Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

Huyu shule yake (both formal and informal) inaonekana kuwa ndogo, au vipi?

Ni kama ulikuwa katika mawazo yangu mkuu kwani mtu aliyekuwa na cheo kama cha huyu hategemewi kufanya haya.lakini pia mi naona pengine kuna kitu anatumia na kinafanya akili isifanye kazi kwa mwendo wa kawaida maana inaonekana ni kama haziko timamu.
 
Polisi kupigiana simu siyo tatizo,kwa sababu Kampuni ya simu yoyote inaweka record ya mazungumzo yote ya simu yanayofanywa.
Lakini mimi napinga Serkali kupinga uamuzi wa Mahakama kumuachia huru Zombe. Napinga kusema kwamba Mahakama siyo Serikali,kusema kwamba Mahakama siyo sehemu ya uongozi wa Nchi hii.
Kama Mahakama imeridhia utendaji kazi wa Zombe na wenzake,kama Mahakama ina imani na utendaji wa Polsi katika kuwakabili wahalifu,basi Serkali inapaswa kuwa na imani na Mahakama.
Kwa sababu Jaji ana uzoefu mwingi sana katika kazi yake; ya kusamehe watu na kuadhibu watu;na kutathmini athari za kusamehe watu,[au kuamua hawana hatia]na kutathmini athari za kuadhibu watu. Kwa hiyo Jaji lazima aachiwe afanye kazi yake. Kama Serikali itaonyesha wasiwasi na Mahakama,hizo kesi nyingine za ufisadi zitafanyika vipi?
Pia sio sahihi kusema kwamba Polisi hawezi kufanya extra judicial killing. Polisi wanaruhusiwa kufanya extra judicial killing,na wanafanya hivyo mara nyingi. Mara nyingi Polisi wanafanya extra judicial killing wanapopambana na magenge ya wahalifu,kama,kwa mfano, Mafia.
Pia huyo Zmbe amekaa kizuizini miaka mitatu. Mtu wa heshima yoyote,ukimtishia kwenda jela miaka mitatu,ataogopa kufanya kosa. Mtu wa heshima hataki kabisa kufika kituo cha Polisi kwa kosa lolote lile.
 
Hawa watu wataendelea kutuchezea tu na pesa zinaenda...

Hilo ndilo swala nililiongea jana kwamba hawa wanataka kutumbua pesa zetu tu hawana lolote hawa ndugu zangu wanatufanya vipofu hatuoni jamani hata kusikia pia au tumekua mabubu pia.
 
Tumechoka na kusikiliza na kusoma mabandiko ambayo actually ni mawazo ya watu. Twambie kwamba umeambiwa na masha au nani siyo unaleta mawazo yako hapa. Katika majeshi yote, hizo nyenzo ulizosema zinatumika tu iweje tanzania zisitumike.

Ni juzi tu wanajeshi wa marekani walioko Afghanstan, waliokuwa kwenye helicopter gunship wakienda kwenye jimbo la Helmand, waliambiwa na mwenzao anayeanalyse picha za satellite kwa simu ya upepo kuwa warudi eneo fulani kulikuwa na talibani wanachimbia bomu (IED) kwenye barabara moja na walirudi na kuwaona watu hao na kuwaua kwa helicopter guns na misiles. Je, kwa mawazo yako potofu watu waliokuwa kwenye helicopter wangesubiri wapewe amri/taarifa kwa maandishi na wako angani sijui ingekuwaje!!

Jaribu kufikirisha akili yako.
 
Tugange yajayo wananchi,tuachane na hivyo vituko vyao!Vyovyote wanavyopanga/walivyopanga ni juu yao wenyewe!
Wanajishtaki wenyewe,hukumu wanajipa wenyewe,huru wanajiachisha wenyewe sisi hatuna say yoyote kwao...!!!
 
Zombe ana confo dunia nzimaa wajuaa....maana anajuaa maovu ya wenzake wote wakubwa....lazima awe na confo...hata huko keko alikuwa ana confo hadi kumzidii mkuu wa gereza uliza......
Sasa wewe kuweka bango la presida wa Amerika kama utambulisho wako ndio nini?Aibu, mtu mzima ovyo,wadudu wadogowadogo wananyevuanyevua.Badilika jali utaifa wako acha kushabikia mambo ya walami huko majuu,angalia jamaa hao wameanza mchezo mbaya kwa waafrika wanaowaiga,ooohh usije ukaitwa 'rafiki'
 
WATAALAMU wa sheria wamesema aliyekuwa Kamanda wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na wenzake tisa waliaochiwa huru katika kesi ya mauaji, hawawezi kushitakiwa tena kwa kosa hilo.

