Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

Maendeleo soma hapa kutoka gazeti la mwananchi

Kesi ya Zombe sasa ni hadi Februari mwakani
Na Nora Damian

KESI ya mauaji ya wafanyabiashara watatu wa Mahenge na dereva teksi, inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam ACP, Abdallah Zombe na wenzake 12 inatarajia kuendelea kusikilizwa mwezi Februari mwakani.


Akizungumza na gazeti hili jana, Msajili wa Mahakama Kanda ya Dar es Salaam, Saul Kinemela alisema kesi hiyo itaendelea kusikilizwa baada ya uzinduzi wa mwaka mpya wa mahakama.


Septemba 26 mwaka huu kesi hiyo iliahirishwa na Jaji Kiongozi Salum Massati baada ya upande wa mashitaka kufunga ushahidi ambapo jumla ua mashahidi 37 walitoa ushahidi.


Hata hivyo upande wa utetezi uliwasilisha ombi mahakamani hapo ukitaka shahidi wa 22 Mrakibu wa Polisi (SP) Juma Bwire ambaye ni mtaalamu wa uhunguzi wa silaha makao makuu ya Jeshi la Polisi aitwe tena kutoa ushahidi.


Upande wa utetezi unataka shahidi huyo aitwe tena ili atatue utata uliojitokeza kuhusu sampuli zilizopelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kama zilitokea katika tukio la Sinza au msitu wa Pande.


Washitakiwa hao walifikishwa mahakamani mwaka 2006 baada ya wananchi kulalamika kuwa waliouawa hawakuwa majambazi.


Wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge na dereva teksi mmoja wa Manzese ambao wanaodaiwa kuwa majambazi waliuawa Januari 14 mwaka 2006 kwa maelezo kuwa ni majambazi.


Baada ya malalamiko kuzidi Jeshi la polisi liliunda tume kuchunguza sakata hilo lakini kabla halijamaliza uchunguzi wake, Rais Jakaya Kikwete aliunda tume ambayo iliongozwa na Jaji Kipenka.


Uchunguzi wa tume hiyo ndio iliosababisha kufunguliwa kwa kesi hiyo ambayo mbali na Zombe, washtakiwa wengine ni Rashidi Lema na Rajabu Bakari.


Wengine ni SP Christopher Bageni, ASP Ahmed Makelle, F.5912 PC Noel Leonard, WP 4593 PC Jane Andrew, D6440CPL Emmanuel Mabula, E6712 CPL Felix Cedrick, D8289 PC Michael Sonza, D 2300CPL Ebeneth Saro na D.1367 D/CPL Festus Gwabisabi.

shukrani mkuu maana wangeweza kutumia hiki kipindi kufunika kombe mwanaharamu apite-
 
shukrani mkuu maana wangeweza kutumia hiki kipindi kufunika kombe mwanaharamu apite-

kwa utaratibu wa kimahakama Tanzania, mwezi wa 11 & 12 kesi huwa hazisikilizwi ni muda wa majaji kuwa likizo hutajwa 2. nisahihishwe kama nimekosea

Kwa watu kama kina Mramba ukikosa dhamana ndio hadi next year hiyo
 
Mshitakiwa Mkuu wa kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini na dereva taksi Abdalah Zombe na wenzake leo walipandiswa tena kizimbani kujibu mashtaka hayo huku mmoja wa washitakiwa hao Ramadhani Lema akionekana dhaifu sana kiafya.

Zombe akiteta na wakili wake
301.jpg




Mmoja wa washitakiwa kulia Ramadhani Lema choka mbaya!
300.jpg



Askari magereza akiwaonya akina Zombe waache vurugu mahakamani
299.jpg


Source: http://www.nifahamishe.com
 
Huyo mshitakiwa Lema kweli anaumwa, mpaka anapewa msaada kutembea. Pia kichwani kama ana mapele. Ukiugulia nje tu unapopata huduma za ndugu ni kazi, sasa kuugulia ukiwa kizuizini kweli ni hatari sana. Mola amsaidie apate nafuu ili aweze kuendelea vyema na kesi inayomkabili.
 
