Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

Zombe yuko mahabusu akikabiliwa na tuhuma nzito,ya mauaji ya wafanyabiashara wanne wa madini.Hata hivyo kwa muonekano,anaoneka si mtu anayepata adha huko aliko,kwa vile sio siri,kapendeza kama mtu aliyeko nyumbani kwake.Hali hii inanipa wasiwasi mkubwa. Inaonekana wazi kabisa kwamba kuna 'unequal treatment of prisoners,' kwenye jela zetu,kwamba wale wenye uwezo kifedha na madaraka wanatendawa vizuri zaidi kuliko wenzangu na mimi.Hii sio sawa kwenye nchi inayo tamba kwamba inadumisha utawala bora.

Nililotaka kuongea hata hivyo ni hili la Zombe kudai kwamba polisi hawajui sheria, kwa hiyo wapelekwe vyuoni ili wajifunze sheria.Ninalojiuliza mimi ni kwamba, kwani yeye alikuwa wapi siku zote,si alikuwa huhumo kwenye jeshi la Polisi,tena kiongozi.Alishindwa nini kutoa wazo hilo wakati huo, ili hoja yake iweze kufikiriwa na hatimaye kutekelezwa?Ni kweli tunajua polisi ni wakiukaji wakubwa wa haki za binadamu,na hili halina ubishi,lakini wazo la polisi kufundishwa sheria linapotoka kwa mtu kama Zombe kuna maswali mengi ya kujiuliza.Hii ndio aina ya viongozi tulio nao Tanzania,wanaojali maslahi yao tu, bila kujali wengine.Zombe analalama kwa vile yale aliyokua anafanyia wenzake ndiyo anayo fanyiwa sasa.Alipo yafanya yeye aliona sawa.Mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu.
 
Kesi ya Zombe na wenzake (Majira)

Na Grace Michael

OFISI ya Mkemia Mkuu wa Serikali imethibitisha kuwa damu iliyokutwa mahali panapodaiwa kuuawa wafanyabiashara wa madini na sampuli yake kupelekwa katika ofisi hiyo, ilikuwa ni ya binadamu.

Bw. David Elias (47), mkemia wa ngazi ya daraja la pili katika ofisi hiyo ambaye ni shahidi wa 37 wa upande wa mashitaka, alidai katika mahakama kuu kuwa akiwa ofisini kwake Machi 9 2006 alipelekewa sampuli ya damu na Inspekta wa polisi Bw. Omary (shahidi wa 31) na kuipima.
Akiongozwa na Wakili wa Serikali Bw. Angaza Mwipopo, sehemu ya mahojiano na shahidi huyo ilikuwa kama ifuatavyo.

Wakili: Ulitakiwa ufanye nini?

Mkemia: Nilitakiwa nichunguze kama ni damu, kujua ni ya kitu gani, binadamu au mnyama pamoja na kujua kundi la damu hiyo.

Wakili: Je ulifanya kazi hiyo?

Mkemia: Ndiyo nilifanya na majibu yake yalionyesha kuwa damu hiyo ni ya binadamu lakini sikufanikiwa kujua kama ni kundi gani kwani chembechembe zilikuwa zimeshakufa.

Mahakama ilipokea ripoti ya Mkemia huyo ambayo itatumika kama kielelezo katika kesi hiyo.
Akihojiwa na wakili wa upande wa utetezi shahidi huyo alikana kupokea sampuli nyingine tofauti na hiyo aiyoifanyia kazi Machi 9 2006.

Mapema, shahidi wa 36 SACP Sydney Mkumbi (59) aliiambia mahakama kuwa washitakiwa wote isipokuwa Bw. Zombe waliandika maelezo ya nyongeza ambayo yanafanana na ya Bw. Lema ambaye alikiri kufika Pande na kushuhudia mauaji.

Pia alidai kilichopelekea mauaji hayo ni tamaa ya fedha waliyokuwa nayo wahusika.

Akihojiwa na upande wa utetezi ilikuwa kama hivi:

Swali: Mpaka hapa unaweza ukawa unajua nini hasa chanzo cha kuuawa marehemu?

