi ndani ya katiba hiyo. Hii ni kwa sababu Wakenya wamezingatia kwamba Kenya ni Taifa lisilo na dini, hivyo haikuwa vyema mamlaka hiyo kidini kuwa sehemu ya Katiba. Lakini bdo uhuru wa kidini kwa raia wake umezingatiwa sana.

Sasa vioja huku Tanzania ni kwa wale wanokomalia kifungu cha mahakama ya kadhi kuwepo kwenye katiba. Yaani wakati wenzetu wameona athari zake huku kwetu bado kuna watu wanaitaka. Mimi naikubali sana hiyo mahakama kama itaanzishwa na kuendeshwa na wenyewe wenye dhini yao na si kutaka serikali iitambue kwenye katiba yetu. Hivi, mnajua kwamba Mufti wa Zanzibar na timu yake yooote ni waajiriwa wa SMZ. Kwa hiyo kitendo cha kuruhusu ni kutaka serikali ya Tanzania ijiingize kugharimia asasi ya kidini, kwa manufaa ya wanadini hiyo. Hii haikubaliki hata kidogo.

Lakini hebu, fikiria wewe ni mkristo, kijana wako kampenda binti wa kiislamu na akaamua kusilimu, ukaridhia maana wamependana. Sasa inatokea kasheshe kijana wako anatuhuma fulani, anapelekwa kwenye mahakama ya kadhi, anahukumiwa kukatwa mikono, utajisikajee?. Dini zingine bwana.

Nawaomba sana wenye hoja hiyo wasiingize nchi kwenye matatizo. Inasemekana JK amewaahidi kimya kimya jamaa zake kwamba akishinda sasa, mahakam hiyo inakuja kwa ridhaa ya serikali. Sijui itakuwaje ikitokea hivyo. Nnachoweza kutabiri tu kwamba yatatokea machafuko ambayo hayajawahi kuonekana. Narudia, kama Wakenya wameliona hilo, nasi tusijipeleke huko.
 
Ni hatua ya matumaini na kutia moyo..Lakini pia ni ujasiri wa juu sana.Hapo ndipo Watanzania tunapotofautiana na Wakenya!..Linapokuja jambo la kitaifa wanashikamana kama kitu kimoja!
Mungu aibariki sana siku hii kubwa kwenu!

PK,
You can say that again,comrade.
 
Baado Tanzania tuna safari ndefu,angalia mambo CCm inayoyafanya kwa kuvunja sheria,inatumia magari ya serikali,mawaziri wake bado wako ofisini na wakati huohuo wako kwenye kampeni,wanaagiza mabango toka Canada na halipii ushuru,

Ndio maana sikuhangaika kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura,kwani hakuna lolote litakaloweza kufanywa kwa kutumia haki yangu ya kupiga kura bila ya kubadilisha katiba,na nimeapa kama katiba haitabadilishwa sitajiandikisha kupiga kura hadi kaburini,mambo yanayofanyika sasa hapa nchini kwetu ni kuchezeana akili,hebu angalia mtu anaweka pingamizi la hovyo ili apite bure kisa eti jina limekosewa herufi.Mfano hai ni wa Waziri Masha,alivyokuwa anampigia simu mgombea kupitia Chadema,na hao ndio viongozi vijana tunaowategemea watufikishe Kanaani kwenye nchi ya asali na maziwa!.Kwa mara ingine hongereni Wakenya mmejitofautisha na nchi zote za EAC,kama Uganda ambako M7 anang'ang'ania madaraka,Rwanda kwa dikteta Kagama na Burundi ambako kote huko mambo ni hovyo hovyo.
 
PIX+3.jpg

A section of Uhuru Park crowds witnessing the promulgation of the constitution


PIX+12.jpg

At the entrance to Uhuru Park Nairobi on August 27, 2010.


PIX+11.jpg



PIX+9.jpg

Former Sports heroes arrive at Uhuru Park for Constitution promulgation.
 
DNKIBAKISIGN2708.jpg

Presdient Kibaki signs the new constitution into law




 
Last edited by a moderator:
x610.jpg


Prime Minister Raila Odinga takes oath of office based on the new constitution
 
Inaelekea mabadiliko hayo ni mazuri. Tupo na Mkenya huku kwenye nchi za watu, yaani tangu asubuhi amefurahi, na ananipa stori kwamba hii ni Kenya mpya!
 
Hongerani sana Wakenya kwa mafanikio haya, ukweli mimi kama Mtz najisikia kuwatamani. Mmepiga hatua moja mbele, tena hatua ya muhimu sana sisi tutabaki na maneno meeeeengi lakini tupo hapa hapa.
Mungu awabariki sana!.
 
Issue ya mahakama ya kadhi kuwekwa kwenye katiba ya nchi haipo. Kama unasikia JK amewaahidi kuwa ataichomeka ujue anawadanganya tu kama ilivyokuwa mwaka 2005. Just rest assured kuwa hakuna kitu kama mahakama ya kadhi inayotambuliwa kikatiba hapa TZ.

Just relax, hii kitu imeshazikwa kabisa. You cant rely on CCM promises my friend. Such promises are just lies. When they speak lies they speak of their own. Liars from the beginning
 
sijasoma hiyo katiba, na hiyo ni habari njema kwa Wakenya na ni somo kwa WaTz.kutoka moyoni mwangu naamini kadhi ni ibada, na ibada inaendeshwa na waumini, kwanini tulazimishwe tusioamini kushiriki kwenye ibada zao.Nawaheshimu Waislamu dunia nzima, lakini hili la kadhi endesheni wenyewe, kwa amani.
 
Back
Top Bottom