Kesi ya Mbowe na wanasheria wa Tigo na Airtel ikumbushe wenye mamlaka kutunza siri za wateja ni muhimu kujenga sekta imara ya benki na mawasiliano

Kesi ya Mbowe na wanasheria wa Tigo na Airtel ikumbushe wenye mamlaka kutunza siri za wateja ni muhimu kujenga sekta imara ya benki na mawasiliano

Shahidi wa leo, kwenye kesi dhidi ya Mh. Mbowe na wenzake, bwana Fredy ametudhihirishia wateja wa mitandao ya simu kuwa polisi wanaweza kwenda kwenye hii mitandao na kuwaambia wenye mitandao wawape taarifa zako zote, kama mawasiliano, ulipo, miamala yako, wao hata hawaulizi ni kwaajili ya nini, wanawapa.

Watanzania hatupo salama kiusalama wala kifaragha, kila unapotumia mtandao wa simu. Polisi mwenye nia mbaya nawe, anaweza kwenda kwenye mitandao, na kuomba location yako, atapewa; akitaka kujua una mahusiano na mtu gani, atapewa; akitaka kujua simu yako ilituma hela kwa nani na ina balance kiasi gani, anapewa; atapewa chochote anachotaka alimradi tu ni polisi.

Hii ni wakeup call, kuwa usitumie mitandao ya simu kama siyo lazima sana. Labda utumie zaidi data ili mawasiliano yawe kwa whatsap, skype au telegram, huduma ambazo savers hazipo nchini, lakini siyo sms wala calls, au kutuma hela.
kama wewe sio Gaidi unaogopa nini??!!
 
Hata mimi nimeshangazwa sana. Kwa wenzetu, ni lazima kuwepo na amri ya mahakama. Yani uchunguzi umefikia mahali ambapo mahakama inaona ni sahihi taarifa hizo zikatolewa. Lakini hapa kwetu ni polisi tu akiamua anapewa hizo taarifa. What a stupid country.
 
kama wewe sio Gaidi unaogopa nini?
magaidi ndio watakao ogopa maana wana tumia vibaya mawasiliano.
 
Aiseee pole kama ndiyo unajua leo,wengi kuongea mambo ya siri/Madili wanatumia whatsapp call au Facebook call.....Mwendazake alienda mbali hadi kurekodi maongezi na kusoma meseji za watu aliowatarget.
 
Sheria inasema taarifa inaweza kutolewa kama mtumiaji wa simu anatuhumiwa kutenda kosa fulani. Lakini uthibitisho uliotolewa leo ni kwamba polisi hawaelezi hata sababu, na tigo hata hawaulizi taarifa inahitajika kwa sababu gani.
Kaka km unacho kile kielelezo cha barua kutoka polisi kwenda tigo tuwekee km hawakutoa sababu maana wakili wa utetezi alisema visisomwe ila aongozwe tu kwa kuwa vitachukua muda mrefu
 
Sheria inasema taarifa inaweza kutolewa kama mtumiaji wa simu anatuhumiwa kutenda kosa fulani. Lakini uthibitisho uliotolewa leo ni kwamba polisi hawaelezi hata sababu, na tigo hata hawaulizi taarifa inahitajika kwa sababu gani.
Hili ndio tatizo na weakness ya huyo shahidi aliodhihirisha leo mahakamani. Pili alipaswa ashirikishe uongozi wa kampuni katika kudisclose customer's infos.
Labda aliwekwa TIGO na mfumo kwa kazi maalumu who knows.?
 
Shahidi wa leo, kwenye kesi dhidi ya Mh. Mbowe na wenzake, bwana Fredy ametudhihirishia wateja wa mitandao ya simu kuwa polisi wanaweza kwenda kwenye hii mitandao na kuwaambia wenye mitandao wawape taarifa zako zote, kama mawasiliano, ulipo, miamala yako, wao hata hawaulizi ni kwaajili ya nini, wanawapa.

Watanzania hatupo salama kiusalama wala kifaragha, kila unapotumia mtandao wa simu. Polisi mwenye nia mbaya nawe, anaweza kwenda kwenye mitandao, na kuomba location yako, atapewa; akitaka kujua una mahusiano na mtu gani, atapewa; akitaka kujua simu yako ilituma hela kwa nani na ina balance kiasi gani, anapewa; atapewa chochote anachotaka alimradi tu ni polisi.