Jibu: Najua, ni begi la fedha ambalo lilikuwa kwenye buti ya gari lao ambalo hata alipokamatwa mtuhumiwa mmoja alisikika akisema ni begi lake.

Swali: Je ulishawahi kumuuliza Bw. Bageni kuhusiana na hilo?

Jibu: Hapana kwani tangu mwanzo alikuwa amedanganya.

Swali: Je kuna ushahidi mwingine ukiachilia mbali maelezo ya Bw. Lema na Bw. Rajab Bakari unahusu kwenda kwao Pande?

Jibu: Ndiyo, washitakiwa wote waliandika maelezo ya nyongeza na maelezo yao yalifanana na ya Bw.Lema na Bw.Rajab.

Swali: Je ile karatasi ya maelezo ambayo yanadaiwa kuandikwa na Zombe na kupewa askari kukariri ulipewa?

Jibu: Hapana Bw. Lema alinionesha tu na kusema kuwa hawezi kumpa mtu yoyote na hata mke wake hawezi kumwachia.

Pia shahidi huyo alihojiwa na Jaji Salum Massati ambapo ilikuwa kama hivi:

Jaji: Ebu shahidi nisaidie kitu kiomoja kwa uzoefu wako hao askari waliokuwa katika ukuta wa posta na wale wa Pande wangewezaje kuzuia kosa kutendeka huku walikuwa wamepewa amri?

Jibu: Mheshimiwa Jaji kama walipewa amri isiyo halali walitakiwa kuripoti kwa Ofisa yoyote mara baada ya kutoka kwenye tukio hilo na wangeeleza ukweli.

Kesi itaendelea leo.

Washitakiwa katika kesi hiyo wanadaiwa kuwa Januari 14, mwaka juzi wakiwa katika msitu wa Pande Luisi ulioko Mbezi, Dar es Salaam walimuua kwa makusudi Bw. Ephraim Chigumbi, Bw. Sabinusi Chigumbi, Bw. Juma Ndugu na Bw. Mathias Lukombe.

Washitakiwa hao ni Bw. Zombe, Bw. Bageni, Bw. Makele, F5912 Noel, YP4513 Jane, D6440 Nyangerella, D1406 Mabula, E6712 Felix, D8289 Michael, D2300 Abeneth, B1321 Rashid, D4656 Rajab na D1367 Philipo.


Shahidi: Nina karatasi ya siri ya ACP Zombe (Tanzania Daima)

na Salehe Mohamed na Asha Bani

SHAHIDI wa 36 katika kesi ya mauaji inayomkabili aliyekuwa Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Abdallah Zombe na wenzake 12 wanaokabiliwa na kesi ya mauaji, Sydney Mkumbi, amedai mtuhumiwa wa 11 katika kesi hiyo, Rashid Lema ana kikaratasi chenye maelezo waliyopewa na Zombe wakaandike.

Mkumbi alidai alipomhoji mtuhumiwa huyo, alimuonyesha maelezo hayo, lakini mtuhumiwa huyo alisema hatamwamini mtu yeyote kumkabidhi karatasi hiyo hata mkewe, kwani anaamini maelezo hayo yataweza kumsaidia siku za usoni.

Alidai karatasi hiyo ina maandishi ambayo yameshachapwa na alipewa na Zombe ayasome, ili aende kuzungumza katika Tume ya Jaji Musa Kipenka iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kuchunguza mauaji hayo.

"Alinionyesha karatasi aliyodai kupewa na Zombe ambayo ilikuwa na maelezo ambayo aliwaambia wakayaseme katika Tume ya Jaji Kipenka, lakini pia alisema hataweza kumuamini na kumpa mtu yeyote hata mkewe, kwani anaamini yatakuja kumsaidia hapo baadaye," alidai Mkumbi.

Aidha, Jaji Kiongozi Salum Masati anayesikiliza kesi hiyo, alimhoji shahidi huyo kuwa wale askari wanaoshitakiwa kwa kosa la mauaji wangeweza vipi kuzuia mauaji yale baada ya kupata amri ya mkuu wao wa kazi.

