Kesi ya Mbowe na wenzake inaanika hadi 'mambo ya siri za nchi'. DPP hujachelewa kuifuta

Kesi ya Mbowe na wenzake inaanika hadi 'mambo ya siri za nchi'. DPP hujachelewa kuifuta

Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu mkubwa mwenendo wa kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na wenzake watatu. Nafuatilia kwa kwenda mwenyewe Mahakamani. Hata sasa nipo Viunga vya Law School of Tanzania ilipo Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi kwa ajili ya kuhudhuria kesi ya akina Mbowe. Sitaki kupitwa wala kusimuliwa. Najionea na kusikia mwenyewe moja kwa moja.

Yanayozungumzwa Mahakamani hapa yanashtua, yanaogofya na kuanika hata visivyofaa kuanikwa. Wengi wanaofuatilia wanajua kuwa kesi hiyo sasa imezaa kesi ndogo. Kesi ndogo ni imezaliwa baada ya Maelezo ya Mshtakiwa wa pili (Adamoo) kupingwa na upande wa Utetezi Mahakamani hapa. Ndipo Jaji Siyani anayeisikiliza kesi kuu alipotoa amri ya kuendeshwa kesi ndogo ndani ya kesi kuu kuhusu pingamizi hilo.

Mwisho wa kesi ndogo inayoendelea kutolewa ushahidi sasa ni kukubaliwa au kukataliwa kupokelewa kwa maelezo ya Adamoo yanayodaiwa aliyatoa huko Polisi alipokamatwa na kuhojiwa/kuchukuliwa maelezo. Yeye mwenyewe Adamoo kwenye ushahidi wake ameyakana Maelezo hayo akisema aliletewa yakiwa yameshaandikwa na kusainishwa chini ya vitisho vikubwa vya polisi (ACP Kingai). Jana shahidi wa pili (Bwana Ling'wenya) alianza kutoa ushahidi wake na anaendelea leo hii.

Kuna mambo yameshasemwa hapa Mahakamani na mashahidi wa Utetezi yanaogofya sana. Kwanza, kuna idadi kubwa ya wanajeshi wamekamatwa na wanateswa kwenye vituo vya polisi. Kuna nini na kumetokea nini jeshini huko hadi kufikia hapo? Pili, aliyetajwa na ACP Kingai kama mtoa taarifa za uhalifu wa Mbowe na wenzake (Luteni Urio) naye alishakamatwa na kuteswa na polisi. Je, aliteswa ili 'amchome' Mbowe na wenzake?

Kuna jambo linaogofya zaidi. Ushahidi wa kwamba wanajeshi wanakamatwa na kuteswa na polisi waweza kupika chuki na hasira kwenye mioyo ya wawili hao na kuzua suitafahamu ambayo itashindikana hata kusemeka huko mbeleni. Yaani, kunaweza kukachemka 'bifu' kati ya wapambanaji hao. Ikifika hapo, hali itakuwa tete. DPP, hujachelewa kuzuia kuvuja zaidi mambo ya ndani kuliko maini ya nchi na kuzuia taharuki isiyo na hata mkuki.

Buriani Ole Nasha!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Kwenye katiba mpya tuongezee hili:

"Mambo ya siri za serikali dhidi yetu hatuyataki."

Kuendeleza haya ya siri za Baraza la mawaziri ndiyo yaliyotufikisha huku.

Hivi serikali kama ni yetu inakuwa je na siri dhidi yetu?

Simon Sirro:

"Tunawataka Moses Lijenje na Luteni Urio wakiwa hai kutokea mikononi mwako."

Vivyo hivyo itatupa Ben Azory Mawazo na utatwambia waliaomuru, kuratibu na kutekeleza shambulizi la Lissu.
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu mkubwa mwenendo wa kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na wenzake watatu. Nafuatilia kwa kwenda mwenyewe Mahakamani. Hata sasa nipo Viunga vya Law School of Tanzania ilipo Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi kwa ajili ya kuhudhuria kesi ya akina Mbowe. Sitaki kupitwa wala kusimuliwa. Najionea na kusikia mwenyewe moja kwa moja.