Leo tutaambiwa kama wanakesi ya kujibu au la? maendeleo yakoje?
 
Huyo mshitakiwa Lema kweli anaumwa, mpaka anapewa msaada kutembea. Pia kichwani kama ana mapele. Ukiugulia nje tu unapopata huduma za ndugu ni kazi, sasa kuugulia ukiwa kizuizini kweli ni hatari sana. Mola amsaidie apate nafuu ili aweze kuendelea vyema na kesi inayomkabili.
Kuna taarifa kuwa mshitakiwa Lema amefariki dunia huko gerezani...taarifa bado kuthibitishwa na maelezo zaidi yanapatikana hapa
 
Kuna taarifa kuwa mshitakiwa Lema amefariki dunia huko gerezani...taarifa bado kuthibitishwa na maelezo zaidi yanapatikana hapa

Daah! Huyu jamaa kama kweli kafariki ni pigo sana kwenye kesi ya kina Zombe, coz alikuwa shahidi muhimu sana (kama sikosei #11)...so hopefully kina Zombe watakuwa wanachekelea, Je, kutakuwa na mkono wa mtu re. Kunyweshwa sumu (slowly killing one)etc
 
Kuna taarifa kuwa mshitakiwa Lema amefariki dunia huko gerezani...taarifa bado kuthibitishwa na maelezo zaidi yanapatikana hapa

Nadhani tuvute subira mpaka itakapothibitishwa, nachelea yasije yakawa kama yale ya yule dada wa kihindi anayekabiliwa na kesi ya mauaji yeye na mumewe.
 
Kwa hiyo ina maana walikuwa wanavuta subira ili afe ushahidi strong ukosekane??? Was it a delay tactics purposely to serve Zombe and those who were involved in the killings?? Naomba Mungu asiwe amekufa ili apate kusema ukweli maana hata waliobaki kujitetea hakika kuna ambao hawana hatia na walitakiwa huyu Rashid Lema awaokoe. So what next??
 
Mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya mauaji ya
wafanyabiashara wa madini, Abdallah Zombe, ameiomba Mahakama Kuu aruhusiwe kutoa tena ushahidi wake mahakamani hapo ili kutoa ufafanuzi kuhusu baadhi barua alizodai kuwa zina utata. Barua hizo ni alizodai ziliandikwa na washitakiwa wenzake katika kesi hiyo wakiwa gerezani, ambazo zilielekezwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) wakati huo (Geofrey Shahidi) bila kufuata utaratibu wa kuzipitisha kwa Mkuu wa Gereza na zikiwa na tarehe zinazopishana.

Akiongozwa na wakili wake, Jerome Msemwa, Zombe ambaye wakati wa tukio alikuwa Kaimu Kamanda wa Polisi Dar es Salaam alidai mbele ya Jaji Salum Massati kuwa anaiomba mahakama imruhusu kutoa tena ushahidi kama ilivyoomba notisi ya wakili wake aliyoitoa Februari mwaka huu ili atoe ufafanuzi ambao hakuutoa wakati akijitetea awali. “Mheshimiwa Jaji naomba shahidi namba moja (Zombe) aje atoe tena ushahidi wake mahakamani hapa na naamini hii ni mahakama ya haki, lazima haki itendeke hivyo nyaraka hizo tulizoelezwa zipo kwa DPP ziletwe sasa hivi maana ofisi yake si mbali ili mteja wangu asikilizwe,” alidai Msemwa.

Wakati huo Zombe akiwa kizimbani tayari kutoa ushahidi tena, tafrani fupi ilizuka baada ya Zombe kutaka kujitetea mwenyewe kwa kumtaka Jaji asimamie haki itendeke kwa kusema; “Jaji naamini hii ni mahakama ya haki….” Hata hivyo, Jaji Massati alimtaka atulie kwani malumbano baina ya mawakili hayajafikia mwisho hadi kumwezesha shahidi kuingilia kati shauri.

