Kesi ya Mbowe: Maslahi gani Washitakiwa kunyimwa Haki?

Kesi ya Mbowe: Maslahi gani Washitakiwa kunyimwa Haki?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Jambo la kupongezwa kuona mawakili wa utetezi wakipambana vilivyo kuona haki za washitakiwa haziporwi.

Hata hivyo inashangaza ni kwa motisha gani upande wa mashtaka kupambana kikuku kuona ikiwezekana washitakiwa hawapati haki zao.

Faulo za upande wa mashtaka ziko nyingi na ziko wazi:

1. Kwenye shauri la Adamoo wakiwa wameahidi kuleta shahidi wao mwingine, walifunga sehemu yao ya ushahidi ghafla asubuhi asubuhi. Hatua hii ikawawekea shinikizo utetezi kuanza bila kutarajia na (labda) bila kujiandaa kikamilifu.

2. Leo wakiwa pia wameahidi kuleta shahidi, wamefika mahakamani wakiwa wamechelewa na ghafla bila kutarajiwa wakafunga sehemu yao ya ushahidi. Kama #1 wakawaweka upande wa utetezi katika kuendelea na kesi.

3. Si mara moja, wakiamua hupoteza muda ili kesi iahirishwe kwa maslahi yao. Wamefanya hivyo pia leo.

4. Wao hukomaa kweli kweli ili kuingiza exhibits zozote hata kama ni zenye utata mtupu.

5. Wameonekana kukomaa pia kuzuia kata kata Ling'wenya asiwasilishe chochote kinachoweza kumsaidia katika lolote analoshtakiwa.

Hali hii kibinadamu inashangaza na kutia kichefu chefu. Hasa ikizingatiwa kuwa wanafanya hivi kinadharia kwa niaba yetu.

Izingatiwe Ling'wenya ni komando aliyelitumikia taifa hili na hawa jamaa ni watu wanaokula kodi zetu mahotelini pasipokuwa na ridhaa zetu:

IMG_20211125_174519_783.jpg


Hivi kwani, hawapo mawakili wa serikali Dar? Au hizi per diem ni sehemu ya motisha huo?

Au hawa ndugu wana ahadi fulani fulani zenye kufungua fursa zaidi kwao?

Walisema kua uyaone: "haki za watu zinapogeuka kuwa bidhaa kama nyanya tu, gengeni."

Utetezi: "Kwa mustakabala huu chonde chonde, hakuna kimwangalia nyani usoni."

Ushahidi wa kisayansi ni takwa la msingi wala si ombi tena. Jiwe moja lisibakie juu ya jingine.

---------
Kesi ya Mbowe: Madai Mahakamani yathibitishwe Kisayansi
 
Safi sana. Umeshtukia mchezo! Basi mie nilijua wote ni wa Dar - kumbe! Perdiems tu. Hizo bado za Jaji mwenyewe manake ninasikia anatokea Mwanza. Ila wacha tu Mbowe afungwe - ni mbegu njema inapandwa kwa ajili ya ukombozi wa kunyanyaswa!

Ila wajue patachimbika na si cha mtoto.
 
Kesi kuanza saa 6 huku Jaji aliamuru saa 3 nini maana yake.

Kibatala " Wengine wanajiona bora zaidi ya wengine"Kwenye ulingo wa sheria wote ni sawa.Je neno wakili msomi limefutika

Tafsiri zikoje kibinadamu.

Palikuwa na uzi hapa kumhusu huyu jaji kutoka kanda ya Mwanza:

Kufanana na kutofautiana kwa Majaji Tiganga na Siyani

Huyu anashuku shahidi Ling'wenya anapata usaidizi tokea nje ya kizimba wakati shahidi Msemwa kupiga chabo kizimbani hiyo sawa.
 
Jambo la kupongezwa kuona mawakili wa utetezi wakipambana vilivyo kuona haki za washitakiwa haziporwi.

Hata hivyo inashangaza ni kwa motisha gani upande wa mashtaka kupambana kikuku kuona ikiwezekana washitakiwa hawapati haki zao.

Faulo za upande wa mashtaka ziko nyingi na ziko wazi:

1. Kwenye shauri la Adamoo wakiwa wameahidi kuleta shahidi wao mwingine, walifunga sehemu yao ya ushahidi ghafla asubuhi asubuhi. Hatua hii ikawawekea shinikizo utetezi kuanza bila kutarajia na (labda) bila kujiandaa kikamilifu.

2. Leo wakiwa pia wameahidi kuleta shahidi, wamefika mahakamani wakiwa wamechelewa na ghafla bila kutarajiwa wakafunga sehemu yao ya ushahidi. Kama #1 wakawaweka upande wa utetezi katika kuendelea na kesi.

