Kesi ya Mbowe Serikali imeingia kwenye mtego huu iuepuke mapema

Kesi ya Mbowe Serikali imeingia kwenye mtego huu iuepuke mapema

Fundi Madirisha

Senior Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
184
Reaction score
988
Katika jambo kubwa ambalo nafikiri wengi hawaliongelei na hawataki kulielewa huenda labda ni makusudi waone kuna kitu gani mwishoni ni kuhusu mwenendo mzima wa kesi ya Ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe. Kuna mtego mwingine mkubwa kwenye hii kesi na watakaoumia zaidi ni CCM na serikali wanayoongoza. Kwa viongozi wenye kutazama mbali zaidi wangeachana na hii kesi, mwisho wake si mzuri.

Kiukweli kabisa majibu yeyote yale kwenye hukumu ya kesi hii hayataiacha CCM na serikali yake salama kisiasa, labda watolewe kafara watu wachache waliofungua hii kesi ili kuweka balance kwenye mitazamo ya Watanzania.

Maana Mbowe mpaka sasa kila mtanzania hata asiyependa anajua kua alikamatwa kwa sababu ya kongamano la kudai katiba mpya, kwahiyo hata akifungwa ni katiba mpya ndiyo itakayomfanya na siyo ugaidi maana mpaka sasa ushahidi unaotolewa mahakamani unajikanganya na hata hisia za ugaidi hakuna.

Kwahiyo, itaamka ari mpya ya watu kudai katiba mpya na hawataogopa wataona ni bora nao waende jela kama Mbowe, hili vuguvugu litawagawa sana watanzania na hawatazielewa mamlaka. wakifuta mashtaka watakaolaumiwa ni Polisi na serikali kwa ubambikiziaji kesi na itaonekana kwamba suala la katiba mpya ni la msingi ndiyo maana Wanawasumbua wapinzani, kwenye hili atakayepewa umaarufu ni Mbowe na chama chake.

Bado hata Mhe Mbowe akishinda kesi hii itaonekana ni ya uongo na kubambikiwa na kuamsha hasira za wananchi na kuichukia serikali yao. Kwa vyovyote vile matokeo yeyote ya maamuzi ya kesi hii si mazuri, huu mtego ni mbaya labda itafutwe namna nzuri ya kulimaliza bila kuathiri upande wowote. Sasa inaonekana kua taifa liko kwenye mgogoro wa kikatiba kwa sura ya nje na ndani.

Huu mtego kwa Mbowe anahangaishwa kwa sababu ya kudai katiba mpya ni kitu ambacho hakikuwepk tangu nchi hii ipate Uhuru, ngumu sana kuingia akilini kumshtaki kwa tuhuma za ugaidi mtu ambaye hana rekodi zozote za kushiriki mauaji au kitendo chochote cha utovu wa nidhamu. Kwanza ni dhambi mbele za Mungu Mola maana atashusha laana kwa watawala na wahusika wengine.

Kuna wanaodhani kuwa kesi ya Mbowe ingeweza kuzima vuguvugu la madai ya katiba mpya ambayo ina maslahi kwa watanzania wote lakini wamesahau kua kutajwa tajwa kwa hii kesi ndiyo kunachochea neno Katiba Mpya kutajwa sana maana ndivyo inavyo hukuliwa kua Mbowe ana kesi kwa sababu ya kudai katiba mpya na ugaidi juu yake ni vitu vya kufikirika.

Hii kesi ni mtego mkubwa sana kwenye uwajibikaji wa kusimamia shughuli za maendeleo nchini, suala la kisiasa halimalizwi kwa kumweka mtu jela, alikaa sana jela Rais Hichilema wa Zambia, kina Raila Odinga, kina Hayati Mandela kwa kesi za uongo na kutunga lakini walitoka.

Naishauri CCM na serikali watambue kua CHADEMA wana wanachama zaidi ya milioni 8 kwa takwimu zao, hii idadi si ndogo wapime madhara yanayoweza kuwakumba baadaye.
 
CCM inaungwa mkono na watu wajinga - TWAWEZA.