Aidha, ombi hilo la kurudia utetezi wake, lilipingwa na mawakili wa serikali pamoja na mawakili wengine wa upande wa utetezi akiwamo, Gaudias Ishengoma anayemtetea mshitakiwa wa pili (Christopher Bageni) na Majura Magafu anayewatetea washitakiwa watano katika kesi hiyo kwa madai kuwa endapo barua hizo zitaletwa mahakamani kama kielelezo na Zombe akapewa nafasi ya kujitetea tena, akiwagusa washitakiwa wenzake, mahakama itoe nafasi ya wao kujitetea vilevile.

“Tunaomba suala hili liangaliwe kwa makini sana, wakati ule mawakili wa serikali walibaini kuwa nyaraka nyingine ni za bandia, tunaomba lisichukuliwe kirahisi, tunaomba maelezo ya kina yatolewe ili lisiathiri mwenendo mzima wa kesi,” alidai Magafu. Jaji Massati alisema atatolea uamuzi suala hilo leo saa nne asubuhi ili kujua kama atatoa utetezi tena au la, na akamruhusu shahidi pekee wa Zombe kutoa ushahidi mahakamani hapo.

Shahidi huyo, Mkuu wa Gereza la Ukonga, Samwel Nyakitina (59) akitoa ushahidi wake uliolenga kuieleza mahakama anachofahamu kuhusu utaratibu wa wafungwa na mahabusu kutembelewa gerezani au uandikaji wa barua na washitakiwa kumiliki simu na fedha baada ya Zombe katika ushahidi wake wa awali kulalamikia baadhi ya washitakiwa wenzake walikamatwa na simu gerezani na barua na namna ambavyo aliandika barua za malalamiko kwa DPP na Waziri wa Mambo ya Ndani kupitia kwake, shahidi huyo alionyesha kuwa kinyume na matarajio ya Zombe. Sehemu ya mahojiano baina ya shahidi na Wakili Msemwa mbele ya mahakama hiyo yalikuwa kama ifuatavyo.

Wakili: Shahidi hebu ieleze mahakama utaratibu wa mfungwa au mahabusu kuandika barua na kuipeleka nje ya gereza ukoje.

Shahidi: Akishaandika barua inapita mapokezi kisha inakwenda ofisi ya Mkuu wa Gereza inagongwa mihuri na saini ndipo inaenda nje, bila hivyo inakuwa si halali na ni ngumu kutumika katika ofisi za serikali…..lakini sasa ni juu ya mwandikaji na mpokeaji huko nje.

Wakili: Unasema nini kuhusu barua ya Zombe ya Februari 14, 2007 kwenda kwa Jaji Mkuu Mfawidhi na ile ya kutoka kwa Zombe kwenda kwa Waziri wa Mambo ya Ndani akimlalamikia kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka amemtengenezea kesi ya mauaji?

Shahidi: (akiwa ameshika barua hizo) Saini ni kama yangu na mihuri ya Gereza la Ukonga, lakini sina ukakika nazo mpaka nikaangalie katika makabrasha yangu maana mmenishtukiza sikujiandaa.

Wakili: Unaiambia nini mahakama kuhusu vielelezo kama simu na fedha ulizowakuta nazo washitakiwa wakati kuwa na hivyo vitu gerezani ni kinyume cha sheria na taratibu za gereza.

Shahidi: (akatoa vielelezo ambavyo ni simu nne) siku ya tarehe 15/09/2006 siwezi kusema hapa mshitakiwa yupi alikamatwa na simu, labda mpaka nikaangalie katika majalada, lakini siku hiyo askari waliwapekua mahabusu 30 na waliotoka mahakamani na wafungwa zaidi ya 1,000 walioenda kazini kama utaratibu unavyoelekeza na walikutwa na simu nne na fedha taslimu Sh 153,000. Tukio hilo sina kumbukumbu zake zote hapa.

