KESHO YA SIMBA NI BORA KULIKO LEO YA YANGA

KESHO YA SIMBA NI BORA KULIKO LEO YA YANGA

Upo sahihi..simba wanajitafuta...ila wakati wanajitafuta kuna mwenzie anatumia hali yenu ya kujitafuta kujitengenezea ufalme wa vikombe na heshima juu yenu..sasa miaka miwili ijayo wachezaji mliowatengemeza wataamza kusambaa kwingine kwa mikataba kuisha au kudakwa na timu zingine..mana mikataba mingi ni miaka 2 au 3..wakati huo nao washajanjaluka kiwango kizuri..kwahiyo future ya club zetu hizi ni uimara kiuchumi na kiuongozi kisha kupata wachezaji wazuri na wazoefu..timu hizi kubwa hazilei sana vijana, hapa mashabiki wanataka mchezaji avumiliwe msimu mmoja au awe vema mwanzoni kabisa
 
View attachment 3130558Ni kweli Simba kafungwa mechi 4 mfululizo na kapoteza ubingwa mara 3 mfululizo lakini haiondoi ukweli kwamba muelekeo wa ni sahihi na wanakaribia kuupata ule ubora wao wa misimu minne iliyopita.

Simba kwa sasa haifungwi kwa makosa ya kiufundi ya Timu nzima bali inafungwa kwa makosa ya kibinadamu ya mchezaji mmoja mmoja kitu ambacho timu yoyote inaweza kupitia hiyo hali.

Tazama magoli yaliyoikesha alama 2 za Coastal Union kisha tazama bao la jana utagundua kwamba magoli waliyofungwa sio ya kitimu.

Hii ni hatua nzuri kwa ujenzi wa Timu na wanapaswa kutulia na kuongeza wachezaji wachache sana kwenye usajili dirisha lijalo.

Ukitoa bao la kujifunga hakuna moment ambayo Simba walionekana kuzidiwa na kuonesha utofauti wa daraja la ubora kati yao na Yanga ambao wana kikosi kilichokaa pamoja kwa muda mrefu.

Wakati Simba wanaanza kushuka na Yanga kutawala soka la Tanzania hivi karibuni dalili zilikuwa hizi hizi...kutoka kushinda kwa mbwembwe hadi kuomba Mungu mechi iishe.

Siku za mashabiki wa Simba kufurahi haziko mbali...na siku za mashabiki wa Yanga kutoka kinyonge Lupaso zipo karibuni.

Inaweza isiwe leo au kesho lakini hata Yanga wenyewe wanajua kuwa Simba hii sio ya miaka miwili nyuma...wameimarika sana!

✍️Sospeter Ilagila.
Endeleeni tu kujiliwaza kila msimu Yanga wachezaji bora wanaingia. Yanga haijakalili kukaa na wachezaji kama Simba. Msimu ujao kuna maingizo mapya kama kawaida. Mtasubiri sana na hao under 17 wenu.
 
Mimi ni simba ila ukweli ni kwamba timu ni dhaifu,uongozi ni dhaifu.Hakuna uimara nje na ndani ya uwanja kwa Simba.
Na yanga ataendelea kutufunga.
Simba uhuni, ujanja ujanja mwingi
 
Kwakweli inabidi nijitafakari kwanini Simba wanafungwa mara 4 mfululizo wakati Yanga ikiwa unga na wanajitafuta kipindi hicho hakuwa wanyonge kiasi cha kukubali kiwa wateja wa kufungwa tu kila mchezo na Simba. Najitafakari sana mkuu huyu Gamondi
🚮
 
Kaka Yanga wapo smart sana kwenye kujenga timu. Angalia replacements za wachezaji zinavyofanyika.

Sitegemei Yanga kushuka kiwango miaka ya karibuni ila nategemea kuwa na Simba imara na Yanga imara miaka ya karibuni.

Japo wanaonitia wasiwasi hapo Simba ni aina za viongozi walionao, wanamanage timu kisela sana. Imagine mpo kwenye kipindi cha kujenga timu na kuleta umoja anajitokeza kiongozi tena anapost hadharani kabisa akimtumuhumu Kipa amehujumu mechi.
 
View attachment 3130558Ni kweli Simba kafungwa mechi 4 mfululizo na kapoteza ubingwa mara 3 mfululizo lakini haiondoi ukweli kwamba muelekeo wa ni sahihi na wanakaribia kuupata ule ubora wao wa misimu minne iliyopita.

Simba kwa sasa haifungwi kwa makosa ya kiufundi ya Timu nzima bali inafungwa kwa makosa ya kibinadamu ya mchezaji mmoja mmoja kitu ambacho timu yoyote inaweza kupitia hiyo hali.

Tazama magoli yaliyoikesha alama 2 za Coastal Union kisha tazama bao la jana utagundua kwamba magoli waliyofungwa sio ya kitimu.

Hii ni hatua nzuri kwa ujenzi wa Timu na wanapaswa kutulia na kuongeza wachezaji wachache sana kwenye usajili dirisha lijalo.

Ukitoa bao la kujifunga hakuna moment ambayo Simba walionekana kuzidiwa na kuonesha utofauti wa daraja la ubora kati yao na Yanga ambao wana kikosi kilichokaa pamoja kwa muda mrefu.

Wakati Simba wanaanza kushuka na Yanga kutawala soka la Tanzania hivi karibuni dalili zilikuwa hizi hizi...kutoka kushinda kwa mbwembwe hadi kuomba Mungu mechi iishe.

Siku za mashabiki wa Simba kufurahi haziko mbali...na siku za mashabiki wa Yanga kutoka kinyonge Lupaso zipo karibuni.

Inaweza isiwe leo au kesho lakini hata Yanga wenyewe wanajua kuwa Simba hii sio ya miaka miwili nyuma...wameimarika sana!

✍️Sospeter Ilagila.
Kesho yake wachezaji wazuri watachukuliwa na timu bora na Simba watasubiri wanaomaliza mikataba!
 
Back
Top Bottom