Hii ni wakeup call, kuwa usitumie mitandao ya simu kama siyo lazima sana. Labda utumie zaidi data ili mawasiliano yawe kwa whatsap, skype au telegram, huduma ambazo savers hazipo nchini, lakini siyo sms wala calls, au kutuma hela.
TIGO WAMEPELEKA MTU FAMBA, AMEHARIBU IMAGE YA TIGO.....TIGO MLIPENI CHEQUE YAKE AONDOKE....AMECHAFUA
 
Shaidi ambaye ni wakili katika kesi ya Mbowe kwa jina la Frank Kapara ameeleza kwa mlolongo mrefu uzoefu na utendaji wa kazi yake katika kampuni ya Tigo. Pia ameeleza jinsi gani anavyotoa taarifa za wateja kwa vyombo vingine pale anapohitajika kufanya hivyo. Maelezo yake anaonyesha ni rahisi sana kwa taarifa za wateja kutoka kampuni za simh kutolewa kwa vyombo kama polisi zinapotakiwa jambo ambalo si afya ksa faragha ya mawasiliano kwa wateja. Hali hiyo inaweza kuwa hivyo pia kwa mabenki.

Tatizo la upatikanaji kwa urahisi taarifa za wateja iwe kwenye mawasiliano, benki, hospitali au sehemu nyingine ni taarifa hizo kuweza kutumiwa vibaya na watu wenye nia ovu. Lakini pia kila binadamu anapenda na kuhusudu faragha. Hii ndio sababu imezifanya nchi nyingi zilizoendelea na kustaarabika kuweka sheria kali za kulinda siri za wateja hata za kawaida tu.

Pia duniani kuna ncho zinazotambulia kama nchi nzuri zaidi za watu kuhifadhi fedha zao na zimevutia watu wengi kutoka kila kona ya dunia kuhifadhi fedha zao. Nchi hizo ni pamoja na Panama, Cayman, Switzerland, Luxembourg, Seychelles,Singapore, Belize Ujerumani n.k. Sifa kuu katika nchi hizi ni utunzaji wa siri za wateja wao. Sifa hii imefanya nchi hizi kuwa na ukwasi mkubwa wa kifedha kwa njia ya mitaji inayotumika kuziendeleza. Ili upate taarifa za mteja katika nchi hizi ni lazima usote sana mahakamani na majaji wajiridhishe kwamba kweli kuna ulazima huo jambo ambalo huwa nadra sana majaji kukubali.

Kesi ya Mbowe inayoendelea iliamshe bunge kama mhimili na chombo cha kutunga sheria, kuweka sheria madhubuti za upatikanji taarifa za wateja katika simu, mabenki, hospitali na huduma nyingine. Hii itasaidia sana pia kuvutuia uwekezaji kutoka nje.
Hao watu (mamlaka) wanaopewa taarifa ni kwa mujibu wa sheria zilizopo.
Kuna mamlaka hazinyimwi hizo taarifa
sheria zipo zinazi guide hivyo vitu
 
Police ni chambo cha usalama na kudai taarifa za mtuhumiwa yeyote au mtu anayepelelezwa ni sawa kabisa ...achani ushabiki wa kisiasa..maana ya usalama nini sasa..kwa hiyo wasipewe huo uwezo ili nchi itekwe mara moja..achani ushabiki na ujinga..kwa hiyo police wakatufute order mahakani ili process ya kubaini wahalifu mara moja liwe complicated..acheni ushabiki
Hao unadhani wanajielewa basi
 
Hiyo yote ilikuwa ni master mind ya utawala wa Magufuli. Chini ya utawala wake haki ya kikatiba ya faragha Ni moja ya Sheria zilizovunjwa sana. Wahanga Ni wengi, Kama Membe, Makambas, Nape, Kinana, Mawaziri wote, wakuu wa mikoa, Wilaya nakadhalika.

Ninachojua faragha ya mtu inaweza kuingiliwa kwa Amri ya Mahakama. Kilichofanyika Chini ya Magufuli Ni uharamia na ubakaji wa Hali ya juu wa matakwa ya katiba.