Awali katika ushahidi wake, mshitakiwa wa 13 ambaye ni wa mwisho katika kesi hiyo inayowakabili washitakiwa tisa hivi sasa, Festus Gwabisabi alidai kuwa alishiriki kuwapekua watuhumiwa waliouawa katika eneo la Sinza Palestina wakiwa hai siku ya tukio bila majibizano yoyote ya risasi na kwamba alishangaa kusikia kupitia vyombo vya habari siku mbili baadaye kuwa wameuawa.

Akiongozwa na wakili wake Longino Myovela, Gwabisabi alidai akiwa na Mkuu wa Upelelezi Kituo cha Urafiki, Ahmed Makelle, mshitakiwa wa tatu, alimpekua mtuhumiwa mmoja na kumkuta na bastola moja na mkoba mweusi waliodai una Sh milioni tano na kwa mara ya pili huo mkoba na bastola aliuona mezani kwa Zombe asubuhi ya Januari 15, 2006 walipoitwa kupongezwa kwa kazi nzuri ya kukamata majambazi.

Alidai pia kuwa Zombe aliwafundisha washitakiwa hao namna ya kujieleza pindi watakapoitwa kuhojiwa katika Tume ya Jaji Kipenka kuhusu tukio hilo kwamba waeleze kulikuwa na majibizano ya risasi katika Ukuta wa Posta, Sinza jambo ambalo yeye (shahidi) alilikataa kwani aliwakamata kwa amani bila majibizano na alishauri wapelekwe kituoni kuhojiwa, lakini hakujua walikopelekwa.

Zombe na wenzake wanatuhumiwa kuwaua Sabinus Chigumbi, Ephraim Chigumbi, Matius Lukombe na dereva taksi, Juma Ndugu katika msitu wa Pande, Mbezi Louis, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam Januari 14, 2006. Wakati kesi hiyo inaahirishwa Februari mwaka huu, Jaji Massati aliwaachia huru washitakiwa watatu ambao ni Noel Leonard, Moris Nyangelela na Felix Cedrick baada ya kuonekana kuwa hawana kesi ya kujibu kuhusu mauaji hayo.

SOURCE: Habari Leo
 
Mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya mauaji ya
wafanyabiashara wa madini, Abdallah Zombe, ameiomba Mahakama Kuu aruhusiwe kutoa tena ushahidi wake mahakamani hapo ili kutoa ufafanuzi kuhusu baadhi barua alizodai kuwa zina utata. Barua hizo ni alizodai ziliandikwa na washitakiwa wenzake katika kesi hiyo wakiwa gerezani, ambazo zilielekezwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) wakati huo (Geofrey Shahidi) bila kufuata utaratibu wa kuzipitisha kwa Mkuu wa Gereza na zikiwa na tarehe zinazopishana.

Akiongozwa na wakili wake, Jerome Msemwa, Zombe ambaye wakati wa tukio alikuwa Kaimu Kamanda wa Polisi Dar es Salaam alidai mbele ya Jaji Salum Massati kuwa anaiomba mahakama imruhusu kutoa tena ushahidi kama ilivyoomba notisi ya wakili wake aliyoitoa Februari mwaka huu ili atoe ufafanuzi ambao hakuutoa wakati akijitetea awali. “Mheshimiwa Jaji naomba shahidi namba moja (Zombe) aje atoe tena ushahidi wake mahakamani hapa na naamini hii ni mahakama ya haki, lazima haki itendeke hivyo nyaraka hizo tulizoelezwa zipo kwa DPP ziletwe sasa hivi maana ofisi yake si mbali ili mteja wangu asikilizwe,” alidai Msemwa.

Wakati huo Zombe akiwa kizimbani tayari kutoa ushahidi tena, tafrani fupi ilizuka baada ya Zombe kutaka kujitetea mwenyewe kwa kumtaka Jaji asimamie haki itendeke kwa kusema; “Jaji naamini hii ni mahakama ya haki….” Hata hivyo, Jaji Massati alimtaka atulie kwani malumbano baina ya mawakili hayajafikia mwisho hadi kumwezesha shahidi kuingilia kati shauri.

