Kesi ya Liyumba, Utata na Maendeleo yake

Status
Not open for further replies.

Nadhani hapo kwenye highlights panaweza kutusaidia zaidi kuona kwamba ikulu itachukuwa hatua gani kumtafuta Liyumba, Wakati Masha ana offer msaada kwa mkuu wa nchi(technically) Liyumba yeye ana ambaa ambaa.
 
Mimi naona kama yale ya Balali yanakuja, serikali ilisema ikimwitaji itampata lakini kwa wakati huo haikuwa inamwitaji. Serikali ilipomwitaji ikawa ndio hivyo tena. Sasa hapa huyu mjinga aliyepewa dhamana ya uwaziri nyeti anasema hawajaambiwa wamkamate, yaani hata leo hii polisi wakimwona sanasana aliyeona atahangaika kupiga simu PCCB ili waje wamkamate apate hilo donge nono kama vile la kutoa taarifa za waua maalbino. Hivi viongozi wa nchi hii wataacha lini upumbavu wa kiwango hiki? Ni kwanini wanatuona sisi hatuna akili kiasi hicho? PCCB na Masha kuna umbali gani hadi wasubiri barua ndio wamtafute? liyumba ni mkubwa kiasi gani hadi serikali ijadili kumtafuta? Je polisi wakishapewa barua liyumba atakuwa kwa hawara yake akiwasubiri wamkamate kama kweli ana nia ya kutoroka? Kwanini mahakama ilivunja sheria kumwachia kwa dhamana ya kuku na mbuzi isiyofikia kiwango? Kwanini Mahakama ilikubali kupokea passport iliyokwisha muda wake? Ni ngumu sana kulielewa swala hili, halina tofauti sana na suala la Kagoda na mengineyo. LIYUMBA ASIPOONEKANA HAJATOROKA, AMETOROSHWA NA SERIKALI KUTUPOTOSHA UKWELI..!
 
Naomba mnisaidie kwani a'm totally confused with this argument . Kwa hiyo mimi nimpeleka mtu mahakamni akitoroka , mimi ndio natakiwa kumtafuta ? Kwani mahakama hiko chini ya TAKURU ?
 
...kuna jambo linafumbiwa macho hapa;

PCCB ya HOSEA imeingiaje hapa? na kama kuna Rushwa imehusishwa, nani mhusika/mpokeaji katika mahakama aliyewekwa ndani?

...tuwe makini na haya mazingaombwe, ndio haya haya tulosikia 'makachero' wa serikali walikuwa wanamfuatilia Daudi Balali...

Watanzania tumekuwa kama tumo kwenye ngoma ya mdundiko, ikipita basi alokuwemo na asokuwemo wooote wanaunga tela, hawajui mwanzo wake wala mwisho wake...

Kuna mtu keshajiuliza kitu kinachoitwa intimidation of witnesses?. Mwenye macho haambiwi tazama, kesi ya Balali ilikufa baada ya 'kifo' chake!

...msipoangalia, kesi ya Liyumba nayo itakufa baada ya kifo chake...
na baada ya hapo hakutakuwa na ushahidi tosha wa kesi za EPA, Richmond etc etc zinazohusiana na Benki kuu...nyie mmeshikilia kumkimbiza Liyumba huyoooo, liyumba... kalaghabaho! protection of 'key witnesses' ipo wapi jamani?

duuuuh! ama kweli "wajinga ndio waliwao!"
 
Last edited:
Wajameni huu mjadala wa Liyumba bado ni mrefu lakini hatimayake ni siku ya Jumanne. Aliachiwa kwa dhamana halali na mahakama, hata kama ni kwenye mazingira ya kutia shaka, lakini ile dhamana yake ni genuine.
Masharti ya dhamana hiyo yanamtaka awepo mahakamani hapo Jumanne ya terehe 24.
Hakuna kifungu kinachomlazimu awepo mahali popote ama lazima alale nyumbani kwake. Hivyo pia mimi najiunga na wanao amini Liyumba yupo mahali fulani akijipumzikia kwa raha zake huku akila lile tunda analolipendelea kufidia zile siku alizolikosa.