3. Si mara moja, wakiamua hupoteza muda ili kesi iahirishwe kwa maslahi yao. Wamefanya hivyo pia leo.

4. Wao hukomaa kweli kweli ili kuingiza exhibits zozote hata kama ni zenye utata mtupu.

5. Wameonekana kukomaa pia kuzuia kata kata Ling'wenya asiwasilishe chochote kinachoweza kumsaidia katika lolote analoshtakiwa.

Hali hii kibinadamu inashangaza na kutia kichefu chefu. Hasa ikizingatiwa kuwa wanafanya hivi kinadharia kwa niaba yetu.

Izingatiwe Ling'wenya ni komando aliyelitumikia taifa hili na hawa jamaa ni watu wanaokula kodi zetu mahotelini pasipokuwa na ridhaa zetu:

View attachment 2023282

Hivi kwani, hawapo mawakili wa serikali Dar? Au hizi per diem ni sehemu ya motisha huo?

Au hawa ndugu wana ahadi fulani fulani zenye kufungua fursa zaidi kwao?

Walisema kua uyaone: "haki za watu zinapogeuka kuwa bidhaa kama nyanya tu, gengeni."

Utetezi: "Kwa mustakabala huu chonde chonde, hakuna kimwangalia nyani usoni."

Ushahidi wa kisayansi ni takwa la msingi wala si ombi tena. Jiwe moja lisibakie juu ya jingine.

---------
Kesi ya Mbowe: Madai Mahakamani yathibitishwe Kisayansi
Kwa nini unalalamikia mawakili wetu kulipwa posho ya kujikimu wanayolipwa wakati wakipambana kisheria na magaidi hatari ya kiwango cha ukomando yaliyokusudia kuvuruga taifa letu? Mbona huwa hulalamikii maposho kedekede yanayolipwa kwa wabunge wetu kwa ajili ya kukaa tu bungeni hata kama muda mwingi wanasinzia tu bungeni (walio wengi wasiochangia cho chote mjengoni).
 
Kwa nini unalalamikia mawakili wetu kulipwa posho ya kujikimu wanayolipwa wakati wakipambana kisheria na magaidi hatari ya kiwango cha ukomando yaliyokusudia kuvuruga taifa letu? Mbona huwa hulalamikii maposho kedekede yanayolipwa kwa wabunge wetu kwa ajili ya kukaa tu bungeni hata kama muda mwingi wanasinzia tu bungeni (walio wengi wasiochangia cho chote mjengoni).

Labda wewe kama ni mgeni, kwamba una kamba mguuni:

1. Kuhusiana na bungeni tumeandika na kuandika na bado hatujachoka. Hii ikiwamo kuukabili ule mbuyu wenyewe:

Ndugai: Ya Ulimwengu ni Maoni ya Wengi

Ndugai: Uhuru wa kukusanyika ni upi?

Kwani huja watambua humo kwenye jungu kuu hili?

IMG_20211119_091739_123.jpg


2. Mawakili wenu wapi unaona waongelea wewe dhidi ya gaidi yupi?

Lijenje, Adamoo, Bwire, Ling'wenya, Mbowe na wenzao ni victims wa kubambikiwa kesi na hukumu batili zilizoandaliwa nje ya mahakama.

Hawa wataingia kwenye vitabu vya historia vya nchi hii kama mashujaa wetu wakiwa hai au wafu.

Pana watu mko nao kwenye jungu hilo kuu (mark my words):

IMG_20211119_091739_123.jpg


mtajikuta kwenye mahakama za haki kutuelezea kinagaugaba waliko kina Lijenje, Ben, Azory, jinsi mlivyo ratibu ya Lissu na nani mliwaweka kwenye viroba.

Tayari Sabaya anawakilisha na mwingine mpendwa anasemekana yuko kwenye pipeline njia moja anakuja.

Kwamba "mawakili wetu?" Tafadhali usitujumuishe na sisi wengine humo. Kwa kweli ni kutukosea sana kutujumuisha sisi kama tunavyoonekana nje ya sufuria:

IMG_20211119_091739_123.jpg


Si mbaya ukajua malipo yao, kwetu tuna hesabu hasara tu kwa taifa hili maskini linaobambikizia watu wake kodi na tozo lukuki ambao kwenye sufuria haziwahusu.

Habari ndiyo hiyo.
 
CCM janga la Taifa.Ila auaye kwa upanga,nae hufa kwa upanga.Jiwe hivi yupo ziara ya mkoa gani vile!.

Maana yeye ndo mwenye haki ya kuongea na wanannchi.ila wengine mpaka kwenye majimbo yao.

Swali,je uchaguzi ulikuwa fear.mtafuteni atupe majibu.
Tumwongezee mhura,angarau miaka 7
 
Jambo la kupongezwa kuona mawakili wa utetezi wakipambana vilivyo kuona haki za washitakiwa haziporwi.

