Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
Kama ulidhani jambo hili ni utani, basi ulijidanganya, mambo tayari yako Mahakamani.
Kesi hii yaweza kuwa fundisho kwa mitandao mingine ya simu inayoshirikiana na Watekaji na Wauaji, hata kama watekaji hao ni Watu wa Serikali
Taarifa kamili hii hapa
---
Mchakato wa usikilizwaji wa kesi inavyohusiana na kukamatwa kwa mwanahabari Erick Kabendera, aliyoifungua mwanahabari huyo dhidi ya kampuni ya huduma za Mawasiliano Kwa simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Ltd unaanza leo.
Katika kesi hiyo Kabendera anaoimba mahakama hiyo iiamuru kampuni hiyo imlipe fidia ya Dola za Marekani 10 milioni (sawa na Sh28 bilioni) akiituhumu kuwa ndio iliyofanikishwa kukamatwa kwake na askari Polisi, tukio analoliita kutekwa, na kisha kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi, mwaka 2019.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa na Jaji Mfawidhi Salma Maghimbi na pande zote zimeitwa kufika mahakamani hapo leo Julai 9, 2024.
Kwa mujibu wa hati ya wito wa mahakama kwa wadaawa (pande zote) kufika mahakamani, kesi hiyo namba 12799/2024 imepangwa kutajwa asubuhi hii, huku ikiitaka kampuni hiyo kufika bila kukosa na kuwasilisha nyaraka zake ambazo inatarajia kuzitumia katika utetezi wake.
PIA SOMA
- Mwandishi Eric Kabendera aelezea jinsi Vodacom Tanzania ilivyomkamatisha kwa vyombo vya Usalama
- Madai ya fidia ya dola milioni Moja ya Erick Kabendera dhidi ya Vodacom yakienda mahakamani tutarajie nini?
- Erick Kabendera aitaka Vodacom imlipe Dola Milioni 1 kwa kufanikisha kutekwa kwake 2019
Kesi hii yaweza kuwa fundisho kwa mitandao mingine ya simu inayoshirikiana na Watekaji na Wauaji, hata kama watekaji hao ni Watu wa Serikali
Taarifa kamili hii hapa
Mchakato wa usikilizwaji wa kesi inavyohusiana na kukamatwa kwa mwanahabari Erick Kabendera, aliyoifungua mwanahabari huyo dhidi ya kampuni ya huduma za Mawasiliano Kwa simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Ltd unaanza leo.
Katika kesi hiyo Kabendera anaoimba mahakama hiyo iiamuru kampuni hiyo imlipe fidia ya Dola za Marekani 10 milioni (sawa na Sh28 bilioni) akiituhumu kuwa ndio iliyofanikishwa kukamatwa kwake na askari Polisi, tukio analoliita kutekwa, na kisha kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi, mwaka 2019.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa na Jaji Mfawidhi Salma Maghimbi na pande zote zimeitwa kufika mahakamani hapo leo Julai 9, 2024.
Kwa mujibu wa hati ya wito wa mahakama kwa wadaawa (pande zote) kufika mahakamani, kesi hiyo namba 12799/2024 imepangwa kutajwa asubuhi hii, huku ikiitaka kampuni hiyo kufika bila kukosa na kuwasilisha nyaraka zake ambazo inatarajia kuzitumia katika utetezi wake.
PIA SOMA
- Mwandishi Eric Kabendera aelezea jinsi Vodacom Tanzania ilivyomkamatisha kwa vyombo vya Usalama
- Madai ya fidia ya dola milioni Moja ya Erick Kabendera dhidi ya Vodacom yakienda mahakamani tutarajie nini?
- Erick Kabendera aitaka Vodacom imlipe Dola Milioni 1 kwa kufanikisha kutekwa kwake 2019