DOKEZO Kero: Madarasa katika Shule Teule ya Sekondari Kigoma Ujiji yanavuja, ni kero kubwa kwa Walimu na Wanafunzi

DOKEZO Kero: Madarasa katika Shule Teule ya Sekondari Kigoma Ujiji yanavuja, ni kero kubwa kwa Walimu na Wanafunzi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Joined
Jul 13, 2024
Posts
5
Reaction score
3
Naomba kuwasilisha kero kwa Mamlaka zinazohusika kwani madarasa ya Shule ya Sekondari Teule ya Kigoma Ujiji katika Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji yanavuja jambo linalowapa shida Wanafunzi.

Wakati mvua zinaponyesha kunakosekana utulivu wa kusoma kwakuwa kila mahali panakuwa panavuja, hali hiyo pia inachangia hata Walimu kusitisha mchakato wa masomo kwa kuwa kila mtu anakuwa katika kujiweka katika nafasi nzuri kukwepa kulowana.

Natoa wito Uongozi wa Shule urekebishe suala hili, ni jambo dogo lakini linakera na linasababisha usumbufu mkubwa kwa Walimu na Wanafunzi.

IMG_20250130_145948_575.jpg

IMG_20250130_144321_621.jpg

 
Shule inaitwa Kigoma Ujiji inapatikana kata ya kigoma mjini ni shule teule ya mkoa wa kigoma ambayo zamani ilikuwa ikitambulika kama Agacan
 
Pole kwa wanafunzi na waalimu
Me ni miongoni mwa wanafunzi tunaopitia adha hiyo jambo ambalo nimekwisha lalamika kwa mkuu wa shule lakini akasema hakuna pesa ya kufanikisha ukarabati hivyo tunapata tabu mvua zinaponyesha mtusaidie kupaza sauti kwa mamlika zinazohusika
 
Back
Top Bottom