WanaCCM wengi, hata waliomo humu JF, kwa kiasi kikubwa ni watu wenye akili ndogo, ambao uwezo wao wa kuona mambo unaishia siku moja, mwenye akili kidogo, hazidi zaidi ya mwaka.

Mleta mada umeileta hii kwa kufikiria hata huko CCM kuna watu ambao ni analytical thinkers, wakati ukweli CCM imejaa watu ambao ni low IQ, wenye akili wana unafiki mkubwa. Hakuna mtu ambaye ni super intelligent mwenye free thinking capacity ambaye yupo CCM kwa sasa. Hawa wa sasa hawawezi kuelewa chochote, mpaka siku hiyo ifike.
 
HAKUKAMATWA KWA SABABU YA KONGAMANO LA KATIBA ONDOA UPOTOSHAJI

Mbowe na wenzake walikamatwa kwa sababu ya kongamano la katiba. Wakiwa mahabusu, wakaanza kuwatafutia mashtaka kwa sababu walijua la kudai katiba, siyo kosa.

Labda uwe na upum.bavu uliopindukia ndiyo unaweza kuwaamini hao wendawazimu walimbambikizia Mbowe kesi ya ugaidi, tena kwa namna ya ujinga wa hali ya juu.

Mwenye akili, akiamua kudanganya, uwongo anauweka kwa namna ambayo inaweza kufanana na ukweli. Lakini uwongo wa mwendawazimu, kama huu, kila mmoja, hata mwenye akili kidogo, anajua kuwa ni kesi ya kubambikiziwa.
 
Mbowe na wenzake walikatwa kwa sababu ya kongamano la katiba. Wakiwa mahabusu, wakaanza kuwatafutia mashtaka kwa sababu walijua la kudai katiba, siyo kosa.

Labda uwe na upum.bavu uliopindukia ndiyo unaweza kuwaamini hao wendawazimu walimbamkbikizia Mbowe kesi ya ugaifi, tena kwa namna ya ujinga wa hali ya juu.

Mwenye akili, akiamua kudanganya, uwongo anauweka kwa namna ambayo inaweza kufanana na ukweli. Lakini uwongo wa mwendawazimu, kama huu, kila mmoja, hata mwenye akili kidogo, anajua kuwa ni kesi ya kubambikiziwa.
Wakati akiendelea naharakati za katiba mwanza alikuwa na kesi mahakamani,na wenzake walikuwa wameshakamatwa kitambo,aliyebakia alikuwa ni yeye pekee,na hakuwa amekamatwa kwa sababu alikuwa Dubai,hivyo alivyokuja tu akajificha haraka katika mwavuli wa katiba mpya.ili ndio iwe KINGA yake!( YThe man are so intelligent)
 
Katika jambo kubwa ambalo nafikiri wengi hawaliongelei na hawataki kulielewa huenda labda ni makusudi waone kuna kitu gani mwishoni ni kuhusu mwenendo mzima wa kesi ya Ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe. Kuna mtego mwingine mkubwa kwenye hii kesi na watakaoumia zaidi ni CCM na serikali wanayoongoza. Kwa viongozi wenye kutazama mbali zaidi wangeachana na hii kesi, mwisho wake si mzuri.
Kuna uhusuano gani kati ya Sabaya / katiba mpya na Mbowe?
 
CCM inaungwa mkono na waru wajinga - TWAWEZA.

WanaCCM wengi, hata waliomo humu JF, kwa kiasi kikubwa ni watu wenye akili ndogo, ambao uwezo wao wa kuona mambo unaishia siku moja, mwenye akili kidogo, hazidi zaidi ya mwaka.

Mleta mada umeileta hii kwa kufikiria hata huko CCM kuna watu ambao ni analytical thinkers, wakati ukweli CCM imejaa watu ambao ni low IQ, wenye akili wana unafiki mkubwa. Hakina mtu ambaye ni super intlligent mwenye free thinking capacity ambaye yupo CCM kwa sasa. Hawa wa sasa hawawezi kuelewa chochote, mpaka siku hiyo ifike.
Hata majina yao tu humu ni ushahidi tosha wa hiki ulichokisema! Mfano mtu na akili zake anajiita jingalao 🤔 Magonjwa Mtambuka 🤔, Bia yetu 🤔............!