Kauli ya wanasheria hao imetokana na kuwapo kwa taarifa kuwa, serikali inakusudia kukata rufani, kutokana na kutoridhishwa na uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, uliotolewa Jumatatu wiki hii wa kuwaachia huru.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Salum Massati, aliwaachia huru Zombe na wenzake, waliokuwa wakidaiwa kuwaua wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge, Morogoro na dereva wa teksi, kutokana na upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao.

Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Harold Sungusia, alisema kisheria hakuna nafasi tena kwa upande wa Jamhuri kutoa ushahidi mpya, hata kama anayetafutwa kwa mauaji hayo akikamatwa, hivyo njia pekee ni kukata rufani.

"Hata kama aliyeua akikamatwa kama Mahakama Kuu ilivyoagiza, Zombe na wenzake wanaweza kuitwa kutoa ushahidi tu na si kushitakiwa kwa kuwa itakuwa ni kukiuka misingi ya haki za binadamu, na endapo watafikishwa mahakamani, wataachiwa huru tena," alisema Sungusia.

Kwa upande wake, Wakili Domitian Rwegoshora wa Kampuni ya Uwakili ya MK Partners ya Dar es Salaam, alisema: "Hukumu yoyote ya kesi inatokana na ushahidi unaotolewa, kesi ya mauaji adhabu yake ni kubwa, hivyo kwa ushahidi dhaifu mahakama haiwezi kuwatia hatiani washitakiwa".

Naye Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa CHADEMA, Tundu Lissu, alisema hukumu hiyo ilitokana na udhaifu wa Jeshi la Polisi katika kufanya upelelezi.

Lissu alisema wanaopaswa kubeba mzigo ni Jeshi la Polisi, kwa kuwa halina wataalamu wa kisasa wanaoweza kuchunguza makosa ya jinai, hivyo kuwasilisha ushahidi usiojitosheleza.

"Sheria za nchi zote zinataka ili mtu atiwe hatiani kwa kosa la jinai ni lazima kuwe na ushahidi usio acha shaka yoyote kwa mtuhumiwa," alisema Lissu.

Alisema ingawa hajaisoma hukumu ya jaji iliyowaachia huru watuhumiwa hao, lakini anafikiri alichokitumia ni ushahidi uliowasilishwa, hivyo kama haukujitosheleza hawezi kutoa hukumu isiyo na haki.

Wengine walioachiwa huru ni Christopher Bageni, Ahmed Makelle, Rajab Bakari, Philipo Gwabisabi, Jane Andrew, Emmanuel Mabula, Michael Shoza na Abeneth Saro.

Walikuwa wakituhumiwa kuwaua wafanyabiashara wa madini Sabinus na Ephraim Chigumbi, Mathias Lunkombe na dereva wa teksi Juma Ndugu.

Mauaji hayo yalifanyika msitu wa Pande, mkoani Dar es Salaam, Januari, 2006.
 
Una hakika hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kumwaga ubongo wa mtu?

Tumwachie Mungu. Zombe anaweza kuwa ameathirika sana kisaikolojia, Aidha kwa kutuhumiwa kuua au kwa kuua kweli. Zipo sababu kadhaa za kunifanya niamini Zombe kwa sasa si yule wa zamani.

Amepoteza kazi, ameandikwa mara nyingi magazetini tena vibaya, amekaa gerezani (hata kama alikuwa anakula na kulala vizuri - hakuwa huru), amepoteza umaarufu wake, nk. Naamini shughuli zake nyingi alizohitaji kusimamia mwenyewe zilikwama na hivyo kupunguza kipato chake alichokuwa amezoea.

Lazima AMECHANGANYIKIWA!!!!
 
Hi si kweli na sidhani kama huyu aliyekuambia ni afisa wizara ya mambo ya ndani.

Jamhuri ya muungano inmihimili mitatu yaani Bunge,mahakama na serikali(executives).

Na mihimili hii haingiliana kiutendaji wala kimaamuzi. leo inakuwaje eti mahakam imeingiliwa katika maamuzi na serikali?