Endapo ni kweli atakuwa ametoroka, basi kesi yake itafutwa rasmi hiyo siku ya Jumanne na Kweka ataachiwa huru, japo Kweka atakamatwa tena baada ya muda mfupi na kufunguliwa mashtaka mapya.

Mambo yote ni mpaka Jumanne.
 
Naomba mnisaidie kwani a'm totally confused with this argument . Kwa hiyo mimi nimpeleka mtu mahakamni akitoroka , mimi ndio natakiwa kumtafuta ? Kwani mahakama hiko chini ya TAKURU ?

Mahakama kazi yakeni kupokea kesi toka kwa mawakili wa serikali na kisikiliza hoja za waliopeleka kesi na mawakili wa mtuhumiwa. Kwa sasa kesi nyingi hupelekwa mahakamani aidha na Polisi au Takukuru baada ya kupata idhini ya DPP. Kukitokea issue ya mtu kukamatwa etc, mahakama hutoa hati ya kukamatwa kwa taasisi inayosimamia kesi hiyo. Kama ni Polisi oda itaenda Polisi. Kama ni Takukuru oda itaenda Takukuru. Ndio maana hapa Takukuru inahangaika kwani kesi hii ni wao ndio wameipeleka mahakamani.
 


Mahakama "inasimamia" Sheria...Polisi wanajukumu la kuhakikisha "utekelezaji" wa sheria hizo kwa mujibu wa Katiba.

Sio Jukumu la TAKUKURU "kusimamia" kama sheria inatekelezwa...wao ni jukumu lao ni "kuchunguza" iwapo sheria imevunjwa katika misingi ya rushwa, matumizi mabaya ya madaraka n.k. Hivyo wakiona sheria imevunjwa wanapeleka kesi yao "mahakamani", kama ilivyo hii ya Liyumba.

Mtuhumiwa akishafikishwa "mahakamani" jukumu la TAKUKURU kumlinda linakwamia hapo, Mahakama inatumia vyombo vyake ambavyo ni Polisi na Magereza kuhakikisha sheria na haki inasimamiwa.

Mtuhumiwa akitoroka (baada ya kufikishwa mahakamani) anakuwa ametoroka akiwa chini ya Ulinzi wa Polisi, na sio TAKUKURU. Hakimu aliposema akamatwe arudishwe rumande, alikuwa ametoa amri hiyo Polisi na sio TAKUKURU.

Polisi na Magereza vyote vipo chini ya Wizara ya Masha...anaposema anasubiri kuombwa na TAKUKURU ndio wafanye kazi yao...nashindwa kuelewa.

Iwapo Katiba imebadilishwa, naombeni kuelimishwa.
 
Mahakama kazi yakeni kupokea kesi toka kwa mawakili wa serikali na kisikiliza hoja za waliopeleka kesi na mawakili wa mtuhumiwa. Kwa sasa kesi nyingi hupelekwa mahakamani aidha na Polisi au Takukuru baada ya kupata idhini ya DPP. .

Swali la kujiuliza kwa nini wanahitaji idhini ya DPP ? Je hauoni ya kuwa kwa kufanya hivyo polisi wanakuwa involved pia ?

This is preposterous, how can these two organs function under different set of rules? That is why corruption is inevitable in our country, and we kept on fostering it by creating loop holes and red tapes. It is a shame that the Hon. Minister of Home affairs, who was supposed to enforce our laws, is not only a Kihiyo when it come to those laws but also utterly clueless. No wonder he can’t protect innocent albino who are being butchered everyday under his watch! Let the truth be told …. This guy ought to be fired! Tanzania can’t afford on job training, we need a person who is going to be ready on day one…
 

Hapo ndio mujue tuna WAZIRI KIJANA anayekwenda na WAKATI
 

Oooh my God! I couldn't put it better than that. Big up YY.
 
