Tetesi: Kesho Magari kufanyiwa ukaguzi maalum yanayokwenda Mkoani Kilimanjaro siri imejificha

Watakagua kutokea wapi sasa?
 
Hii habari ni SHILAWADU tu mtoa Post inaelekea umemaliza kazi zoote umebakiza umbea ulioubandika hapa tu.
 

Aisee, lengo la zoezi hilo nini eti ?

Ni zoezi la kawaida la PT kutekeleza majukumu yao au nyuma yake kuna msukumo wa kisiasa ?

Je, ina maana wanahisi Arusha na pengine na Manyara yote itatiririka kuelekea Moshi kuhudhuria mazishi ya huyu mzee kwa kutumia private & public transport na kwa maana hiyo polisi watumie mbinu ya "delaying tactics" na Ikilazimu kwa kunusa kwamba hawa wanaenda kwenye msiba na ni wafuasi wa chama pendwa CHADEMA basi wawabambikie road traffic offences siyo ?

Loooh !!

Ukiona hivi, tambua mara moja kuwa mgonjwa wetu CCM atapatapa na anakaribia kukata roho (kufa), tujiandaeni kwa mazishi tu !!!

Ama kweli, Magufuli Mzee wa Chato, ifikapo 2020 kwa mwendo huu, Tanzania yetu itakuwa tayari ni nchi ya V- WONDER kama Somalia !!
 
Ndo madhara ya kuzuia mikutano ya siasa na siasa, wadau wanapopata nafasi wanaitumia ipasavyo, mpaka itafikia hatua ataogopa kuruhusu mikutano ya siasa kabisa!!!!!!
 
Hizo ni propaganda maana kama mtu alikua na nia ya kuja kwa ajili ya msiba Angekuja tokea weekend, pia huwezi toka Dar leo na ukakuta ibada ya mazishi labda utoke na gari yako saa 10 alfajiri
 

Kama ni kweli hiyo operation itakuwepo basi naona ni muendelezo wa lile zoezi lililoanzishwa la kufanyia ukaguzi magari yote ya abiria so inaelekea ratiba ya ukaguzi wa mabasi ya route ya dar-arusha imekutana na shughuli hiyo ya kumsitiri huyo mzee so let's take it as simple as lunar eclipse.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…