Nadhani mtoa hoja akajipanga upya kwa hili,nadhani serikali walitakiwa kuwa makini katika shitaka lao hasa katika upelelezi,haingii akilini eti waliangizwa kwa mdomo wakawaue raia wema, wakati kazi ya jeshi la polisi ni kulinda maisha ya raia wema na mali zao.
 
Ni kweli Zombe hawezi kushtakiwa tena labda mahakama ya Rufaa itoe maelekezo ya kurudiwa kwa kesi lakini that is not easy verdict to come up with unless there is serious procedural error during the hearing of the case. Kuna principle katika criminal law inasema mtu akishtakiwa na mahakama na kuonekana hana hatia hawezi kushtakiwa tena. hiyo principle inaitwa autrefois acquit which mean previously acquitted by a court of competent jurisdiction of the same or substantially the same offence with which he is now charged.

lakini jeshi la polisi laweza mchukulia hatua Zombe kwa kutoa taarifa za uongo au bila kudhibitisha kwa kusema waliokufa ni majambazi wakati sio kweli. that could lead to his demotion or some measures be taken.
 
i still believe kuwa udhaifu wa jeshi letu la polisi ndio chanzo cha yote haya.mi naona wanatapatapa tu maa impact ya hii kitu ni kubwa sana pasipo wao kutarajia.Jaji Masati alikuwa very clear katika hukumu yake na ameliagiza jeshi la polisi kumtafuta aliyetekeleza mauaji hayo...
 
Ni kweli Zombe hawezi kushtakiwa tena labda mahakama ya Rufaa itoe maelekezo ya kurudiwa kwa kesi lakini that is not easy verdict to come up with unless there is serious procedural error during the hearing of the case. Kuna principle katika criminal law inasema mtu akishtakiwa na mahakama na kuonekana hana hatia hawezi kushtakiwa tena. hiyo principle inaitwa autrefois acquit which mean previously acquitted by a court of competent jurisdiction of the same or substantially the same offence with which he is now charged.

lakini jeshi la polisi laweza mchukulia hatua Zombe kwa kutoa taarifa za uongo au bila kudhibitisha kwa kusema waliokufa ni majambazi wakati sio kweli. that could lead to his demotion or some measures be taken.

Umesema sawa, lakini bado watuhumiwa hawa wanaweza kukutwa na hatia ya mauaji kama Mahakama ya Rufaa ya Tanzania itafikia uamuzi kwamba Mahakama Kuu ya Tanzania haikuzingatia ushahidi fulani uliotolewa wakati shauri lilipokuwa linasikilizwa, na kwamba upande wa mashtaka ulithibitisha madai yao bila ya kuwa na shaka lolote (beyond a reasonable doubt). Rufaa zote zinazokatwa kwenda Mahakama ya Rufaa ni "on a point (s) of law" na sio "facts". Mahakama Kuu ya Tanzania ilikuwa "Trial Court" katika shauri hili kwa kuwa ndio mahakama yenye uwezo kisheria wa kusikiliza mashauri ya mauaji. Rufaa zingine zinazopelekwa Mahakama Kuu toka mahakama za chini, pia husikilizwa "point(s) of law" katika rufaa na sio "facts".
 
WATAALAMU wa sheria wamesema aliyekuwa Kamanda wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na wenzake tisa waliaochiwa huru katika kesi ya mauaji, hawawezi kushitakiwa tena kwa kosa hilo.

Kauli ya wanasheria hao imetokana na kuwapo kwa taarifa kuwa, serikali inakusudia kukata rufani, kutokana na kutoridhishwa na uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, uliotolewa Jumatatu wiki hii wa kuwaachia huru.

Jaji wa Mahakama ya Rufani, Salum Massati, aliwaachia huru Zombe na wenzake, waliokuwa wakidaiwa kuwaua wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge, Morogoro na dereva wa teksi, kutokana na upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao.

Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Harold Sungusia, alisema kisheria hakuna nafasi tena kwa upande wa Jamhuri kutoa ushahidi mpya, hata kama anayetafutwa kwa mauaji hayo akikamatwa, hivyo njia pekee ni kukata rufani.

"Hata kama aliyeua akikamatwa kama Mahakama Kuu ilivyoagiza, Zombe na wenzake wanaweza kuitwa kutoa ushahidi tu na si kushitakiwa kwa kuwa itakuwa ni kukiuka misingi ya haki za binadamu, na endapo watafikishwa mahakamani, wataachiwa huru tena," alisema Sungusia.

