Kesi inayomkabili mshtakiwa Derick Derick Junior, ambaye alionekana katika kipande cha picha jongefu (video) kilichosambazwa katika mitandao ya kijamii, akimshambulia mtu mwingine kwa mateke na kitako cha bastola, imepangwa kuanza kusikilizwa ushahidi Januari 21, 2025, katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni.
Pia Soma
- DOKEZO - √ - Masaki: Anayedaiwa kuwa Afisa Usalama (TISS) afanya vurugu, amjeruhi mwananchi
- Derick Derick Junior aliyemjeruhi mtu kwa Bastola (Club 1245) aachiwa kwa Dhamana
Tarehe hiyo ilipangwa jana Jumatano, Novemba 20, 2024 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Is-haq Kupa, wakati ilipoitwa kwa ajili ya usikilizwaji wa awali huku upande wa mashtaka ukieleza unatarajiwa kuwa na mashahidi 12 na kuwasilisha vielelezo kadhaa.
Derick (36), ambaye ni Ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), mkazi wa Salasala jijini Dar es Salaam anakabiliwa na mashtaka mawili, kujeruhi na kutembea na silaha hadharani kwa namna ya kuleta utisho, akidaiwa kutenda makosa hayo Oktoba 27, saa 12.30 asubuhi, eneo la Maaki katika Club ya 1,245, iliyopo wilayani Kinondoni.
Katika shtaka la kwanza, Anadaiwa katika shtaka la kwanza alimjeruhi usoni sehemu ya jicho na puani Julian Bujuru kwa kumpiga kwa kitako cha bastola.
MWANANCHI