Aidha, ombi hilo la kurudia utetezi wake, lilipingwa na mawakili wa serikali pamoja na mawakili wengine wa upande wa utetezi akiwamo, Gaudias Ishengoma anayemtetea mshitakiwa wa pili (Christopher Bageni) na Majura Magafu anayewatetea washitakiwa watano katika kesi hiyo kwa madai kuwa endapo barua hizo zitaletwa mahakamani kama kielelezo na Zombe akapewa nafasi ya kujitetea tena, akiwagusa washitakiwa wenzake, mahakama itoe nafasi ya wao kujitetea vilevile.

“Tunaomba suala hili liangaliwe kwa makini sana, wakati ule mawakili wa serikali walibaini kuwa nyaraka nyingine ni za bandia, tunaomba lisichukuliwe kirahisi, tunaomba maelezo ya kina yatolewe ili lisiathiri mwenendo mzima wa kesi,” alidai Magafu. Jaji Massati alisema atatolea uamuzi suala hilo leo saa nne asubuhi ili kujua kama atatoa utetezi tena au la, na akamruhusu shahidi pekee wa Zombe kutoa ushahidi mahakamani hapo.

Shahidi huyo, Mkuu wa Gereza la Ukonga, Samwel Nyakitina (59) akitoa ushahidi wake uliolenga kuieleza mahakama anachofahamu kuhusu utaratibu wa wafungwa na mahabusu kutembelewa gerezani au uandikaji wa barua na washitakiwa kumiliki simu na fedha baada ya Zombe katika ushahidi wake wa awali kulalamikia baadhi ya washitakiwa wenzake walikamatwa na simu gerezani na barua na namna ambavyo aliandika barua za malalamiko kwa DPP na Waziri wa Mambo ya Ndani kupitia kwake, shahidi huyo alionyesha kuwa kinyume na matarajio ya Zombe. Sehemu ya mahojiano baina ya shahidi na Wakili Msemwa mbele ya mahakama hiyo yalikuwa kama ifuatavyo.

Wakili: Shahidi hebu ieleze mahakama utaratibu wa mfungwa au mahabusu kuandika barua na kuipeleka nje ya gereza ukoje.

Shahidi: Akishaandika barua inapita mapokezi kisha inakwenda ofisi ya Mkuu wa Gereza inagongwa mihuri na saini ndipo inaenda nje, bila hivyo inakuwa si halali na ni ngumu kutumika katika ofisi za serikali…..lakini sasa ni juu ya mwandikaji na mpokeaji huko nje.

Wakili: Unasema nini kuhusu barua ya Zombe ya Februari 14, 2007 kwenda kwa Jaji Mkuu Mfawidhi na ile ya kutoka kwa Zombe kwenda kwa Waziri wa Mambo ya Ndani akimlalamikia kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka amemtengenezea kesi ya mauaji?

Shahidi: (akiwa ameshika barua hizo) Saini ni kama yangu na mihuri ya Gereza la Ukonga, lakini sina ukakika nazo mpaka nikaangalie katika makabrasha yangu maana mmenishtukiza sikujiandaa.

Wakili: Unaiambia nini mahakama kuhusu vielelezo kama simu na fedha ulizowakuta nazo washitakiwa wakati kuwa na hivyo vitu gerezani ni kinyume cha sheria na taratibu za gereza.

Shahidi: (akatoa vielelezo ambavyo ni simu nne) siku ya tarehe 15/09/2006 siwezi kusema hapa mshitakiwa yupi alikamatwa na simu, labda mpaka nikaangalie katika majalada, lakini siku hiyo askari waliwapekua mahabusu 30 na waliotoka mahakamani na wafungwa zaidi ya 1,000 walioenda kazini kama utaratibu unavyoelekeza na walikutwa na simu nne na fedha taslimu Sh 153,000. Tukio hilo sina kumbukumbu zake zote hapa.

