KESI YA MAUAJI: Utetezi wa Elizabeth Michael (Lulu) ndani ya mahakama kuu

KESI YA MAUAJI: Utetezi wa Elizabeth Michael (Lulu) ndani ya mahakama kuu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
=> "Nilipofika kwa marehemu 'Kanumba' nilimkuta yupo kwenye dressing table, nilikaa kitandani kwa kuwa hapa kuwa na sehemu ya kukaa"- Lulu

=> "Nilikuwa nataka kutoka ila marehemu 'Kanumba' alinikataza, alikuwa hataki nitoke na marafiki zangu"- Lulu

=> Mara nyingi marehemu alikuwa ananipiga kila akilewa na sio kwa akili zake"- Lulu

=> Marehemu nilipomwambia natoka na marafiki zangu alinikimbiza na taulo na mimi nilikuwa naogopa kupigwa"-Lulu

=> "Alipoona simu yangu inaita akahisi ni simu ya mwanaume akasema kwanini naongea na simu ya mwanaume mbele yake?"

=> Marehemu akaingia uvunguni akatoa panga akasema leo nakuua huku akinipiga na panga kwenye mapaja" - Lulu

=> "Nilipoona hivyo ananikimbiza na taulo nilitoka nikakimbilia chooni na kupiga kelele - Lulu

=> "Marehemu alianguka mwenyewe na kujigonga kwa nguvu na kuinuka sehemu nyingine alikuwa kama anatapatapa - Lulu

=> "Baada ya muda mchache nilisikia kishindo kama mtu anafungua mlango - Lulu

=> "Nilimkuta amelala, nilihisi amejifanyisha nikaanza kumwambia kuwa wakija watu nitawambia kila kitu ulivyonipiga na panga"

=> "Nilimwambia Seth kuwa Kanumba amedondoka na akajaribu kumuamsha hakuamka akasema anaenda kumuita daktari" -Lulu

=> "Alivyosema anaenda kumuita daktari nikasema na mimi naondoka nikiogopa anaweza akaamka akaanza kunipiga - Lulu

=> "Niliondoka nikawasha gari kuelekea Coco Beach, Huko Coco Beach hakukuwa na kitu nilienda tu kutuliza akili - Lulu

=> "Nilivyofika Coco Beach SMS zilianza kusambaa kuniuliza kuwa nasikia Kanumba amefariki - Lulu

=> "Nikachukua simu nikampigia kidume 'rafiki yake Kanumba' kumuuliza Kanumba yupo hospitali gani? nije kumuona-Lulu

=> "Akaniambia wewe usije hospitali, niambie uko wapi tuonane Bamaga? "- Lulu

=> "Tulivyokutana Bamaga alikuwa kama anataka kuongea na mimi ghafla wakaja askari kunikamata - Lulu

=> "Na kunipeleka Oysterbay polisi, Nilipofika Oysterbay nilikuta watu wengi sana niliyemtambua ni Ray- Lulu

=> "Nilijua Kanumba amefariki nikiwa polisi"- Lulu

=> "Nilipomkuta Ray Oysterbay polisi nikajua Kanumba amekamatwa kwasababu ya makelele niliyokuwa nayapiga kule nikajua watu walisikia" - Lulu

=> "Kwa namna yoyote ile mimi sijasababisha kifo cha Kanumba, na mimi ndiye nilieshambuliwa na marehemu " - Lulu

=> ....kutokana na umbile langu nilikuwa mdogo na alikuwa na uwezo wa kufanya chochote kwenye mwili wangu kwa sababu yeye ndo alikuwa na silaha

Maswali kutoka kwa wakili wa serikali


=> Wakili wa Serikali = Wewe na Kanumba mlianza mahusiano kwa muda gani?
= "KWA MIEZI MINNE" - Lulu

=> Wakili wa Serikali "Inamaana Kanumba alikukimbiza na taulo mpk nje halikuanguka?"
= Jibu "NDIO ALINIKIMBIZA AKIWA PEKU NA TAULO" - Lulu


Chanzo: BONGO 5

====================================

USHAHIDI ALIOUTOA LULU MAHAKAMANI KUHUSU KIFO CHA KANUMBA

Msanii wa filamu, Elizabeth Michael (22) amejitetea katika kesi ya kuuwa bila kukusudia katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Katika utetezi wake, Lulu amesema anakumbuka siku ya tukio ilikuwa Ijumaa ya April 6/2017 ambapo aliahidiana na rafiki zake kwamba wangetoka usiku.

Amesema kuwa asubuhi ya siku hiyo alienda kuonana na rafiki zake maeneo ya Mikocheni, ambapo pia alikuwa akiwasiliana na Kanumba.

"Marehemu alikuwa ni msanii mwenzangu lakini pia nilikuwa naye na mahusiano naye ya kimapenzi,".

Lulu alisema kuwa marehemu Kanumba alikuwa hapendi kumuona akitoka, hivyo hadi siku ya tukio hakutaka kumwambia kwamba atatoka na rafiki zake.