Kwa upande wake, Wakili Domitian Rwegoshora wa Kampuni ya Uwakili ya MK Partners ya Dar es Salaam, alisema: "Hukumu yoyote ya kesi inatokana na ushahidi unaotolewa, kesi ya mauaji adhabu yake ni kubwa, hivyo kwa ushahidi dhaifu mahakama haiwezi kuwatia hatiani washitakiwa".

Naye Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa CHADEMA, Tundu Lissu, alisema hukumu hiyo ilitokana na udhaifu wa Jeshi la Polisi katika kufanya upelelezi.

Lissu alisema wanaopaswa kubeba mzigo ni Jeshi la Polisi, kwa kuwa halina wataalamu wa kisasa wanaoweza kuchunguza makosa ya jinai, hivyo kuwasilisha ushahidi usiojitosheleza.

"Sheria za nchi zote zinataka ili mtu atiwe hatiani kwa kosa la jinai ni lazima kuwe na ushahidi usio acha shaka yoyote kwa mtuhumiwa," alisema Lissu.

Alisema ingawa hajaisoma hukumu ya jaji iliyowaachia huru watuhumiwa hao, lakini anafikiri alichokitumia ni ushahidi uliowasilishwa, hivyo kama haukujitosheleza hawezi kutoa hukumu isiyo na haki.

Wengine walioachiwa huru ni Christopher Bageni, Ahmed Makelle, Rajab Bakari, Philipo Gwabisabi, Jane Andrew, Emmanuel Mabula, Michael Shoza na Abeneth Saro.

Walikuwa wakituhumiwa kuwaua wafanyabiashara wa madini Sabinus na Ephraim Chigumbi, Mathias Lunkombe na dereva wa teksi Juma Ndugu.

Mauaji hayo yalifanyika msitu wa Pande, mkoani Dar es Salaam, Januari, 2006.

Wanasheria kibao lakini hawaelezi sababu ya kisheria ya kwa nini hawezi kushitakiwa tena.
 
Last edited:
... hiyo principle inaitwa autrefois acquit which mean

Hiyo misingi ya common law sio lazima iwe na mamlaka kila mahala!

Huwezi kwenda mbele ya jaji ukaibua principle la common law kutoka vitabu vya shuleni, atakwambia nionyeshe panapoipa mamlaka hiyo sheria yako katika mahakama yangu!

Kuna mwanasheria hapo juu kasema Zombe hawezi kushitakiwa tena kwa sababu za haki za binadamu, kituko! Sheria ya Tanzania inasemaje? Sio misingi ya dini na haki au misingi ya vitabu vya shule, sheria ya nchi.
 
Haya yote yalionekana tokea mwanzo isipokuwa watu wengi walisukumwa na hisia zao na mategemeo ya kusikia kile walichopenda kusikia mpaka kutupilia mbali misingi ya kisheria na hii inatokea katika mijadala mingi siku hizi hapa bongo.

Nikilinganisha na kile ninachokiona katika channel ya CI-criminal investigations (DSTV) mara nyingi nakubaliana kabisa na wachangiaji wengi kwamba mapungufu makubwa yako katika jeshi la polisi na waendesha mashitaka kwamba hawafanyi kazi zao kwa kiwango kinachotakiwa kiasi kwamba wakifika mahakamani wanafika na kesi zisizo kamili.

Kukamata watu wasio na hatia na kuwaweka lupango kwa zaidi ya miaka mitatu hata kama ungalikuwa wewe ni usumbufu mkubwa. Media kama kawa inaendelea pia kukandamiza watu wasio na hatia kwa kuuza habari na upeo mdogo wa waandishi na wamiliki pia utaendelea kuathiri watu wengi kama hatukuchukua hatua sasa.
 
Kukata rufaa sio kushtaki upya.. whoever wrote this is unfamiliar with the workings of "autrefois acquit"
 
Mh. Judge. S. Massati alieleza katika hukumu yake kuwa kesi iliyo mbele yake ni ya mauaji hivyo kazi yake ilikuwa kumhukumu muuaji, DPP anaweza kuwafungulia watuhumiwa kesi ya kupanga au kubuni au kushiriki utekelezaji wa mauaji (Conspirancy to murder) lakini sio kuuwa.
 
Back
Top Bottom