Kenya’s economy to grow fastest in Africa in 2021 - World Bank

Wakati nikiwa mdogo hakukua na Omo wala Blue band Tanzania, badala yake tulikuwa na Tan bond, sabuni za Mbuni (za mche) pamoja na Foma (sabuni ya unga). Baiskeli tulikuwa na kiwanda chetu pale Mwenge (Dar) kinaitwa Swala. Bata haikuwepo Tanzania, tulikuwa na maduka yetu ya viatu vya Bora.

Kumbe wewe ni bwana mdogo sana, huijui historia ya nchi yako. Ndiyo maana Magufuli juzi alimwagiza Ndalichako aangalie upya mitaala na ufundishaji wa historia ya Tanzania.
 
Wewe unazungumza Dar, Arusha na Kilimanjaro vilikuwepo, hata hivyo unavyovitaja vilikuwa vinapatikana kwa kukimbiza mkokoteni kisha unanipanga foleni kwenye maduka ya bidhaa muhimu, napo unaweza ukapata au ukakosa. Dar ilikuwa ukionekana na Colgate unakamatwa muhujumu uchumi! Sabuni mbuni uwe na kakipande ukiwa na mche utalala rumande kwa kuhujumu uchumi. Viwanda vya Tanzania tatizo lake vina eksipaya deti, kama vilivyoeksipaya vya simenti! Tanga kwisha, Mbeya kwishneyi!

Moro kimezinduka cha mmasai! Dar hata cha Tabisco kilitushinda, hiyo Tanbond ilikuwa kituko Mara ya njano, mara, nyeupe, mara chumvi kibao, mara Haina chumvi na makopo mengine unakuta imeyeyuka na hauwezi kuigandisha.

Kutokiona Omo haikuwa na maana kiwanda kilikufa! Ila watanzania walichubuka mikono na mbuni, kodroyi na visabuni vya hovyohovyo vilivokuwa vinatengenezwa hapa. Hicho kiwanda cha Swala pale Mikocheni kilidumu siku chache tu.

Unapotetea kitu tetea cha viwango vya juu, achana na vyerehani vinne ni kiwanda! Huo ni ujuha.
 
Wewe unaongelea maisha ya kupanga foleni baada ya vita vya Uganda ambapo IMF walikataa kumkopesha Nyerere. Tanzania ya miaka ya 1969 - 1979 watu walikuwa hawapangi foleni.
 
Wewe unaongelea maisha ya kupanga foleni baada ya vita vya Uganda ambapo IMF walikataa kumkopesha Nyerere. Tanzania ya miaka ya 1969 - 1979 watu walikuwa hawapangi foleni.
Miaka yote uliyoitaja bidhaa za Kenya ndizo jilizojaa madukani, kukosekana bidhaa kulianza kabla ya vita baada ya kuanzisha maduka ya ujamaa (COSATA) na kufunga ya watu binafsi, hii ilikuwa kabla ya vita.
 

Hawa vijana wanakosa kujua mambo meengi sana ya historia.

Hawajui hata kwamba Tanzania iliwahi kuwa na kiwanda cha magari, machine tools, Mang'ula.

Shirika la ndege lililorusha ndege mpaka Heathrow International Airport. Pia reli inayounganisha nchi jirani ya Zambia, mpaka Afrika Kusini. Orodha ni ndefu sana.
 
Kenya mko juu kama nikweli pamoja na effect ya corona bado mkuu vizur # while sisi Watanganyika hatuna corona na uchumi unashuka kila siku GDP yetu ni US$65 miaka nenda rudi.
Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi Kenya imefika viwango vya juu vya ukuaji wa uchumi

Kwa ukubwa wa GDP yao hiyo rate ya growth ni kubwa Sana yaani Tzn sijui itapunguza lini gap ikiwa tumepitwa Hadi kwenye economic growth
 
Siri ni kuwekeza kwenye raslimali ya nguvu kazi, ukiwa na aina hii ya raslimali taifa lako linanawiri tu hata yakitokea majanga ya aina gani.
Ni kweli maana mind set zao zinawaza biashara na wako agressive kuliko watanzania ambao Wana mawazo ya kijamaa na kutegemea serikali Kila kitu.