Mkumbi alijibu askari wale walipaswa kutekeleza amri hiyo kama walivyofanya, lakini waliporejea walipaswa kuwasiliana na maofisa wengine na kueleza kila kitu kilichofanyika.

Alidai askari hao hawakufanya hivyo badala yake walidanganya, yote ikiashiria walikuwa wamepanga njama ya kutekeleza mauaji hayo.

Alidai ni kosa kwa askari wa chini kutotekeleza amri halali ya mkuu wake wa kazi na hata askari hao walipokuwa wanakwenda na watuhumiwa katika msitu wa Pande walikuwa sahihi, lakini utekelezaji wa amri hiyo haukuwa sahihi.

"Kazi ya askari ni kuzuia kosa lisitendeke, lakini pia kutekeleza amri ya wakuu wake wa kazi hivyo kama waliona wametekeleza amri isiyo halali baada ya kutoka msituni walipaswa watoe taarifa kwa maofisa wengine na si wale waliowatuma," alieleza Mkumbi.

Aidha, shahidi huyo alikana kuwapo kwa sampuli mbili za uchunguzi wa damu walizozipeleka katika ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa uchunguzi.

Alidai achokijua yeye kuwa ni kupeleka sampuli ya udongo uliochanganyika na damu kutoka katika msitu wa Pande na si Sinza kama shahidi wa 31, Nickobay Mwakajinga, alivyodai mahakamani hapo alipokuwa akitoa ushahidi wake.

Alidai kama Nickobay alifanya hivyo, basi ni katika kipindi kingine, lakini si katika uchunguzi wa timu yake.

Baada ya kufunga ushahidi wake, wakili wa utetezi, Majura Magafu alitaka kujua kama alishawahi kusikia kuwa askari hao walichukua fedha za wafanyabiashara waliouawa kwa madai ya ujambazi.

Shahidi huyo alidai aliwahi kuyasikia, lakini hakuwahi kuyafanyia upelelezi kwa kuwa ni kosa la wizi na yeye kwa wakati huo alikuwa anashughulikia suala la mauaji.

Sehemu ya mahojiano kati ya shahidi huyo na Wakili Magafu yalikuwa kama ifuatavyo:

Myovela: Mbali na ushahidi wa Rashid na Rajabu kuna ushahidi mwingine mlioupata?

Shahidi: Ndiyo, nimesikia watuhumiwa wakiwa gerezani waliandika maelezo mengine ambayo hayakuwa tofauti na yale waliyoyatoa mtuhumiwa wa 11 na wa 12.

Myovela: Hivi shahidi unafikiri kwamba endapo Rajabu na Lema wasingeandika maelezo hayo mngeweza kuwakamata watuhumiwa na kuwafikisha mahakamani?

Shahidi: Uchunguzi nilioufanya ungeniongoza kufikia hatua hiyo ya watuhumiwa kupelekwa mahakamani.

Myovela: Ni kosa kwa askari wa chini kukataa kutii amri ya mkuu wake?

Shahidi: Ndiyo ni kosa.

Aidha, shahidi wa 37 katika kesi hiyo, Mkemia Mkuu daraja la pili katika ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, David Elias, alidai ofisi yake ilipokea ombi moja la uchunguzi wa sampuli nne za damu zilizoletwa na Ofisi ya Upelelezi wa Kituo cha Polisi Osterybay.

Alidai alitakiwa kuchunguza kuwa sampuli hizo nne kuwa ni za damu ya binadamu, mnyama na kundi la damu na wala hakupokea ombi jingine kutoka Makao Makuu ya Polisi.

Alidai alishindwa kutambua kundi la damu hizo kutokana na chembe chembe zilizokuwa zimeharibika, hivyo hakukuwa na uwezakano wa kujua ni damu ya kundi gani.

Baada ya mkemia huyo kumalizia kutoa ushahidi wake, Wakili Magafu alimuuliza shahidi huyo kuwa ni kemikali gani wanayotumia katika kutambua sampuli hizo.