Hata hivyo inashangaza ni kwa motisha gani upande wa mashtaka kupambana kikuku kuona ikiwezekana washitakiwa hawapati haki zao.

Faulo za upande wa mashtaka ziko nyingi na ziko wazi:

1. Kwenye shauri la Adamoo wakiwa wameahidi kuleta shahidi wao mwingine, walifunga sehemu yao ya ushahidi ghafla asubuhi asubuhi. Hatua hii ikawawekea shinikizo utetezi kuanza bila kutarajia na (labda) bila kujiandaa kikamilifu.

2. Leo wakiwa pia wameahidi kuleta shahidi, wamefika mahakamani wakiwa wamechelewa na ghafla bila kutarajiwa wakafunga sehemu yao ya ushahidi. Kama #1 wakawaweka upande wa utetezi katika kuendelea na kesi.

3. Si mara moja, wakiamua hupoteza muda ili kesi iahirishwe kwa maslahi yao. Wamefanya hivyo pia leo.

4. Wao hukomaa kweli kweli ili kuingiza exhibits zozote hata kama ni zenye utata mtupu.

5. Wameonekana kukomaa pia kuzuia kata kata Ling'wenya asiwasilishe chochote kinachoweza kumsaidia katika lolote analoshtakiwa.

Hali hii kibinadamu inashangaza na kutia kichefu chefu. Hasa ikizingatiwa kuwa wanafanya hivi kinadharia kwa niaba yetu.

Izingatiwe Ling'wenya ni komando aliyelitumikia taifa hili na hawa jamaa ni watu wanaokula kodi zetu mahotelini pasipokuwa na ridhaa zetu:

View attachment 2023282

Hivi kwani, hawapo mawakili wa serikali Dar? Au hizi per diem ni sehemu ya motisha huo?

Au hawa ndugu wana ahadi fulani fulani zenye kufungua fursa zaidi kwao?

Walisema kua uyaone: "haki za watu zinapogeuka kuwa bidhaa kama nyanya tu, gengeni."

Utetezi: "Kwa mustakabala huu chonde chonde, hakuna kimwangalia nyani usoni."

Ushahidi wa kisayansi ni takwa la msingi wala si ombi tena. Jiwe moja lisibakie juu ya jingine.

---------
Kesi ya Mbowe: Madai Mahakamani yathibitishwe Kisayansi
Na wao ni kikosi kimoja na Kingai. Wasio julikana
 
CCM janga la Taifa.Ila auaye kwa upanga,nae hufa kwa upanga.Jiwe hivi yupo ziara ya mkoa gani vile!.

Maana yeye ndo mwenye haki ya kuongea na wanannchi.ila wengine mpaka kwenye majimbo yao.

Swali,je uchaguzi ulikuwa fear.mtafuteni atupe majibu.
Tumwongezee mhura,angarau miaka 7

Hivi wanapojitathimini wanaona wanaifanyia hii nchi service kweli?

Hiiiiii bagosha!
 
Kesi kuanza saa 6 huku Jaji aliamuru saa 3 nini maana yake.

Kibatala " Wengine wanajiona bora zaidi ya wengine"Kwenye ulingo wa sheria wote ni sawa.Je neno wakili msomi limefutika

Tafsiri zikoje kibinadamu.

Utakuwa umegundua hilo. Wameanza hata kuitana “Mr. Hilla” na Mtobesya akauliza “na nikielezea sababu watafanya nini?”. Mara jaji nae “mimi mnanipa wakati mgumu na nyie mko huko”. Wakili was Serikali nae “watake wasitake, sisi pia ni mawakili wa mahakama”.

Gloves off, bare nuckles week ijayo!! Na hakimu bahati mbaya alikubali barua ya shahidi ambayo mazingira yanafanana na hii inayopingwa sasa. Utetezi wanamkumbusha hilo!!
 
Jambo la kupongezwa kuona mawakili wa utetezi wakipambana vilivyo kuona haki za washitakiwa haziporwi.

Hata hivyo inashangaza ni kwa motisha gani upande wa mashtaka kupambana kikuku kuona ikiwezekana washitakiwa hawapati haki zao.

Faulo za upande wa mashtaka ziko nyingi na ziko wazi:

1. Kwenye shauri la Adamoo wakiwa wameahidi kuleta shahidi wao mwingine, walifunga sehemu yao ya ushahidi ghafla asubuhi asubuhi. Hatua hii ikawawekea shinikizo utetezi kuanza bila kutarajia na (labda) bila kujiandaa kikamilifu.