Yanayozungumzwa Mahakamani hapa yanashtua, yanaogofya na kuanika hata visivyofaa kuanikwa. Wengi wanaofuatilia wanajua kuwa kesi hiyo sasa imezaa kesi ndogo. Kesi ndogo ni imezaliwa baada ya Maelezo ya Mshtakiwa wa pili (Adamoo) kupingwa na upande wa Utetezi Mahakamani hapa. Ndipo Jaji Siyani anayeisikiliza kesi kuu alipotoa amri ya kuendeshwa kesi ndogo ndani ya kesi kuu kuhusu pingamizi hilo.

Mwisho wa kesi ndogo inayoendelea kutolewa ushahidi sasa ni kukubaliwa au kukataliwa kupokelewa kwa maelezo ya Adamoo yanayodaiwa aliyatoa huko Polisi alipokamatwa na kuhojiwa/kuchukuliwa maelezo. Yeye mwenyewe Adamoo kwenye ushahidi wake ameyakana Maelezo hayo akisema aliletewa yakiwa yameshaandikwa na kusainishwa chini ya vitisho vikubwa vya polisi (ACP Kingai). Jana shahidi wa pili (Bwana Ling'wenya) alianza kutoa ushahidi wake na anaendelea leo hii.

Kuna mambo yameshasemwa hapa Mahakamani na mashahidi wa Utetezi yanaogofya sana. Kwanza, kuna idadi kubwa ya wanajeshi wamekamatwa na wanateswa kwenye vituo vya polisi. Kuna nini na kumetokea nini jeshini huko hadi kufikia hapo? Pili, aliyetajwa na ACP Kingai kama mtoa taarifa za uhalifu wa Mbowe na wenzake (Luteni Urio) naye alishakamatwa na kuteswa na polisi. Je, aliteswa ili 'amchome' Mbowe na wenzake?

Kuna jambo linaogofya zaidi. Ushahidi wa kwamba wanajeshi wanakamatwa na kuteswa na polisi waweza kupika chuki na hasira kwenye mioyo ya wawili hao na kuzua suitafahamu ambayo itashindikana hata kusemeka huko mbeleni. Yaani, kunaweza kukachemka 'bifu' kati ya wapambanaji hao. Ikifika hapo, hali itakuwa tete. DPP, hujachelewa kuzuia kuvuja zaidi mambo ya ndani kuliko maini ya nchi na kuzuia taharuki isiyo na hata mkuki.

Buriani Ole Nasha!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Ngoja inyeshe tujue panapovuja. Kumbe polisi wamepewa madaraka mpaka ya kutesa makomandoo wa JWTZ ? Wallahi sikujua...
 
Kwenye hili suala la kuwepo wanajeshi vituo vya polisi hata mimi limenistua,na huyo shahidi anasema hao wenzie nao walikamatwa kwa kesi hizo hizo za ugaidi,kulitokea nini huko jeshini?!

Yule shahidi anasema aliona Luteni Urio akiteswa na wanajeshi wa special forces(aliokuwa nao kambi moja so anawajua) pamoja na polisi kwenye magari mabovu pale Tazara police.
Na mimi nimeamini kabisa ushahidi huu maana sidhani kama wanajeshi wangeweza kukamatwa na kushughulikiwa bila kuhusisha wajeda wenzao.Sasa nini kilitokea huko jeshini?
Kuna nini pia kwa wanaostaafu huko jeshini?

Pili,ni kwanini kesi hii imeachwa wazi hivi huku inaonekana kama inakwenda kureveal vitu vizito dhidi ya serikali ambavyo si busara kuviweka hadharani?
Naamini kabisa tiss wangetaka iwe kimya kimya wasingeshindwa kwa mvua kwa jua na hii kesi isingekuwepo kabisa in the first place,lazima ingefutwa kama ni Mbowe na Chadema wangetafuta namna nyingine ya kudeal nao.

Hii kesi naishangaa sana.
Kuna smokescreen gani hapa?!
 
Yaani DPP afute kesi kisha magaidi watoke nje waendelee na njama zao haramu za kupanga mikakati ya kuhatarisha Amani ya nchi yetu??!!
 
wenye akili zao hawewezi kuamini maneno ya uongo ya Ligwenya/ Adamoo, huyo ni mtuhumiwa wa Ugaidi anaye daiwa kumtumikia mtuhumiwa Mbowe.
kama walidhani wanaweza kupoteza amani yetu ya Tz basi wajue amani ya Tz lazima ilindwe kwa gharama yoyote ile.
Mbona wewe umeshahakikisha tayari wakati wote ni watuhumiwa?
 
