Kesi ya Malisa kituko! Wafika Mahakamani leo Julai 18 wakuta haijasajiliwa!

Kesi ya Malisa kituko! Wafika Mahakamani leo Julai 18 wakuta haijasajiliwa!

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
malisa.png

Kesi ya uchochezi inayomkabili Mwanaharakati na Mkurugenzi wa GH Foundation, Godlisten Malisa imezua sintofahamu baada ya kufika mahakamani leo, Julai 18, 2024 mkoani Kilimanjaro na kukuta kesi hiyo bado haijasajiliwa.

Pia soma: Kilimanjaro: Godlisten Malissa afikishwa Mahakamani

Malisa akiongozana na mawakili wake watatu kati ya saba, wakiwamo Dickson Matata, Hekima Mwasipu na Peter Kidumbuo, walifika mahakamani hapo saa tatu asubuhi kama alivyotakiwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Kilimanjaro (RCO) kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo inayomkabili.

Pia soma: Malisa aripoti Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi, ajulishwa kuwa upelelezi haujakamilika

Wengine waliofika mahakamani hapo ni wafanyakazi wa taasisi yake, akiwamo James Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Kilimanjaro, Michael Kilawila na marafiki zake wa karibu.

Mwananchi
 
Hii nchi unaitwa uende mahakamani kwenye kesi unafika vizuri unakuta haijasajiliwa? Hakuna aliye serious na kazi
 
Naanza kuona uchovu wa serikali ya CCM unahamia kwenye mihimili mingine ya nchi, mahakama nayo imeanza kuchoka kwa mtindo huo huo.

Lile bunge la Spika Tulia nalo lilishachoka siku nyingi, tangu liamue kupigia mstari kuruhusu maliasili za taifa kutolewa bure kwa wageni.

Uchovu wa serikali unaonekana kuwa cancer iliyoanza kuitafuna nchi yertu kwa namna tofauti, kwenye idara tofauti.

Tumebaki watanganyika, nasi tumeshachoshwa na uchovu wa serikali ya CCM au bado tuna nguvu? kwa namna tulivyokimya kuyafanyia kazi mapema mabaya ya hii serikali sielewi ukimya wetu ni dalili ya uchovu, au bado tuna nguvu tunaendelea kuwahesabia siku wahuni!
 
Back
Top Bottom