Na Kuna uwezekano hata hacking ilifanyika Sana kwenye anuani za watu. Hii kesi itatupa mengi, Tuendelee kufuatilia. Lakini at least tumeshaona jinsi MITANDAO hii ya simu, Voda(kipindi Cha kina Membe) na Tigo ilivyo fragile and weak kutunza faragha za wateja wao.

Ni JAMIIFORUMS pekee, so far, ndio walioonesha ukomavu, uelewa na ufahamu katika kutetea faragha ya wateja wao. Heko Maxi Mello.

ni upuuzi kiwango 1000% kudhani kwamba mtandao utaheshimu faragha za mjinga mmoja dhidi ya serikali,hakuna nchi ya hivi,haipo.
zipo policy kati yako,mtandao,na serikali kama utatu mtakatifu katika biashara,lakini kuna policy kati ya mtandao na serikali.

wewe mkuu ukiua,ukahitajika ushahidi kutoka katika simu,polisi ambao ni sehemu ya serikali wana mamlaka ya kwenda tigo au kwingine wakapewa mkeka wote wa mawasiliano yako,na huwezi kuja hapa unalalamikia faragha kwamba umesalitiwa na mtandao husika,maana utaonekana kichaa.

hao wahanga unaojaribu kuwataja ni kundi hili hili la kwako wanaoamini kutumia mitandao kuna ngao sababu ya sera ya faragha kutoka mtandao husika,unapiga majungu mkuu wa nchi kwenye simu[emoji1787][emoji23][emoji1787].

melo mwenyewe labda sababu hawezi kukwambia kakabidhi nini kwa kazi zipi,ndio maana unaandika hapa,vinginevyo angeeshakula ban saa hizi usijue hata jf iliishakuwepo.
 
Kwa mwenendo wa kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA freeman Mbowe na ushahidi na mashahidi wanaojitokeza kuna vilio vitakuja baadae.

Shahidi namba 05 wa leo ama kwa kujua ama kutokujua au kwa kushinikizwa unaona kabisa ameitumbukiza shimoni TIGO na MIC.

Huyu Shahidi wa TIgo anaonesha kabisa kuwa hajui ama alifanya kwa kufuata maelekezo. Kuna sehemu anasema wao mtu yeyote akipata barua toka Polisi kuhusu kuchunguzwa kwa mtu hawaangalii chochote.

Hapa anabanwa na sheria ya faragha. Mbowe anapiga hela hapa. Hata kama Mbowe atafungwa kwa case atakayofungua dhidi ya TIGO ana uhakika wa familia yake kuishi kwa raha.

TIGO wamejiingiza katika mgogoro mkubwa na watumiaji wengine. Wasijione wapo bora waulize gazeti kongwe duniani lilivyofutika katika uso wa dunia.

Mwanasheria wa TIGO kama mlinda siri wa Wateja.

Hii kesi inaleta mengi.

mambo hayako namna hiyo.

amri ya mahakama haiko mitandaoni huko,kasome sheria mpya ya uhalifu wa mtandao.
watu walilalamika mamlaka kushushwa chini mpaka kwa wakuu wa vituo tu.
 
mambo hayako namna hiyo.

amri ya mahakama haiko mitandaoni huko,kasome sheria mpya ya uhalifu wa mtandao.
watu walilalamika mamlaka kushushwa chini mpaka kwa wakuu wa vituo tu.
Haujui kitu fanya uchambuzi wa kina utajua
 
kama wewe sio Gaidi unaogopa nini?
magaidi ndio watakao ogopa maana wana tumia vibaya mawasiliano.
Faragha ya mtu siyo uhalifu tu. Au kwako, hata serikali au kampuni wakisema hii ni confidential au classified information, basi ni ugaidi?
 
Makampuni mengi ya simu yana bahati ya kufanya kazi katika nchi zenye watu wengi wajinga ila ingekuwa kwenye nchi zilizoendelea leo tigo hisa zao zingeshuka tu kumbe kwao suala la privacy siyo kipaumbele chao kbsa kwa mteja wao shame on them
 
Kuna sehemu anasema wao mtu yeyote akipata barua toka Polisi kuhusu kuchunguzwa kwa mtu hawaangalii chochote.
Hii tunaita ufanyaji wa kazi wa mazoea. Bila kuzingatia kanuni na Taratibu za kampuni yao zilizopo.
 
Back
Top Bottom