"Hata hivyo ilipofika saa 6 kasoro usiku, nilimpigia simu Kanumba na kumwambia nataka nitoke na rafiki zangu, hivyo nitapitia nyumbani kwake nimuage,".

Lulu amesema alienda hadi nyumbani kwa marehemu, ambapo ni Sinza Vatican na akamwambia akikaribia atampigia simu.

" Nilipompigia tena simu akanambia anataka kwenda kuoga, hivyo kama nikifika nipitilize hadi chumbani maana hataweza kupokea simu, ".

Lulu amesema kuwa alipofika nyumbani aliingia mpaka chumbani, ambapo alimkuta Kanumba akiwa kwenye dressing table akipaka mafuta kwenye nywele, huku akiwa anakunywa pombe aina ya Jack Daniel.

Amesema kuwa kutokana na chumba hicho kutokuwa na sehemu ya kukaa, aliamua kukaa kitandani huku akisalimiana na marehemu.

"Baada ya muda kidogo simu ya Kanumba ikaita ambapo alikuwa akiongea na Charles Baba akimuuliza kama ataenda kwenye muziki wa bendi usiku huo, ambapo Kanumba alimwambia anamalizia kujiandaa anakuja,ambapo na mimi nikamwambia nataka nitoke na rafiki zangu,".

Lulu amesema kuwa baada ya kumwambia Kanumba kuwa anataka kutoka alianza kuumuliza anataka kwenda wapi.

" Nilimjibu kuwa nataka nitoke na rafiki zangu twende Disco mimi sipendi muziki wa Dansi kwani nj kama wakizee, lakini yeye alikuwa hataki badala yake anataka twende wote kwenye dansi,".

Lulu ameeleza kuwa wakati akiendelea kuongea na Kanumba, simu yake ikawa inaita ambapo aliogopa kupokea mbele ya Kanumba kwa sababu alihisi rafiki zake wanampigia, hivyo endapo wangemuuliza kuhusu suala la kutoka basi Kanumba angesikia.

Kutokana na hali hiyo, Lulu alisema kuwa aliamwambia Kanumba kwamba anataka akachukue Maji ya kunywa jikoni.

"Nikiwa naelekea kuchukia Maji nilipokea simu, ambapo nikaanza kuongea na rafiki zangu kwamba wasubiri nitatoka, lakini wakati nakata simu Kanumba alikuwa ananifatilia kwa nyuma na kuanza kuniuliza naongea na nani,

" Niliogopa kumwambia kwa sababu ningemwambia naongea na rafiki zangu kuhusu kutoka angenipiga, nikaanza kumtania kwa kumwambia unanifata hadi jikoni kujua naongea na nani,".

Akiendelea na ushahidi wake, Lulu amesema kuwa Kanumba alikuwa akimuuliza anaongea na nani huku akimfata, na akiwa katika hali ya kukasirika ambapo yeye akawa anarudi nyuma.

"Wakati wote huo alikuwa katika hali ya kulewa, hivyo wakati ananifata nikahisi anataka kunipiga na mimi nikawa nazidi kurudi nyuma nikafungua mlango na nikatoka hadi nje,".

Amesema kuwa aliamua kutoka nje akiamini kwamba Kanumba asingeweza kumfata kwa sababu alivaa taulo na alikuwa tumbo wazi, hivyo angeona aibu na angeshindwa kumfata kulingana na umaarufu wake.

" Hata hivyo aliendelea kunifata, ambapo alinikimbiza hadi getini na akatoka hadi nje ya geti akiwa peku peku,".

Lulu amebainisha kuwa kutokana na hali hiyo aliamua kukimbia hadi lilipo gofu la baa ya Vatican ambayo ilikuwa haifanyi Kazi kwa wakati huo.

"Wakati tukio likiendelea umeme ulikatika, ambapo mimi niliingia hadi kwenye ghofu hilo na kujificha, lakini Kanumba alinifata hadi nilipojificha na kuanza kunipiga makofi ya uso,".

Amesema kuwa baada ya kumpiga alimshika mikono na kuanzia kumburuza kutoka nje hadi kumuingiza ndani, ambapo alimuingiza hadi chumbani kwake kisha kufunga mlango na funguo, kisha kumrusha kitandani.

"Baada ya kunitupa kitandani, aliinama chini na kuchukua Panga ambapo akaanza kunipiga nalo kwenye ubapa hasa maeneo ya mapajani, kutokana na mimi nilikuwa natapatapa ambapo nilijiziba uso ili asiweze kunikata huku nikipiga kelele za kuomba msaada,

*wakati akinipiga alikuwa akilalamika kwamba kwanini naongea na simu na mwanaume mwingine mbele yake,".

Lulu amebainisha kuwa wakati Kanumba akimpiga alikuwa katika hali ya jazba na kuema kwa haraka.

" Ghafla nikasikia sauti ya Panga limedondoka chini, pia nikasikia sauti kama ya mtu amekabwa, ambapo nilitoa mikono na kuona ameanguka kwa kujigonga kichwani kwenye ukuta, kisha akawa kama mtu anayetapatapa ambapo alirudi tena nyuma na kujigonga ukutani,,".