Hili halina shida, ndio kiu
wenye akili zao hawewezi kuamini maneno ya uongo ya Ligwenya/ Adamoo, huyo ni mtuhumiwa wa Ugaidi anaye daiwa kumtumikia mtuhumiwa Mbowe.
kama walidhani wanaweza kupoteza amani yetu ya Tz basi wajue amani ya Tz lazima ilindwe kwa gharama yoyote ile.
Ila kwa huu ushahidi wa polisi kuna ndoto ya hiki unachokisema kutokea?
 
inawezekana kuna mambo ya ndani sana inapofika issue ya wanajeshi wengi kuhusishwa hata kuteswa kwenye vituo vya polisi...Hawa wanajeshi wanaingia kwenye kesi ya Mbowe, na kama kweli ni hivyo,Je Mbowe na jeshi uhusiano wao kwanini ulikuwa mkubwa kiasi hicho...

Simtetei yeyote hapa najaribu kuwaza kwa upana kidogo kulingana na mtoa mada hapo juu...
 
Hili halina shida, ndio kiu Ila kwa huu ushahidi wa polisi kuna ndoto ya hiki unachokisema kutokea?
Mimi sijui, Jamuhuri ndio inajua zaidi.
wewe endelea kusikiliza kesi mpaka mwisho wake.
sikiliza hadi shahidi wa mwisho.
hadi wa mwisho.
hadi wa mwisho.
hadi wa mwisho.
 
wenye akili zao hawewezi kuamini maneno ya uongo ya Ligwenya/ Adamoo, huyo ni mtuhumiwa wa Ugaidi anaye daiwa kumtumikia mtuhumiwa Mbowe.
kama walidhani wanaweza kupoteza amani yetu ya Tz basi wajue amani ya Tz lazima ilindwe kwa gharama yoyote ile.
Lingwenye na wenzake sasa wamebaki kutapatapa, maji ya shingo, watajuta kuchezea amani yetu.
kichwani zimo? wewe ni mjinga na una akili.
 
Mbona wewe umeshahakikisha tayari wakati wote ni watuhumiwa?
angalia vizuri juu ya comment nimesema mtuhumiwa/watuhumiwa.
bado ni watuhumiwa.
tuache kelele mingi, ngoma bado mbichi sana.
ndio kwanza trela picha lenyewe halijaaanza
 
inaonesha serikali hawakujua kibatala anaweza akachimba mashitaka na kupelekea uzalishaji wakesi ndogo ndani yakubwa
 
Kuna wakili yule wa serikali anaonekana ni jeuri na mtu wa majungu sana, kuna maswali alikuwa akimuuliza Adamo akitaka kujua yale ambayo yanafanyika kule DRC, kuna wakati anachonokoa kutaka kufahamu ni kwa jinsi gani Makomando wanavyofanya kazi.

DPP aingilie kati kuepuka haya kutokea maana tunapoelekea huko siri nyingi zitawekwa wazi, pia itatengeneza uhasama kati ya majeshi haya wawili jeshi la polisi na jeshi la wanannchi.

Swali langu? Hadi huyo luteni Urio kuteswa huko ni kwamba Jenerali Mabeyo hana taarifa na kinachoendelea kwa vijana wake, inasikitisha sana.
Na mara mara nyingi moto huanzia chini kupanda juu
 
Amani ya nchi yoyote ile hulindwa kama mboni ya jicho.
sasa ole wake ujaribu kuchezea amani ya nchi utajuta!!!
unaweza kuchezea kitambi chako au kidevu chako lkn kamwe usijaribu kuchezea AMNI ya Nchi.
 
Na wote waliokamatwa na kuteswa ni kj 92,special force (makomandoo tupu)
Kingai na Mahita hiiiiiiiiiiii!
Samahani. Jamani niulize hawa akina Adamoo, Lingwenye, na Moses WALIKUWA WANAJESHI au ni WANAJESHI. Kwa maana WALIFUKUZWA JESHINI au WAPO JESHINI HADI LEO?
 
Amani ya nchi yoyote ile hulindwa kama mboni ya jicho.
sasa ole wake ujaribu kuchezea amani ya nchi utajuta!!!
unaweza kuchezea kitambi chako au kidevu chako lkn kamwe usijaribu kuchezea AMNI ya Nchi.
Unapata tabu sana
 
Back
Top Bottom