2. Leo wakiwa pia wameahidi kuleta shahidi, wamefika mahakamani wakiwa wamechelewa na ghafla bila kutarajiwa wakafunga sehemu yao ya ushahidi. Kama #1 wakawaweka upande wa utetezi katika kuendelea na kesi.

3. Si mara moja, wakiamua hupoteza muda ili kesi iahirishwe kwa maslahi yao. Wamefanya hivyo pia leo.

4. Wao hukomaa kweli kweli ili kuingiza exhibits zozote hata kama ni zenye utata mtupu.

5. Wameonekana kukomaa pia kuzuia kata kata Ling'wenya asiwasilishe chochote kinachoweza kumsaidia katika lolote analoshtakiwa.

Hali hii kibinadamu inashangaza na kutia kichefu chefu. Hasa ikizingatiwa kuwa wanafanya hivi kinadharia kwa niaba yetu.

Izingatiwe Ling'wenya ni komando aliyelitumikia taifa hili na hawa jamaa ni watu wanaokula kodi zetu mahotelini pasipokuwa na ridhaa zetu:

View attachment 2023282

Hivi kwani, hawapo mawakili wa serikali Dar? Au hizi per diem ni sehemu ya motisha huo?

Au hawa ndugu wana ahadi fulani fulani zenye kufungua fursa zaidi kwao?

Walisema kua uyaone: "haki za watu zinapogeuka kuwa bidhaa kama nyanya tu, gengeni."

Utetezi: "Kwa mustakabala huu chonde chonde, hakuna kimwangalia nyani usoni."

Ushahidi wa kisayansi ni takwa la msingi wala si ombi tena. Jiwe moja lisibakie juu ya jingine.

---------
Kesi ya Mbowe: Madai Mahakamani yathibitishwe Kisayansi
kama mawakili wa serikali wanafanay faulo, hao mawakili wa mbowe wanashindwa nini kufanay faulo na kuwashtukiza kama wano wanavyofanyiwa? nao si mawakili ama? kama kuna mapingamizi ambayo mawakili wa serikali wanayaleta ili adamoo asiingize ushahidi, je? ni mapingamizi ya kisheria au la, mawakili wenu si wapo pale kuwajibu? wewe unapowajibia kwani mawakili wa chadema hawawezi kazi? na je? waendesha mashtaka wakileta nyaraka na ushahidi mawakili wa mbowe hawapingi? kwahiyo kupinga wanatakiwa kupinga mawakili wa mbowe tu,wakipinga mawakili wa serikali nongwa? hebu jaribu kutafakari.
 
Safi sana. Umeshtukia mchezo! Basi mie nilijua wote ni wa Dar - kumbe! Perdiems tu. Hizo bado za Jaji mwenyewe manake ninasikia anatokea Mwanza. Ila wacha tu Mbowe afungwe - ni mbegu njema inapandwa kwa ajili ya ukombozi wa kunyanyaswa!
msishangae per diems, inavyoonekana DPP amechuja akachukua watu wale bora sana kwenye prosecution, ndio maana wanawapa ugumu sana kina kibatala, hao wote wameenda hapo ni wazoefu sana kwenye prosecutions.
 
kama mawakili wa serikali wanafanay faulo, hao mawakili wa mbowe wanashindwa nini kufanay faulo na kuwashtukiza kama wano wanavyofanyiwa? nao si mawakili ama? kama kuna mapingamizi ambayo mawakili wa serikali wanayaleta ili adamoo asiingize ushahidi, je? ni mapingamizi ya kisheria au la, mawakili wenu si wapo pale kuwajibu? wewe unapowajibia kwani mawakili wa chadema hawawezi kazi? na je? waendesha mashtaka wakileta nyaraka na ushahidi mawakili wa mbowe hawapingi? kwahiyo kupinga wanatakiwa kupinga mawakili wa mbowe tu,wakipinga mawakili wa serikali nongwa? hebu jaribu kutafakari.

Haki na udhwalimu havikai upande mmoja.

Kuna aliyewauwa kina Lijenje, Ben, Azory na wengine. Bado akaweka na wengine kwenye viroba. Akapanga mazishi ya watu walio hai. Akajiita mzalendo.

Atamfundisha nani uzalendo mtu huyo?

Ninakazia, haki na udhwalimu havikai upande mmoja. Chagua upande wako ubakie huko huko.
 
msishangae per diems, inavyoonekana DPP amechuja akachukua watu wale bora sana kwenye prosecution, ndio maana wanawapa ugumu sana kina kibatala, hao wote wameenda hapo ni wazoefu sana kwenye prosecutions.

Jaji naye katoka Mwanza. Yeye ni mzoefu kwenye nini?

Si mseme tu per diem hizi ni sehemu ya marupurupu kwenye kufanikisha yaliyopo tayari mifukoni?
 
Back
Top Bottom