Kesi ya Afande sakata la binti wa Yombo yafutwa, hatokabiliwa na shtaka lolote dhidi yake

Kesi ya Afande sakata la binti wa Yombo yafutwa, hatokabiliwa na shtaka lolote dhidi yake

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma imekataa ombi la kusaini malalamiko yaliyotolewa na Paul Kisabo dhidi ya Fatma Kigondo maarufu kama Afande, baada ya kubaini kuwa malalamiko hayo yana dosari mbalimbali ikiwemo kutofuata taratibu za kisheria.

Uamuzi huu wa Mahakama uliotolewa siku ya Ijumaa Oktoba 18, 2024 unamaanisha kuwa Fatma Kigondo hatokabiliwa na shitaka lolote dhidi yake.

Pia soma: Mahakama yatupilia mbali ombi la Afande Fatma kusomewa mashtaka popote alipo

Screenshot_20241018_185450_X.jpg

Paul Kisabo alikuwa amefungua malalamiko akimlalamikia Fatma Kigondo kwa kosa la kubaka kwa kundi, na Oktoba 15, 2024, Wakili wake Peter Madeleka aliiomba mahakama kusaini malalamiko hayo ili yawe hati ya mashtaka rasmi na mshitakiwa asomewe makosa popote atakapokuwa.

Hata hivyo, uamuzi uliotolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma, Nyambuli Tungaraja, umesema kuwa kutokana na dosari mbalimbali zilizojitokeza kwenye malalamiko hayo, hayakidhi vigezo vya kusainiwa kuwa hati ya mashtaka.

Jambo TV
 
Nimeishia hapo kwamba kubaini kua kuna dosari👈
Ngoja ninywe kahawa kidogo kisha nintakuja kumalizia hadi mwisho.
 
ilikua kesi rahisi mno. kwake kushinda manake hata angesimama kizimbanj angesema vijana niliowatuma hawakuwa wale ni wengine
niliwatuma vijana sita warefu waliojazia na sio wale

hakimu anafuta kesi
Wakati wa cross examination angeambiwa awataje hao vijana sita warefu
 
ilikua kesi rahisi mno. kwake kushinda manake hata angesimama kizimbanj angesema vijana niliowatuma hawakuwa wale ni wengine
niliwatuma vijana sita warefu waliojazia na sio wale

hakimu anafuta kesi
Hapo angetiwa hatiani kwa kula njama ya kufanya uhalifu, ushahidi ni kauli yake hiyo

超级截屏_20241018_192730.png
 
Hii imetokea Leo tarehe 18/10/2024
 

Attachments

  • Screenshot_20241018-192605.png
    Screenshot_20241018-192605.png
    175.9 KB · Views: 7
  • Screenshot_20241018-192657.png
    Screenshot_20241018-192657.png
    480.5 KB · Views: 6
Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma imekataa ombi la kusaini malalamiko yaliyotolewa na Paul Kisabo dhidi ya Fatma Kigondo maarufu kama Afande, baada ya kubaini kuwa malalamiko hayo yana dosari mbalimbali ikiwemo kutofuata taratibu za kisheria.

Uamuzi huu wa Mahakama uliotolewa siku ya Ijumaa Oktoba 18, 2024 unamaanisha kuwa Fatma Kigondo hatokabiliwa na shitaka lolote dhidi yake.

Pia soma: Mahakama yatupilia mbali ombi la Afande Fatma kusomewa mashtaka popote alipo


Paul Kisabo alikuwa amefungua malalamiko akimlalamikia Fatma Kigondo kwa kosa la kubaka kwa kundi, na Oktoba 15, 2024, Wakili wake Peter Madeleka aliiomba mahakama kusaini malalamiko hayo ili yawe hati ya mashtaka rasmi na mshitakiwa asomewe makosa popote atakapokuwa.

Hata hivyo, uamuzi uliotolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma, Nyambuli Tungaraja, umesema kuwa kutokana na dosari mbalimbali zilizojitokeza kwenye malalamiko hayo, hayakidhi vigezo vya kusainiwa kuwa hati ya mashtaka.

Jambo TV
Wataandaa nyingine inayokidhi vigezo.

Ngoma bado mbichi. Tabu Iko pale pale.
 
Back
Top Bottom