Awali katika ushahidi wake, mshitakiwa wa 13 ambaye ni wa mwisho katika kesi hiyo inayowakabili washitakiwa tisa hivi sasa, Festus Gwabisabi alidai kuwa alishiriki kuwapekua watuhumiwa waliouawa katika eneo la Sinza Palestina wakiwa hai siku ya tukio bila majibizano yoyote ya risasi na kwamba alishangaa kusikia kupitia vyombo vya habari siku mbili baadaye kuwa wameuawa.

Akiongozwa na wakili wake Longino Myovela, Gwabisabi alidai akiwa na Mkuu wa Upelelezi Kituo cha Urafiki, Ahmed Makelle, mshitakiwa wa tatu, alimpekua mtuhumiwa mmoja na kumkuta na bastola moja na mkoba mweusi waliodai una Sh milioni tano na kwa mara ya pili huo mkoba na bastola aliuona mezani kwa Zombe asubuhi ya Januari 15, 2006 walipoitwa kupongezwa kwa kazi nzuri ya kukamata majambazi.

Alidai pia kuwa Zombe aliwafundisha washitakiwa hao namna ya kujieleza pindi watakapoitwa kuhojiwa katika Tume ya Jaji Kipenka kuhusu tukio hilo kwamba waeleze kulikuwa na majibizano ya risasi katika Ukuta wa Posta, Sinza jambo ambalo yeye (shahidi) alilikataa kwani aliwakamata kwa amani bila majibizano na alishauri wapelekwe kituoni kuhojiwa, lakini hakujua walikopelekwa.

Zombe na wenzake wanatuhumiwa kuwaua Sabinus Chigumbi, Ephraim Chigumbi, Matius Lukombe na dereva taksi, Juma Ndugu katika msitu wa Pande, Mbezi Louis, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam Januari 14, 2006. Wakati kesi hiyo inaahirishwa Februari mwaka huu, Jaji Massati aliwaachia huru washitakiwa watatu ambao ni Noel Leonard, Moris Nyangelela na Felix Cedrick baada ya kuonekana kuwa hawana kesi ya kujibu kuhusu mauaji hayo.

SOURCE: Habari Leo


Kazi ipo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mmhh,hii kesi huwa siielewi kabisa,huwa najitahidi sana kufatilia lakini napata mashaka kama kuna mtu atahukumiwa naona kama viini macho.
 
Mmhh,hii kesi huwa siielewi kabisa,huwa najitahidi sana kufatilia lakini napata mashaka kama kuna mtu atahukumiwa naona kama viini macho.

Watahukumiwa tu, wewe vuta subira. Hukumu ina sehemu mbili, kushinda kesi, ama kushindwa. Hivyo hukumu itatoka, kama una maanisha hukumu kwako ni mpaka mtu aonekane ana makosa, hiyo ni nje ya sheria. Majaji watafuata sheria kuwatia hatiani ama kutowatia.
 
Kwa mujibu wa maelezo ya hakimu leo,kupitia radio-one stereo:

Washtakiwa wooooote wakiongozwa na Zombe mwenyewe wamekutwa na hatia,na watahukumiwa kwa mujibu wa sheria!

Hakimu ameongea mengi sana,akizungumza ukiukwaji wa maadili ya taaluma kwa maaskari hao.Pia ameelezea namna alivyopitia upande wa ushahidi dhidi yao na kutoa hitimisho WOTE WANA HATIA!na watahukumiwa

Kesi itaendelea tena kesho,baada ya baraza la wazee kukaa!


WAKUU,nadhani tupo kwenye episode ya mwisho mwisho,stay tuned!
 
pamoja na 'kumuondoa' koplo lema bado haijasaidia
 
pamoja na 'kumuondoa' koplo lema bado haijasaidia

yah! Zombe's folks walihakikisha Afande Lema anakufa kabla ya kutoa ushahidi wake pia wakawachinyia baharini akina Afande Saad Alawi ili ionekane wamekimbia na kutishwa msala mzima.
 
Back
Top Bottom