Shahidi huyo alidai alitumia kemikali inayoitwa Anti Sera na pia kuna kemikali za kutambua kama damu ni ya mnyama au binadamu.

Sehemu ya mahojiano kati ya Wakili Magafu na shahidi huyo yalikuwa kama ifuatavyo:

Magafu: Damu ikikaa kwa wiki nane au wiki tatu inaweza kutambulika?

Shahidi: Inategemea na hali ya eneo la tukio, lakini damu inaharibika kutokana na mvua, jua, umande na kupitapita kwa watu.

Magafu: Je, nikikuambia kuwa damu iliyoletwa ilikuwa ni moja, lakini katika makundi tofauti utasemaje?

Shahidi: Hilo mimi sijui, inawezekana lakini kazi yangu haikuwa hiyo bali ni kufanya uchunguzi kulingana na ombi la Polisi.

Mbali na Zombe, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Christopher Bageni, Noel Leornad, Jane Andrew, Moris Nyangelela, Emanuel Mabula, Felix Cedrix, Koplo Michael Abeneth, Koplo Rajabu, PC Rashid Lema na Festus Bwabisabi.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya maujai hayo Januari 14 mwaka 2006, ambapo waliwaua wafanyabiashara watatu wa madini, ambao ni Ephraim Chigumbi, Sabinius Chigumbi na Mathias Lunkombe na dereva teksi, Juma Ndugu. Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo.
 
Mtanzania said:
Aidha, Jaji Kiongozi Salum Masati anayesikiliza kesi hiyo, alimhoji shahidi huyo kuwa wale askari wanaoshitakiwa kwa kosa la mauaji wangeweza vipi kuzuia mauaji yale baada ya kupata amri ya mkuu wao wa kazi.

Mkumbi alijibu askari wale walipaswa kutekeleza amri hiyo kama walivyofanya, lakini waliporejea walipaswa kuwasiliana na maofisa wengine na kueleza kila kitu kilichofanyika.

Alidai askari hao hawakufanya hivyo badala yake walidanganya, yote ikiashiria walikuwa wamepanga njama ya kutekeleza mauaji hayo.

Alidai ni kosa kwa askari wa chini kutotekeleza amri halali ya mkuu wake wa kazi na hata askari hao walipokuwa wanakwenda na watuhumiwa katika msitu wa Pande walikuwa sahihi, lakini utekelezaji wa amri hiyo haukuwa sahihi.

Hivi hii hapo juu ni kweli? Kusema ua raia asiye na hatia sio amri halali. Je askari akikataa
atakuwa amefanya kosa? Kama ni hivyo hapo kuna mapungufu makubwa sana kwenye hiyo sheria.
 
nafikiri tunahitaji jukwaa jingine kwa ajiri ya maswala ya ''LEGAL BRIEFING'' kwwaiyo mtu anayehusika na kutengeneza majukwaa afanye jukwaa la maswala ya sheria
 
Dada yangu Naima, hakuna binadamu (mwenye mwili na damu na Nyama / "aliye zaliwa na mwanamke") ambaye hastahili kuonewa huruma.

Hakuna binadamu asiyefanya kosa.

Hakuna binadamu asiyejutia kosa alilofanya hata kimoyomoyo

Lakini mshahara wa Dhambi ni Mauti.

Kama mshahara wa dhambi ni mauti...Then kwanini kila mtu anakufa?
Je kila mtu ana dhambi?
 
Naona kama wanamrahisishia Zombe utetezi. Hao polisi ama wachunguzi kwa nini hawakuomba mkemia mkuu athibitishe kama damu hiyo waliyotoa eneo la tukio ni ya waliouawa ama la? Maana kusema tu damu hiyo ni ya binadamu haitoshi, mtu anaweza kujichanja na kudondosha damu pale! Kama sampuli hizo zimetunzwa, wakafukue maiti zile wafanye ulinganisho kwa DNA, vinginevyo hapa wanamrahisishia tu Zombe utetezi.
 
Waungwana nimeiona hii habari IPPMEDIA, lakini nimeshindwa kuifungua. Kama kuna atakayeweza kuifungua aiweke hapa.

