Kesi inakuzwa;inapotoshwa

Kesi inakuzwa;inapotoshwa

Mtu katolewa jicho huko unasema hakuna bifu?

Tuhuma za hongo, magari, pesa na ukiritimba zimejaa kibao kwa pande zote, uongozi wa CHADEMA unaoburuzana na Zitto, na Zitto mwenyewe.

Unasema hakuna bifu?

Mipasho mpaka Facebook, mtu mzima anasema "I will not die" kama Farao wa zama hizi.

Halafu unasema hamna bifu?

Wewe kama vegetarian sema tu, lakini usiseme hamna bifu.
 
Je,kama sio mistake aliyoifanya Kibatala kama ilivyogunduliwa na Jaji na sio kupanguliwa na Msando ina maana rufani ya Zitto isingesikilizwa?yaani Kamathj Kuu ingeruhusiwa kumjadili uanachama wake?
 
Hoja kuu zilizompeleka Zitto Z.Kabwe mahakamani ni mbili.Kwanza, kuizuia Kamati Kuu ya CHADEMA kumjadili juu ya uanachama wake kufuatia barua aliyopokea ikibeba tuhuma 11 dhidi yake.Pili, kuiomba Mahakama imuamuru Katibu Mkuu wa CHADEMA kumpatia Zitto mwenenndo wa shauri lake ndani ya Kamati Kuu(siku alipovuliwa wadhifa wake) ili Zitto aweze kukata rufaa katika Baraza Kuu la CHADEMA. Hivyo tu. Lakini,kinachoripotiwa ni tofauti. Hatuwezi kunyamazia upotofu.

Kesi hii imekuwa ikiripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini na nje kwa kukuzwa na kupotoshwa sana. Inazungumzwa kana kwamba ni vita ya kufa au kupona kwa mmoja wa pande za kesi hiyo. Kama si Zitto basi CHADEMA.Kwamba,baada ya hukumu ya leo ya Jaji Utamwa, Zitto au CHADEMA ataibuka kidedea na mwenzake atakuwa ameanguka na kuangamia kabisa.

Upotofu huu ndio uliosababisha yanayoshuhudiwa sasa.Kwamba eti kuna kundi la Zitto na CHADEMA. Kwamba eti kuna vurumai kubwa kati ya makundi hayo. Hakuna haja ya vurugu.Hakuna haja ya sherehe.Hakuna haja ya bifu. HAKUNA haja ya kujipongeza au kusikitika.Haki haihitaji uadui.

Kwa matokeo yoyote ya kimahakama leo, bado michakato ya kichama itaendelea.Kama Mahakama itakubaliana na maombi ya Zitto,basi kikao cha Kamati Kuu hakitamjadili juu ya uanachama wake.Pia, Zitto atapewa mwenenndo na Katibu Mkuu wa CHADEMA na kukata rufaa Baraza Kuu la CHADEMA.

Kama Mahakama itakataa maombi ya Zitto, Kamati Kuu yaweza kuitishwa na kumjadili Zitto hasa kuhusu uanachama wake kuhusiana na tuhuma zilizopo dhidi yake. Kwa namna yoyote iwayo, CHADEMA itaendelea kuwepo. Itaendelea na michakato yake kichama na kisiasa.

Kesi inafaa isomeke "Zitto Vs Kamati kuu ya Chadema" na si "Zitto Vs Chadema"
 
Kwa hilo bw petro,umenrna jambo la msingi sna.tatizo letu wabongo ni kukuza mambo ya kizushi na kutashabikia.
 
Hoja kuu zilizompeleka Zitto Z.Kabwe mahakamani ni mbili.Kwanza, kuizuia Kamati Kuu ya CHADEMA kumjadili juu ya uanachama wake kufuatia barua aliyopokea ikibeba tuhuma 11 dhidi yake.Pili, kuiomba Mahakama imuamuru Katibu Mkuu wa CHADEMA kumpatia Zitto mwenenndo wa shauri lake ndani ya Kamati Kuu(siku alipovuliwa wadhifa wake) ili Zitto aweze kukata rufaa katika Baraza Kuu la CHADEMA. Hivyo tu. Lakini,kinachoripotiwa ni tofauti. Hatuwezi kunyamazia upotofu.

Kesi hii imekuwa ikiripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini na nje kwa kukuzwa na kupotoshwa sana. Inazungumzwa kana kwamba ni vita ya kufa au kupona kwa mmoja wa pande za kesi hiyo. Kama si Zitto basi CHADEMA.Kwamba,baada ya hukumu ya leo ya Jaji Utamwa, Zitto au CHADEMA ataibuka kidedea na mwenzake atakuwa ameanguka na kuangamia kabisa.

Upotofu huu ndio uliosababisha yanayoshuhudiwa sasa.Kwamba eti kuna kundi la Zitto na CHADEMA. Kwamba eti kuna vurumai kubwa kati ya makundi hayo. Hakuna haja ya vurugu.Hakuna haja ya sherehe.Hakuna haja ya bifu. HAKUNA haja ya kujipongeza au kusikitika.Haki haihitaji uadui.

Kwa matokeo yoyote ya kimahakama leo, bado michakato ya kichama itaendelea.Kama Mahakama itakubaliana na maombi ya Zitto,basi kikao cha Kamati Kuu hakitamjadili juu ya uanachama wake.Pia, Zitto atapewa mwenenndo na Katibu Mkuu wa CHADEMA na kukata rufaa Baraza Kuu la CHADEMA.

Kama Mahakama itakataa maombi ya Zitto, Kamati Kuu yaweza kuitishwa na kumjadili Zitto hasa kuhusu uanachama wake kuhusiana na tuhuma zilizopo dhidi yake. Kwa namna yoyote iwayo, CHADEMA itaendelea kuwepo. Itaendelea na michakato yake kichama na kisiasa.

hatuwezi kukwepa ukweli,hiyo ndio hali halisi.kwa yeyote yule atakayeshinda ushindi utashangiliwa kama vile mechi ya yanga na simba,hata kama ni mechi ya mtani jembe bado maudhui yake na mihemuko itasimama na kuleta hisia zilezile
 
Mbona kuna wanaosema kuwa chadema imeshindwa katika kesi mahakamani leo?ebu tujuzeni mliopo mahakamani.

Mkuu ni mitizamo tuu...kiukweli zit to kashinda,kapewa Nafasi ya kusikilizwa na baraza kuu...pia chadema imeamriwa kufuata huo utaratibu,ikumbukwe kuwa sio kuwa cdm imeshindwa ila imeamriwa kufuata utaratibu iliouweka yenyewe....pia kesi imekuwa based kwenye makosa ya wakili ambaye pia ni afisa wa iyo mahakama,vivo basi zit to kashinda ,kapewa haki ya kusikilizwa!,
 
Back
Top Bottom