Kama ni kweli itathibitishwa Liyumba ametoroka, kwa mujibu wa mwenendo wa kesi za jinai, kesi hiyo kesho inafutwa rasmi na mtuhumiwa anaachiwa huru.
Hivi ndivyo ilivyofanyika wakati wa Kesi ya Pili ya Uhaini Tanzania, Mwaka 1983, baada ya kutoroka gereza la Ukonga, Mshtakiwa wa kwanza, Father Tom na mshtakiwa wa pili, Hatty McGhee, kesi hiyo ilifutwa rasmi na washtakiwa wengine wote 29 waliachiwa huru. Hata hivyo, washtakiwa wote walikamatwa mara tuu baada ya kutoka mahakani na kesho yake walifikishwa tena mahakamani kusomewa mashitaka mapya.
Kwa hiyo kesi ya Liyumba itafutwa kesho, mshtakiwa mwenza ataachiwa huru, labda serikali ikiamua kumkamata tena na kumfungulia kesi mpya.
Pamoja na jamaa kutoroka, serikali ilikurupuka kufungua mashtaka ya thamani yote ya majengo pacha kana kwamba mradi mzima ni mradi batili.
Angetokea mwanasheria wa John Cochram type, angemwambia Liyummba na mwenzake wakubali kosa, wairudishie serikali hizo
Bilioni 200 na majengo pacha yawe ya mwekezaji mpya.
The-proper charge ya kuitia hasara serikali, ilikuwa ifanyike baada ya valuation ya Twin Towers. Then unacompare value halisi na value iliyozidishwa, ndipo unawafungulia kesi ya kusababisha hasara ya kile kiasi tuu kilichozidi.
Pamoja na hasira zetu zote kuhusiana na hivi vitendo vya ufisadi,
Waliovitenda ni binadamu, hivyo ubinadamu uko pale pale kama Mkapa anavyoheshimiwa pamoja na madudu yote yaliyofanyika wakati wa utawala wake.