Zombe kuanika dili za vigogo
Posted Sat, September,27 2008
Source Alasiri
Kama kweli aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe, ataamua kutimiza azma yake ya kuanika uozo wa selo, kama alivyotangaza jana, baadhi ya wananchi wanasema, vigogo kibao wataumbuka na dili zao haramu kuanikwa!
» Habari Zaidi
 
Please be specific uozo wa selo au uozo wa mapolisi wenzake ?
 
Waungwana nimeiona hii habari IPPMEDIA, lakini nimeshindwa kuifungua. Kama kuna atakayeweza kuifungua aiweke hapa.

Zombe kuanika dili za vigogo
Posted Sat, September,27 2008
Source Alasiri
Kama kweli aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe, ataamua kutimiza azma yake ya kuanika uozo wa selo, kama alivyotangaza jana, baadhi ya wananchi wanasema, vigogo kibao wataumbuka na dili zao haramu kuanikwa!
» Habari Zaidi

Kwa mtizamo wangu na jinsi Zombe anavyotoa kauli mbalimbali

Chache kuzitaja:

- mara ataandika kitabu kuhusu jera akiwa nje,

- mara magazeti yanafanya vizuri sasa hivi, wakati mwanzo wa kesi alikuwa anayakandia na hakutaka hata kuongea nayo;

- mara mapolisi hawajui sheria wakati enzi zake alikuwa halioni hilo,

... na mengine mengi

I conclude by saying that this guy is:

MFA MAJI AMBAYE HAISHI KUTAPATAPA.

Alikuwa wapi siku zote? Angoje sheria ichukue mkondo wake; Mshahara wa dhambi ni mauti;

Njimba
 
Kwa mtizamo wangu na jinsi Zombe anavyotoa kauli mbalimbali

Chache kuzitaja:

- mara ataandika kitabu kuhusu jera akiwa nje,

- mara magazeti yanafanya vizuri sasa hivi, wakati mwanzo wa kesi alikuwa anayakandia na hakutaka hata kuongea nayo;

- mara mapolisi hawajui sheria wakati enzi zake alikuwa halioni hilo,

... na mengine mengi

I conclude by saying that this guy is:

MFA MAJI AMBAYE HAISHI KUTAPATAPA.

Alikuwa wapi siku zote? Angoje sheria ichukue mkondo wake; Mshahara wa dhambi ni mauti;

Njimba


Mkuu njimba sio kweli kuwa "mshahara wa dhambi ni mauti" ninavyojua mie kuwa kila nafsi itaonja mauti. Kwa maana hiyo nafsi zote zitakuwa zinapata mshahara wa dhambi! Siamini kwa hili mkuu. Sijui pengine huelewi unachokisema/andika maana mpo wengi wa aina yenu humu JF. Pengine kwa kukusahihisha ungesema malipo ya dhambi ni moto wa jahanam na sio "mshahara" japo itaona malipo na mshahara ina maana sawa lakini kiswahili ni kama kingereza mfano affection,desire na love zina maana moja ila kila neno hapo linasehemu yake ya kulitumia. Mfano malipo ya mja mwema mbinguni ni pepo na malipo ya mfanyakazi ni mshahara.

Nadhani utakua umenielewa na next time ya wakati ujao utakuwa makini kupost maneno yenye kuleta maana na sio ya kupotezea watu muda.
 
Njimba,

Kwani huyo Zombe kunamtu alimwambia kuwa atachomoka kwenye hiyo kesi mpaka anazungumzia kuandika kitabu na kutoa uozo wa vigogo akitoka? Mi nadhani yeye atakuwa ana machafu mengi katokana na wadhifa aliokuwa akishikilia....Bedui kabisa huyo!!!
 
Kwa mtizamo wangu na jinsi Zombe anavyotoa kauli mbalimbali

Chache kuzitaja:

- mara ataandika kitabu kuhusu jera akiwa nje,

- mara magazeti yanafanya vizuri sasa hivi, wakati mwanzo wa kesi alikuwa anayakandia na hakutaka hata kuongea nayo;

- mara mapolisi hawajui sheria wakati enzi zake alikuwa halioni hilo,

... na mengine mengi

I conclude by saying that this guy is:

MFA MAJI AMBAYE HAISHI KUTAPATAPA.

