Kesho wanafunzi wa chuo kikuu cha dar es salaam wanaanza mgomo rasmi.

Perry

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
10,058
Reaction score
2,195
Hii ni kutokana na kucheleweshewa pesa zao za chakula na malazi,vilevile wanadai mazingira mazuri ya kusomea na malazi.matangazo ya kuhamasisha mgomo,yamezagaa kila kona ya chuo,wanafunzi wote wamehamasishwa kufika revolution square kabla ya saa 1 asubuhi,rout itakua ni kuelekea ikulu kumuona mheshmiwa rais kufikisha malalamika yao.
 
Hawawezi,migomo ilikua long

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
UDSM ilikuwa zamani leo hii watoto wengi sana so mtaishia hapo hapo square hamtaenda popote.
 
mmmh!ikulu moja kwa moja...hakuna mwendaji hapo!
 
matangazo yamewekwa lini na wapi nilikua chuo adi jana usiku sikuona kitu.
 
Ila msivunje chupa kafteria ni za mjuni na si za mkandala wala bodi
 
Wakishaanza kujitokeza waoga kama wewe hakuna mgomo hapo....

But mjiandae na vitu vyenye ncha kali maana Kova naye anatamani kuwa IGP siku moja

uoga wangu kutokuona tangazo au!!? ukishakua udsm ata kama ulikua muoga kiasi gani utakua jasiri tu "SOLIDARITY FOREVER".
 
labda wagome kula tu,
ila sio migomo ile ya UDSM ya kipindi kileeee
 
udsm disunity ni kubwa akuna cha mgomo wala nini,,,watu wanang'ang'ana kukopa kwa washikaj wakati ela yao inakaa tuu bodii,,,mi naamin ata hiyo kesho amna jipya,,
 
Hawa vijana wanaovaa mlegezo wanajua kugoma kweli? lamda wagome kula kama alivyosema mchangia mmoja hapa. Haya tungoje tuone
 
Mgomo wa mwisho wa kueleweka kabisa kwa udsm ulikua wa mwaka 2008 tukiwa na kina Mtatiro, baada ya hapo zimebaki kelele tu.
 
Hawa vijana wanaovaa mlegezo wanajua kugoma kweli? lamda wagome kula kama alivyosema mchangia mmoja hapa. Haya tungoje tuone

Kuna mgomaji basi hapo? Aaghr mi sijui ngoja tungoje kama ulivyomalizia hapo mwisho.
 
chuo kichafu,sijui ni wanafunzi ndo wachafu,vyooni jamani,hall2 ni balaaa,vyoo vya pale ATB,HATARIIIIII
 
Kiukwel inaumuza sana dada zetu wanazaririka kwa kukosa fedha za kujikim so nawatakia mafanikio mema ktk maandamano hyo ila tu yawe ya aman.
 
Wenzenu tulikuwa tunagoma alhamic mpaka ijumaa, then tunaendelea next week. kukwepa ile sheria ya siku tatu za mgomo kupelekea kufungwa chuo.

Mkianza j3 ikifika j5 hamjaingia class chuo kinafungwa.. na hapo inakuwa imekula kwenu.
 
mahine....Eti mgome?
Hakuna mgomaji hapo.Eti unapita chuo unasikia wanachuo wanasikiliza nyimbo za diamond!
 
Naona mlio wengi mmejikina na maneno hawawezi, wataishia hapo hapo n.k.
Naona watu bado wanachuki kwenye nyoyo zao dhidi ya UDSM(tuachane nayo hayo). Pengine nahisi labdo ni njaa imewapana huko waliko na wanaona watumie njio hio kuwaongezea hasira wanaudsm, wakiwa na malengo kua mafanikio watapata wote!
Acheni mawazo finyu. Tambueni kua mgomo ulioanzisha na UDSM uliozaa matunda ya kupanda kwa bumu uliungwa mkono na wanachuo makini wa vyuo vyote Tz.
Mimi naona mngeungana na kutetea haki yanu mkiwa kama kitu kimoja. Tambueni umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
 
Mgomo wa mwisho wa kueleweka kabisa kwa udsm ulikua wa mwaka 2008 tukiwa na kina Mtatiro, baada ya hapo zimebaki kelele tu.

Wa 2010 pia ulitikisa..kutoka 5000 hadi 7500 si mchezo.. ni mgomo pekee wa udsm huko youtube..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…