Yebo Yebo,
Mkuu hapa umezungumza!..tupo pamoja kabisa, ndio maana tunasema mambo mengine yanapatikana - Only in Tanzania...
Haiwezekani kabisa mshtakiwa anapotoroka liwe jukumu la mshtaka kumtafuta.. Huu ujinga gani, bahati PCCB ni chombo cha serikali, sasa kama ingekuwa ni kesi ya watu binafsi ina maana leo hii mimi Mkandara kama mshtaka napewa sheria mkononi kumtafuta mbaya wangu aliyekimbia kutohudhuria mahakama siku ya kesi yetu!..
Ama kweli nchi inaongozwa kiholela!
 


Mkuu
Unashauri nini ama nini kifanyike?
 
Kuna taarifa kwamba Amatus Liyumba, ambaye sasa anatajwa kwamba ametoroka na hajulikani hayumo, HAJATOROKA na kwamba alikuwa amejipumzikia akiangalia afya yake huku akijipanga kutimiza masharti ya dhamana ambayo yanaelezwa kwamba mawakili wake walifanya 'madudu' kwa kushirikiana na Hakimu Khadija Msongo.

Kwa taarifa hizo ambazo hadi sasa ni TETESI, Liyumba sasa anaweza kuibuka tena mahakamani kati ya kesho Jumatatu na Kesho kutwa Jumanne, kuwasilisha hati za ziada za dhamana zenye thamani sawa ama zaidi ya sh bilioni 54.

Kama hiyo ni kweli basi wiki ijayo tutakuwa na mjadala tofauti na tunaoendelea nao sasa.

Mods, mutaangalia kama haistahili mutaiunganisha kule!!!!!!!
 


Asante kwa tetesi.

There is a tendency of being startled as wildebeest herds.
 
Kweli mapenzi hayana siri na siri si ya wawili ------- sasa na hilo donge nono lililotolewa na pccb itakuwaje ?? Au ndio imeshakuwa dili hilo ??
 

Akitimiza masharti ya hiyo dhamana mimi nita kana uraia wangu!!!!!!!
 
Nishauri nini zaidi ya Masha na Hakimu kuondolewa ktk viti vyao na mara moja kuwekwa rumande bila dhamana hadi watakapo tueleza vizuri kilitokea kitu gani..na walichukua hatua gani kuhakikisha kitu kama hicho hakiwezi kutokea....

Zaidi ya yote mkuu mimi nina mashaka kuwa huyu jamaa kaingia mitini isipokuwa wanajaribu kutuchezea vichwa ili kesho Mramba, Yona and the likes wakiingia mitini isionekane kuwa ni jambo geni..huyu jamaa yupo tu nchini kajichimbia mahala, itategemea na reaction yetu...atakimbilia wapi!..
On the otherhand, tukirudi ktk usemi ule wa Watu na Mazingira, mchezo huu unaweza kuwa umechezwa kati ya mawakili wa Liyumba, Prosecutor na Hakimu kupitisha dhamana yenye masharti madogo ya ulinzi ili jamaa aingie mitini..Fedha inaweza kufuta madhambi yako..Lakini bado ni jukumu la wizara ya mambo ya ndani wakishirikiana na PCCB kufuatilia swala hili la fugitive..
Haya mambo ya kusema sio jukumu langu ndio yametukwamisha kuweza kusimamisha kesi nyingine za mafisadi...Na ukweli upo kwa Mkapa, watanzania woite hatufahamu ni jukumu la nani kufungua mashtaka dhidi ya rais mstaafu hata kama sheria ipo ndani ya katiba..
 
Kama kweli atakuwa bado yuko yuko ina maanisha pccb haina ushirikiano wa karibu na mahakama yaani vyombo vyetu vya usalama haviaminiani na havina ushirikiano wa karibu mpaka pccb waamue kutoa donge nono wakati hawana uhakika na kinachoendelea

si ajabu kesho tukasikia mtu kapewa hilo donge nono
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…