Alikuwa wapi siku zote? Angoje sheria ichukue mkondo wake; Mshahara wa dhambi ni mauti;

Njimba


Zombe bwana .Yaani ana echo yale yale viongozi wa Nchi hii kuwa nje ya madaraka ndipo waone matatizo ya Nchi .

Mnakimbuka Sumaye naye alisema hakujua kwamba Tanzania was poor hadi alipokuwa Harvard ?Na Zombe ayasemayo hakuyajua hadi alipotoka Mbinguni na kuja Duniani .
 
Hizi ni hadithi tu alitakiwa huko nyuma alipokua kiongozi angeongelea haya sio mpaka kabanwa na mlango ndio analeta tamthilia,angoje hukumu yake damu za watu hazipotei bure na hata kama hatalipa duniani atalipa kwa MUNGU.Tunaweza kumsikiliza kidogo kama atatuambia walivokua wanavuta % yao na Mahita kutoka kwa majambazi na wauza unga na kutaja majina yao.
 
Huyu anawatisha wenzake inawezekana wamemtupa mara baada ya kuswekwa ndani.
Ana watingishia kiberiti ili wafanye something kumtoa lupango...Inaonekana anataka alete karata ya Plea Bargain...
Zombe hakufanya kazi yake kwa maadili na alikuwa mnyama sana asiyekuwa na huruma...Sifa zake si za afande mwema...Bali za kijambazi kabisa na kigaidi....Huyu yeye alikuwa akiterrorize na hakuwahi kufikiri kuwa kuna mwisho...Extremelly overconfident and naive....Sijui ni sifa gani zilizomfanya apewe vyeo vyote hivyo...Nadhani ni kazi ya Mkapa hii.....Wote hao alihakikisha ni watu wa aina hiyo wa kumdhibiti Mrema ambaye kama si Mwalimu basi nji alikuwa anachukuwa.
Tatizo ni kuwa baada ya umaarufu wa Mrema kushuka sasa wakawa hawana cha kufanya na yale marupu rupu waliyokuwa wakipewa kwa kumtandika mabomu ya machozi Mzee wa Kiraracha....Ikabidi na wao wawe majambazi kwa kujidai wanapambana na ujambazi.
 
Ndiyo maana yake

Sasa mbona kuna wanaodai hawana dhambi?
Ama ina maana hao hawafi?
Ndio maana mafisadi wanakimbilia misikitini na makanisani ili kuendelea kuwapumbaza wadanganyika kuwa sasa wamesamehewa dhambi na no more mentioning EPA,KIWIRA,RICHMOND NK...Just kama alivyofanya mkoloni.
 

Nadhani utakua umenielewa na next time ya wakati ujao utakuwa makini kupost maneno yenye kuleta maana na sio ya kupotezea watu muda.

Sokomomoko you have gone too far!

Wewe ni nani mpaka utoe kauli kama hii hapa?

Je umeelewa nilichotaka kusema lakini? Au wewe umeona la mshahara wa dhambi ni mauti tu? Soma vizuri hili neno ni kibwagizo tu. Nilichotaka kusema sio hicho. Soma na maoni ya watu wengine pia.


Haya na wewe unapoandika "utakua umenielewa na next time ya wakati ujao" Una maana gani sasa hapa?


Sikiliza ndugu yangu hapa hatuangalii makosa madogo madogo ya lugha kikubwa ni nini mtu anataka kuieleza jamii. Nilitaka kukuonyesha jinsi gani hata wewe mwenyewe usivyo makini. Ila siko tayari kubishana na wewe.

Ahsante kwa ushauri wako wa matumizi ya neno mauti.

Njimba
 
Hata mimi naona atashinda sababu yeye wala hakuwepo eneo la tukio zaidi ya kutoa amri "isiyo halali" kwenye simu..!!