Ndio maana huku Tzn serikali inafanya Hadi biashara za guest house sijui watu wake watafanya nini.
 
Kadanganye bibi yako ,miaka yote ya JK uchumi ulikua kwa average ya 7% na maendeleo mengi na ukuaji wa miji ulifanyika kipindi hiki
Majumba yote yanayopamba miji mikubwa yalijengwa awamu ya JK

Alipoingia Mungu Mtu jiwe haambiliki ndio kavuruga uchumi na umekua kwa viwango vidogo kama enzi ya mkapa,ponapona yake ni alipokea nchi ikiwa kwenye misingi mizuri ya uchumi but miradi yake haijawa na tija na haitakuwa na tija maana ni liability na haigusi watu wengi.

Maisha ya mtu mmoja mmja yamekwenda chini Sana maana hawana purchasing power kiufupi kazalisha maskini wengi kuliko kuwatoa kwenye umaskini.
 
Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi Kenya imefika viwango vya juu vya ukuaji wa uchumi
Kwa ukubwa wa GDP yao hiyo rate ya growth ni kubwa Sana yaani Tzn sijui itapunguza lini gap ikiwa tumepitwa Hadi kwenye economic growth

Hilo siyo lengo la Tanzania la kupunguza tofauti ya uchumi na ukuaji wa uchumi kati yake na kenya. Bali ni kufikia malengo na shabaha ambayo kama nchi iliyojiwekea.
 
ukuaji wa uchumi ulikuwa 7% sawa.

unajua mpaka jk anaachia madaraka 2015 tofauti ya uchumi kati ya kenya na tanzania ilikuwa ni kiasi gani???
 
Ni kweli maana mind set zao zinawaza biashara na wako agressive kuliko watanzania ambao Wana mawazo ya kijamaa na kutegemea serikali Kila kitu
Ndio maana huku Tzn serikali inafanya Hadi biashara za guest house sijui watu wake watafanya nini
Eti serikali inafanya hadi biashara ya guest house 😂 😂 😂
Hii Ni kali
 
Mwaka huuhuu wa jamaa Tangatanga now known as jamaa wa wheelbarrow? Na BBI?

 


Unamatatizo ya kusoma na kuelewa. Nilichosema ni mlinganyo kati ya uchumi wa Tanzania na Kenya, wakati wa Kikwete Wakenya walianza kutuacha sana.

Ni kweli maana mind set zao zinawaza biashara na wako agressive kuliko watanzania ambao Wana mawazo ya kijamaa na kutegemea serikali Kila kitu
Ndio maana huku Tzn serikali inafanya Hadi biashara za guest house sijui watu wake watafanya nini
Kumbe huwajui wakenya wewe, wanaujanja ujanja mwingi sana kwenye takwimu zao. Mfano kwenye kilomita za lami huwa wanaongeza urefu kwenye ripoti zao, juzi juzi hapa walishtukiwa na wazungu.

Shirika lao la ndege lina miliki ndege tatu tuu, yaani hata baada ya kufanya ujanja ujanja wote kutuibia ndege zetu baada ya jumuiya kuvunjika wao bado wanamiliki ndege tatu tuu.
 
ukuaji wa uchumi ulikuwa 7% sawa.

unajua mpaka jk anaachia madaraka 2015 tofauti ya uchumi kati ya kenya na tanzania ilikuwa ni kiasi gani???
Tofauti ilikuwa ni kidogo. Gap limeongezeka wakati wa Mungu mtu.
 
Inaonekana hata kazi ya kuwafinyia bibi zao serikali itaandika watu kazi ya kuwatoa nyege bibi zao maana kila kazi lazima wasaidiwe na serikali.
 
Tofauti ilikuwa ni kidogo. Gap limeongezeka wakati wa Mungu mtu.
nyie endeleeni kuongeza gape,sisi tunaongeza standard za maisha.

si umeona huo mchakamchaka!!!!si barabara,si majini,si angani,si huduma za afya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…