Kesi ya mjane wa bilionea Msuya: Jinsi alivyojibu tuhuma za kumuua wifi yake

Kesi ya mjane wa bilionea Msuya: Jinsi alivyojibu tuhuma za kumuua wifi yake

JE, MUNGU YUKO UPANDE GANI KATIKA KESI YA MJANE WA BILIONEA MSUYA?

Mahakama Kuu imemuachia huru mjane wa Bilionea Msuya katika kesi ya mauaji iliyokuwa ikimkabili. Kwa upande wake, Mahakama Kuu imetenda haki. Lakini dada wa Bilionea Msuya na yeye ameibuka na kuilalamikia Mahakama Kuu kuwa haikutenda haki. Yeye anadai kuwa kabla ya hukumu hiyo, nyumba kule Upareni na Arusha zilikuwa zinapakwa rangi na wakisema kuwa atatoka kwa gharama yeyote ile.

Kama forensic investigation itafanyika kuhusu upakaji rangi wa nyumba na kama maneno yao yatakuwa yamerekodiwa na kuchunguzwa juu ya nani aliyeyasema inaweza kufubaza nguvu ya kimaadili ya hukumu hiyo kama kutakuwa na ukweli wowote? Je, watu waliokuwa wakisema maneno hayo walikuwa na maana gani kusema kuwa atatoka kwa gharama yeyote? Je, walijua kabla maudhui ya hukumu hiyo na ndio maana wakaanza kupaka rangi nyumba? Je, mawakili wa utetezi walijua kuwa hoja zao zilishinda na hata kabla ya jaji hajaanza kuiandika hukumu hiyo na wakaenda kuwaeleza ndugu wa mteja ndio maana wakaanza kupaka nyumba rangi?

Je, maneno ya dada huyo ni ya kupuuzwa? Je, kama yatapuuzwa wakati yameibua tuhuma nzito dhidi ya mahakama kwa kuihusianisha hukumu na mambo yaliyokuwa yakiendelea nje ya mahakama juu ya upakaji rangi wa nyumba kule Arusha na Upareni, taswira ya mahakama itakuwaje katika jamii?

Je, mahakama ina fursa ya kujitetea endapo watu wataituhumu nje ya mahakama kufuatia hukumu inazotoa? Ikitokea kuwa tuhuma hizo zina mashiko lakini walalamikaji wakaamua kutokukata rufaa kwa sababu mbalimbali kama kukosa imani na mahakama au kukosa fedha za kuendeshea kesi; mahakama inao ujasiri na uwezo wa kuamua kuipitia upya hukumu?

Je, maneno ya huyo dada yanaweza kuwaibua TAKUKURU kwenda Arusha na Upareni kwa ajili ya kuchunguza mazingira ya upakaji rangi hizo nyumba? Lakini kuna kosa gani kupaka rangi nyumba hata kama mhusika yu gerezani kama ndugu zake wanaweza? Lakini kuna kosa kwa ndugu wa mtuhumiwa kuamini kuwa mtu wao atatoka kwa gharama yeyote?

Je, kusema mtu atatoka kwa gharama ye yote ni kosa? Nini maana ya neno gharama ye yote? Je, dada wa Bilionea Msuya ndiye aliyekuwa ni mlalamikaji katika kesi hiyo au ni Jamhuri? Je, Jamhuri inaposhindwa katika kesi ya mauaji na ikaamua kuishia hapo, ndugu wa marehemu kama wao hawajaridhika watafanya nini?

Je, kuna mapungufu ye yote katika sheria zetu kwa kuacha dhamana ya kulalamika katika kesi ya mauaji mikononi mwa Jamhuri pekee bila ya familia au ndugu kuwa ni wadau pacha au hata walalamikaji wa moja kwa moja? Kama Mungu yuko upande wa wanaoonewa, unafikiri katika hili yuko upande gani? Je, yuko upande wa mke wa Bilionea Msuya au yuko katika upande wa dada wa Bilionea Msuya? Je kwa nini unafikiri hivyo? Unadhani haki haina gharama ye yote?
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 24 Februari 2024; 1:07 usiku
 
Hao wana roho mbaya yaani kuuwa kuiba kwa ajili ya mali ni dakika 1 ndio baba wa taifa aliusia wasipewe ikulu tutaangamia wamejazana pale BOT wamejimilikisha.
Yule alkuwa mshamba tu, ndo MAANA aliacha nchi nyeupe, watu wake wanavaa viraka.. aliwalisha UNGA wa njano.. MAHINDI chakula Cha mifugo alichoomba huko US. Angewasogeza karibu angeondoka kwa heshma kubwa sana.. alikuwa kuchonga meno
 
Yule alkuwa mshamba tu, ndo MAANA aliacha nchi nyeupe, watu wake wanavaa viraka.. aliwalisha UNGA wa njano.. MAHINDI chakula Cha mifugo alichoomba huko US. Angewasogeza karibu angeondoka kwa heshma kubwa sana.. alikuwa kuchonga meno
Mtoto wa juzi unamuongelea mtu ambaye wakati akiwa mtendaji mkuu wa serikali wewe hata hauna ufahamu. Hebu kuwa na heshima na adabu kwa waliotangulia mbele za haki.
 
Back
Top Bottom