Kushinda kwa Zombe katika kesi hii kuko chini ya maelezo atakayotoa Christopher Bageni kwani Bageni kwa "kutii amri" ya Boss wake ndiye aliyemtuma afande wa chini yake Saad Alawi awaue wale raia wema. (Mungu awalaze mahala pema peponi, Amen)

Kwa utii huu kama Bageni atasema kama atakiri kuua na kutamka alikuwa anatekeleza "amri halali ya Boss wake" Bageni atakuwa shahidi mwingine mpya wa kuelezea yaliyojiri hadi akatoa amri hii mbaya ya kukatisha maisha ya Binadamu kikatili kiasi hicho. Kwa hakika hawa watu utadhani hawakuumbwa kwani kama ni kutii amri toka kwa binadamu mwenzako tena ukijua amri hii si halali nyote wawili ni wakosaji. Sidhani kabisa kama kitendo hicho kingetekelezwa kama mmoja wa wale wafanya biashara angekuwa ni mmoja wa ndugu wa maaskari hao walioenda msitu wa Pande. Hakika hawangekufa kinyama hivyo.
Pili kama hawangekuwa na fedha pia hawangeuawa kilicho waponza ni fedha walizokuwa nazo. Tuzidi kusubiri ngwe ya pili ya upande wa utetezi itatoka na nini.
 
Hivi hii kesi imeishia wapi????? Hukumu yake imeshatolewa??????

Maendeleo soma hapa kutoka gazeti la mwananchi

Kesi ya Zombe sasa ni hadi Februari mwakani
Na Nora Damian

KESI ya mauaji ya wafanyabiashara watatu wa Mahenge na dereva teksi, inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam ACP, Abdallah Zombe na wenzake 12 inatarajia kuendelea kusikilizwa mwezi Februari mwakani.


Akizungumza na gazeti hili jana, Msajili wa Mahakama Kanda ya Dar es Salaam, Saul Kinemela alisema kesi hiyo itaendelea kusikilizwa baada ya uzinduzi wa mwaka mpya wa mahakama.


Septemba 26 mwaka huu kesi hiyo iliahirishwa na Jaji Kiongozi Salum Massati baada ya upande wa mashitaka kufunga ushahidi ambapo jumla ua mashahidi 37 walitoa ushahidi.


Hata hivyo upande wa utetezi uliwasilisha ombi mahakamani hapo ukitaka shahidi wa 22 Mrakibu wa Polisi (SP) Juma Bwire ambaye ni mtaalamu wa uhunguzi wa silaha makao makuu ya Jeshi la Polisi aitwe tena kutoa ushahidi.


Upande wa utetezi unataka shahidi huyo aitwe tena ili atatue utata uliojitokeza kuhusu sampuli zilizopelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kama zilitokea katika tukio la Sinza au msitu wa Pande.


Washitakiwa hao walifikishwa mahakamani mwaka 2006 baada ya wananchi kulalamika kuwa waliouawa hawakuwa majambazi.


Wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge na dereva teksi mmoja wa Manzese ambao wanaodaiwa kuwa majambazi waliuawa Januari 14 mwaka 2006 kwa maelezo kuwa ni majambazi.


Baada ya malalamiko kuzidi Jeshi la polisi liliunda tume kuchunguza sakata hilo lakini kabla halijamaliza uchunguzi wake, Rais Jakaya Kikwete aliunda tume ambayo iliongozwa na Jaji Kipenka.


Uchunguzi wa tume hiyo ndio iliosababisha kufunguliwa kwa kesi hiyo ambayo mbali na Zombe, washtakiwa wengine ni Rashidi Lema na Rajabu Bakari.


Wengine ni SP Christopher Bageni, ASP Ahmed Makelle, F.5912 PC Noel Leonard, WP 4593 PC Jane Andrew, D6440CPL Emmanuel Mabula, E6712 CPL Felix Cedrick, D8289 PC Michael Sonza, D 2300CPL Ebeneth Saro na D.1367 D/CPL Festus Gwabisabi.
 
Back
Top Bottom