Lulu amesema kuwa kutokana na hali hiyo, aliinuka kutoka kitandani na kukimbilia chooni kwa ajili ya kujificha, huku akiwa anapiga kelele za kuomba msaada.
 
=> "Nilipofika kwa marehemu 'Kanumba' nilimkuta yupo kwenye dressing table, nilikaa kitandani kwa kuwa hapa kuwa na sehemu ya kukaa"- Lulu

=> "Nilikuwa nataka kutoka ila marehemu 'Kanumba' alinikataza, alikuwa hataki nitoke na marafiki zangu"- Lulu

=> Mara nyingi marehemu alikuwa ananipiga kila akilewa na sio kwa akili zake"- Lulu

=> Marehemu nilipomwambia natoka na marafiki zangu alinikimbiza na taulo na mimi nilikuwa naogopa kupigwa"-Lulu

=> "Alipoona simu yangu inaita akahisi ni simu ya mwanaume akasema kwanini naongea na simu ya mwanaume mbele yake?"

=> Marehemu akaingia uvunguni akatoa panga akasema leo nakuua huku akinipiga na panga kwenye mapaja" - Lulu

=> "Nilipoona hivyo ananikimbiza na taulo nilitoka nikakimbilia chooni na kupiga kelele - Lulu

=> "Marehemu alianguka mwenyewe na kujigonga kwa nguvu na kuinuka sehemu nyingine alikuwa kama anatapatapa - Lulu

=> "Baada ya muda mchache nilisikia kishindo kama mtu anafungua mlango - Lulu

=> "Nilimkuta amelala, nilihisi amejifanyisha nikaanza kumwambia kuwa wakija watu nitawambia kila kitu ulivyonipiga na panga"

=> "Nilimwambia Seth kuwa Kanumba amedondoka na akajaribu kumuamsha hakuamka akasema anaenda kumuita daktari" -Lulu

=> "Alivyosema anaenda kumuita daktari nikasema na mimi naondoka nikiogopa anaweza akaamka akaanza kunipiga - Lulu

=> "Niliondoka nikawasha gari kuelekea Coco Beach, Huko Coco Beach hakukuwa na kitu nilienda tu kutuliza akili - Lulu

=> "Nilivyofika Coco Beach SMS zilianza kusambaa kuniuliza kuwa nasikia Kanumba amefariki - Lulu

=> "Nikachukua simu nikampigia kidume 'rafiki yake Kanumba' kumuuliza Kanumba yupo hospitali gani? nije kumuona-Lulu

=> "Akaniambia wewe usije hospitali, niambie uko wapi tuonane Bamaga? "- Lulu

=> "Tulivyokutana Bamaga alikuwa kama anataka kuongea na mimi ghafla wakaja askari kunikamata - Lulu

=> "Na kunipeleka Oysterbay polisi, Nilipofika Oysterbay nilikuta watu wengi sana niliyemtambua ni Ray- Lulu

=> "Nilijua Kanumba amefariki nikiwa polisi"- Lulu

=> "Nilipomkuta Ray Oysterbay polisi nikajua Kanumba amekamatwa kwasababu ya makelele niliyokuwa nayapiga kule nikajua watu walisikia" - Lulu

=> "Kwa namna yoyote ile mimi sijasababisha kifo cha Kanumba, na mimi ndiye nilieshambuliwa na marehemu " - Lulu

=> ....kutokana na umbile langu nilikuwa mdogo na alikuwa na uwezo wa kufanya chochote kwenye mwili wangu kwa sababu yeye ndo alikuwa na silaha

Maswali kutoka kwa wakili wa serikali


=> Wakili wa Serikali = Wewe na Kanumba mlianza mahusiano kwa muda gani?
= "KWA MIEZI MINNE" - Lulu

=> Wakili wa Serikali "Inamaana Kanumba alikukimbiza na taulo mpk nje halikuanguka?"
= Jibu "NDIO ALINIKIMBIZA AKIWA PEKU NA TAULO" - Lulu
Kwa utetezi huu inaonyesha kiasi fulani ali plan kama self defence fulani.
 
Hivi mtu unayempenda unaku.tia kila siku kaanguka ghafla ndugu yake anasema namtafuta Dr aje ww unaweza kweli ukaenda coco kula upepo. Huyu dogo ahojiwe vzuri.
Noma sana..
 
ila hapo pa kutoka kuwasha gari kwenda coco pana mushkeli
Mushkeli uko wap, kumbuka alikua tayar kakimbilia kujificha chooni. Mtu kaanguka unaskia kishindo. Halafu unaambiwa mtu ghafla anaumwa ngoja aje daktari, hujui anaumwa nn kwa kiasi gan, na mnaugomvi. Ungekua ni ww umefanikiwa kuchoropoka chooni utabaki ndani unamsubir tena daktari na huna uhakika kama kwel anaumwa au atazinduka ghafla.

Issue ya kwamba alienda Coco sio issue hata. Coco kuna club na sehem za refreshment (sio alienda kukaa kwenye mchanga wa bahari au kuogelea). Wenyewe walitaka aende wap sasa?

In my case I honestly buy her statements. Ni logical kabisa.
 
Back
Top Bottom