KERO Kero ya kukatika maji Kawe Ukwamani

KERO Kero ya kukatika maji Kawe Ukwamani

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

meemi

Member
Joined
Mar 19, 2021
Posts
6
Reaction score
1
Takribani mwezi mmoja wakazi wa kata ya Kawe tunataabika na kero ya kukatika maji kiasi bila sababu yoyote ya msingi jambo linalotishia mlipuko wa magonjwa kama kuhara na kipindupindu kutokana na uchafu huku wahusika wakikaa kimya na viongozi wa serikali ya mtaa kutoshughulika na kero hii.

Mbaya zaidi ni pale tunapoona maeneo ya jirani kama Mbezi Beach na Kambi ya jeshi ya lugalo maji yakitoka kama kawaida ila wakazi wa Ukwamani wakihangaika na madumu machafu na mikokoteni ya maji inayobeba maji kwa gharama kubwa ambazo wananchi hatuwezi kumudu, takribani mwezi mzima sasa.

Ni jambo la kushangaza sana kwa karne hii jiji kubwa kama la Dar es salaam kukosa huduma muhimu ya kijamii kama maji.

Tunaomba wahusika washughulikie jambo hili limekuwa kero kubwa

MREJESHO:DAWASA: Kuendelea kwa matengenezo ya umeme katika mitambo ya maji ya Ruvu juu na Ruvu chini
 
GENTAMYCINE jirani zako wanapata shida, hebu waombee msaada kwa mbunge wenu Gwajima awaletee maji upesi
Na bado watapata Shida sana na bahati nzuri nilishahama Kawe tokea tarehe 18 February 2024 na Kuhamia Mapinga Bagamoyo Mkoani Pwani na pia huko nako sikukaa sana nimeacha Familia baada ya Mwenyezi Mungu kunifungulia Mlango wa Baraka na sasa nipo zangu hapa Kampala nchini Uganda nafanya Kazi ambayo baada ya miaka Miwili nitapewa Heshima Kubwa kwa Kuiwakilisha vyema Tanzania na najua hata Rais Samia atataarifiwa na GENTAMYCINE nitapigiwa Saluti na HATERS Wote japo najua WANAROGA mno ila Roho Mtakatifu ananipenda na ananipigania sana na NITABARIKIWA zaidi ya hapa kwa Jina lake Yesu Kristo.
 
  • Kicheko
Reactions: K11
Na bado watapata Shida sana na bahati nzuri nilishahama Kawe tokea tarehe 18 February 2024 na Kuhamia Mapinga Bagamoyo Mkoani Pwani na pia huko nako sikukaa sana nimeacha Familia baada ya Mwenyezi Mungu kunifungulia Mlango wa Baraka na sasa nipo zangu hapa Kampala nchini Uganda nafanya Kazi ambayo baada ya miaka Miwili nitapewa Heshima Kubwa kwa Kuiwakilisha vyema Tanzania na najua hata Rais Samia atataarifiwa na GENTAMYCINE nitapigiwa Saluti na HATERS Wote japo najua WANAROGA mno ila Roho Mtakatifu ananipenda na ananipigania sana na NITABARIKIWA zaidi ya hapa kwa Jina lake Yesu Kristo.
Mbona waraka tena mkuu
Kwani kuna shido🙄
 
Na bado watapata Shida sana na bahati nzuri nilishahama Kawe tokea tarehe 18 February 2024 na Kuhamia Mapinga Bagamoyo Mkoani Pwani na pia huko nako sikukaa sana nimeacha Familia baada ya Mwenyezi Mungu kunifungulia Mlango wa Baraka na sasa nipo zangu hapa Kampala nchini Uganda nafanya Kazi ambayo baada ya miaka Miwili nitapewa Heshima Kubwa kwa Kuiwakilisha vyema Tanzania na najua hata Rais Samia atataarifiwa na GENTAMYCINE nitapigiwa Saluti na HATERS Wote japo najua WANAROGA mno ila Roho Mtakatifu ananipenda na ananipigania sana na NITABARIKIWA zaidi ya hapa kwa Jina lake Yesu Kristo.
Duuh huu waraka una uhusiano gani na post🤔
 
Back
Top Bottom