Orodha ni ndefu kweli kweli!
 
Wakati akiendelea naharakati za katiba mwanza alikuwa na kesi mahakamani,na wenzake walikuwa wameshakamatwa kitambo,aliyebakia alikuwa ni yeye pekee,na hakuwa amekamatwa kwa sababu alikuwa Dubai,hivyo alivyokuja tu akajificha haraka katika mwavuli wa katiba mpya.ili ndio iwe kiongozi.( The man are so intelligent)
Kwa mujibu wa taarifa ya (polisi) mkamataji
 
Wakati akiendelea naharakati za katiba mwanza alikuwa na kesi mahakamani,na wenzake walikuwa wameshakamatwa kitambo,aliyebakia alikuwa ni yeye pekee,na hakuwa amekamatwa kwa sababu alikuwa Dubai,hivyo alivyokuja tu akajificha haraka katika mwavuli wa katiba mpya.ili ndio iwe kiongozi.( The man are so intelligent)
Kwani aliondokea wapi kwenda Dubai? Na aliporudi kutoka Dubai ndege yake ilitua Mwanza moja kwa moja?
 
Labda kama huo ugaidi aliufanya baada ya magu kufa SAwa lakini kama ni kabla isingekuwa rahisi sana kwa magu kumuacha kirahisi eti kusubiria ushahidi ukamilike kwanza in kingai voice,magu ilikuwa ushahidi utausubiria ukiwa ndani.
 
Kumbuka hakuwepo Tanzania kwa kipindi kirefu tu.toka wale wenzake wakamatwe
Alikaa zaidi ya mwaka? Point yangu ni kwamba wakati anaondoka kwenda Dubai alikuwa bado hajatuhumiwa ugaidi? Maana kama mpangaji wa ugaidi anaruhusiwa kuzurura wakati wenzake wameshakamatwa huoni hapo kuna walakini?
 
tafsiri nyingine ni kuwa Kama Mbowe hakufungwa kwa sababu ya katiba Mpya then kudai katiba Mpya sio kosa.
 
Wakati akiendelea naharakati za katiba mwanza alikuwa na kesi mahakamani,na wenzake walikuwa wameshakamatwa kitambo,aliyebakia alikuwa ni yeye pekee,na hakuwa amekamatwa kwa sababu alikuwa Dubai,hivyo alivyokuja tu akajificha haraka katika mwavuli wa katiba mpya.ili ndio iwe kiongozi.( The man are so intelligent)
Sema hivi Mbowe alikuwa anatafutiwa kesi muda mrefu Sana. Uimala wa Mbowe na kuimalika kwa Chadema ni tishio kubwa sana kwa watawala na CCM.

Kama kweri alikuwa na kesi ya ugaidi mbona jamuhuri inaangaika sana kutoa ushaidi usiokuwa na Shaka mpaka sasa.

Ushaidi wa kingai ni kituko, ushaidi wa power kaaya ni ujinga na ushaidi wa koplo Abdallah ni upuuzi mtupu, badala ya Kuja kuonyesha umiliki wa siraha na ndio kitu Kikubwa ktk kesi hii, yeye amekuja na ngonjera yamavipimo ya kijinga kijinga
 
CCM inaungwa mkono na waru wajinga - TWAWEZA.

WanaCCM wengi, hata waliomo humu JF, kwa kiasi kikubwa ni watu wenye akili ndogo, ambao uwezo wao wa kuona mambo unaishia siku moja, mwenye akili kidogo, hazidi zaidi ya mwaka.

Mleta mada umeileta hii kwa kufikiria hata huko CCM kuna watu ambao ni analytical thinkers, wakati ukweli CCM imejaa watu ambao ni low IQ, wenye akili wana unafiki mkubwa. Hakina mtu ambaye ni super intlligent mwenye free thinking capacity ambaye yupo CCM kwa sasa. Hawa wa sasa hawawezi kuelewa chochote, mpaka siku hiyo ifike.
Sio waru na wewe kamanda njaa sema watu
 
Back
Top Bottom