goukun wadey
JF-Expert Member
- Apr 22, 2020
- 241
- 284
Morison akishindwa simba anapokwa point, Morison akishinda yanga anapokwa nini? Na Tff wanapokwa nini?Yanga hawakubaliani na hio kauli ya TFF ndo maana wakaenda kushtaki FIFA na CAS.... Yanga wanasema bado walikuwa na mkataba na Morisson....
Yanga akishinda, Simba watakuwa na kosa la kumchezesha mchezaji ambaye alikuwa na mkataba na timu nyingine
Kumuelewesha UTOPOLO ni kazi kubwa sana.Kwahiyo Yanga ni wajinga wale mpaka kupoteza muda na hii kesi ? Amini nakwambia,, Kuna jambo hapa
Kwanini asaini mkataba wa Simba ilhali bado ana mkataba na Yanga ?
Hawana budi, lazima wafate maagizo.... CAS ni kubwa kuliko TFF
Kumbe na chama cha mpira drc kilisema saini ilighushiwa? au mchezaji lalamikiwa alikuwa huru? au na wao walisema mkataba wa mchezaji unamapungufu hivyo yupo huru?Na ndio maana Tp mazembe baada ya kuona As vita wamechezesha mchezaji ambaye bado alikuwa na mkataba timu aliyotoka, moja moja walipeleka kesi yao kule CAS, na mwisho wa siku As vita kupokwa point za mechi alizocheza yule mchezaji na kuchukuliwa Ubingwa wao kabisa
Ni kweli kabisa case ni Yanga vs Morrison. Kwenye hii case Yanga akishinda huenda akafungua kesi nyingine dhidi ya Simba kwa kumchezesha mchezaji aliyekuwa na mkataba na Yanga ama dhidi ya TFF kwa kuruhusu mchezaji mwenye mkataba na Yanga akaichezee SimbaHivi hamsomi?case imeandikwa Yanga vs Morisson sasa simba anahusishwaje.
Mkuu umejuaje clip ipo CAS?[emoji2]. Ila ile clip ingefika kule ingetusaidia sana!We jamaa jipe moyo tu,nani alisema morison yuko huru,walichosema kuna karatasi haijasainiwa,sasa hiyo paper isiyosainiwa ndio ivunje mkataba,kwa taarifa yako Yanga wana hadi receipt salary ya mshahara aliyochukua morison kupitia mkataba ule alioukataa,na kama utakumbuka morison mwenyewe wakati yuko Yanga alitoa clip kama simba wanamrubuni na wamempa dola 5000 kama zawadi, lakini yeye bado ana mkataba Yanga,from nowhere baadae akaukataa ule mkataba,Yanga ilionewa na shinikizo lilitoka hadi kwa washabiki wa mikia walioko serikalini akiwemo bashite na wengineo kibao walimuhakikishia wao ndio kila kitu nchi hii iwe isiwe atachezea mikia,ile clip morison aliongea kiingereza fasaha na ile clip ipo cas,kitendo tu cha kuongea na mchezaji wa timu nyingine akiwa ndani ya mkataba ni kosa,nyie jiandaeni tu [emoji1787][emoji1787]
NdioKwa hiyo Yanga wanalilia ubingwa wa mezani kutoka CAS. [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kuna kitu kibaya kitatokea kwa soka ya Tanzania...Fisi akisubiri mkono wa binadamu udondoke wakati anatembea!! Namhurumia maana atasubiri sana!!
Hanspope ni Nani?! Ni Tff?Vipi kesi ikipinduka: Morrison mechi za awali wakati anatua Yanga hakua na mkataba itakuaje?
Maana Hanspop aliwahi kuligusia hilo kua Morisson kwenye usajili wa dirisha dogo alichelewa kusajiliwa na alicheza mechi ya kwanza dhidi ya Singida bila mkataba
Hivi katika mgogoro huu huyo Morrison ameichea Simba mechi ngapi za ligi? Kama ni mechi 15 kwa mfano na Kati ya hizo Simba ameshinda 10 in maana Simba atanyang'anywa point 30? Kama ni hivyo madhara yake katika msimamo wa ligi ni yapi?Yanga vs morison,ikithibitika morison mchezaji wa Yanga ni kwamba morison ni mchezajibwa Yanga aliekua anacheza simba kimakosa,automatically simba ilikua inamtumia mchezaji asie wa kwao
Mkuu acha ushabiki zungumzia uhalisia, hukumu haikusema Morrison yupo free ilitoka kwamba ana mkataba wenye mapungufu, angekua huru hata CAS wasinge hangaika na kesi ya kijinga hivyo kumbuka mpka case ipangwe kusiliza hua wana jilidhisha kama kuna hoja za msingi
Yanga akishinda jamaa zetu itabidi hata ubingwa wauteme,hapo ndio tutaona vita hapatakalika msimbazi zitapigwa ngumi hadharani wenyewe kwa wenyewe bonge la mtifuanona sijui manara wakati huo atakua wapi
Akili zenu na TFF hizi subir mana mkisema mwanzo hakuna kesi hapaAtapokonywa na nani?
Simba anahusika vipi kwenye kesi yenu?
TFF walithibitisha kuwa morrison yupo huru, na usajili wake ulikuwa halali sababu TFF walithibitisha kwamba yupo huru.
Hujui kuwa sheria hizo zinawalinda wachezaji kuendelea kucheza vilabu wavitakavyo wakati kesi zao zikiendelea?
Yanga hatoambulia chochote
Kama ndio hivyo ilitakiwa Simba wasubiri mpaka kesi ya CAS iishe ndio waanze kumchezesha Morison.Yanga hawakubaliani na hio kauli ya TFF ndo maana wakaenda kushtaki FIFA na CAS.... Yanga wanasema bado walikuwa na mkataba na Morisson....
Yanga akishinda, Simba watakuwa na kosa la kumchezesha mchezaji ambaye alikuwa na mkataba na timu nyingine
We kenua tu hapo kama hujui madhara ya hizi hukumuKwa hiyo Yanga wanalilia ubingwa wa mezani kutoka CAS. [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mkuu naweza kukubaliana na wewe. Unajua sisi Watanzania tuna tatizo la weledi.Na mapungufu ya mkataba sio jambo linaloweza kufanya mkataba usiwe halali, kwa mapungufu yaliyo kuwepo mkataba ulikuwa halali kabisa, na TFF wakasahau kwamba Yanga wanaweza kwenda kwenye mamlaka ya juu zaidi
Du Watanzania ni watu wa ajabu sana. Mwanzoni tuliaminishwa hakuna kesi ya Morison huko CAS. Sasa hivi tunabishania hukumu itakayotolewa.Weka link mkuu.