Sijasema CCM kuna demokrasia,ninachosea CHADEMA walitakiwa kuonyesha Demokrsia ya kweli.Ndo maana nasema hawana tofauti na CCM,tena nikaongenza bora hata CCM,CHADEMA ndo wanaharibu kabisa.Nyerere aliachia kura ziamue kati na Jakaya na Benjamin,ingawa Nyerere alimnadi Benjamin.Mtei yeye alichokifanya ni kumtoa kabisa Zitto kenye kugombea.Usijitoe akili dada mdogo hivi nafasi ya mwenyekiti wa CCM,hata iliyokuwa Tanu wenyeviti waligombea na nani leo hii Mangula yupo channel ten analalamika sana kuhusu waasi wa CCM wanaotaka kupora madaraka sasa demokrasia gani ya CCM unayoiota
Sijasema CCM kuna demokrasia,ninachosea CHADEMA walitakiwa kuonyesha Demokrsia ya kweli.Ndo maana nasema hawana tofauti na CCM,tena nikaongenza bora hata CCM,CHADEMA ndo wanaharibu kabisa.Nyerere aliachia kura ziamue kati na Jakaya na Benjamin,ingawa Nyerere alimnadi Benjamin.Mtei yeye alichokifanya ni kumtoa kabisa Zitto kenye kugombea.
Tatizo hujui sheria ndo maana unakimbilia kufungua thread mpya na kutumia maneno ya Mh. Tundu Lissu!!
Wewe mwenyewe umeandika kwa hisia bila kuwa na facts, halafu una washangaa waliofungua kesi!! Kweli Nyani haoni kundule.
Eti chama kinahubiri Demokrasia,wanamuita Zitto na kumzuia kugombea ueneyekiti.Kwa nini hawakusubiri wajumbe waamue?Sasa CHEDEMA ina tofauti gani na CCM?bora hata nyerere aliacha kura ziamue kati ya JK na Mkapa,Pamoja na kwamba yeye alimpenda Mkapa
lazima ukweli liwekwe wazi kwa maslai ya taifa na siyo kutishia watu kwa maslai ya watu waovu zito ajiondoe mwenyewe kwani imethibitika wazi anatiuwa na serekali ya ccm kuivuruga chadema na democrasia nchini kwani hata kesi inayoendelea mahakama aliyeidrafti ni jaji alitambulika kwa jina la makaranga na kuituma kwa wakili msando kupitia e-mail adress ili yeye akafungua kesi mahakamani kama alivyofanya na nyaraka hiyo ilishakatwa kwenye mawasiliano ya wakili msando na jaji makaranga je ni halali kwa jaji kumsaidia wakili kuandaa kesi wakati wao ndiyo waamuzi wa kesi zinazofunguliwa mahakamani na hii inaweza kuaribu maamuzi ya mahakama, kama baadhi ya majaji wanashriki kuleta vurungu ndani ya vyama ni makosa makubwa sana na aipaswi kuvumiliwa na wananchi wapenda democrasia aifai hata kidogo
Mchezaji wa simba sports club akihisi coacher hatampanga kwenye mechi anaweza kwenda mahakamani kuzuia mechi isichezwe kwasababu ya hisia kuwa hatapangwa na atapata loss kwa washabiki wake, na fedha ya mechi ya siku.
Jaji atasaidia wengi sana kwenye vyama vya siasa wana hisi vikao vikikaa hawawezi kutendewa haki. Itakuwaje kwenye kura za maoni ambapo kuna wengi huwa wanakatwa majina na vyama vyao, Je hukumu hii si italeta kasheshe kwenye utendaji wa kila siku wa vyama vya siasa, makampuni, na taasisi mbalimbali?
Kesi hii ni kesi ya kipuuzi kabisa kuwahi kufunguliwa kwenye uwanja wa sheria? Sioni ni jinsi gani Jaji wa mahakama kuu atatoa hukumu kwa hisia. Sheria ni pamoja na material evidence, huwezi kuwa na hisia ukashinda kesi.
Kesi hii hata kama ina mkono wa Ikulu labda jaji awe mwehu kabisa. Kweli unazuia kikao cha chama kisikae eti unahisi utafukuzwa chama? Unazuia usijadiliwa kwa hisia utanyang'anywa kadi? Ni vipi mahakama inazuia chama kisisimamie maadili na sheria, kanuni na kanuni zake. Je Ni lazima kuwa mwanachama wa chama fulani is it enforceable by law kuwepo kwenye siasa? Kweli hii ni sababu ya kwenda mahakamani? Kwanini usisubiri ufukuzwe ndio uende mahakamni.
Posho, mshahara, ajira ndio vinapiganiwa sasa. Wasiwasi wangu ni kuwa wakili wa ZZK amemwingiza ZZK choo cha kike bila ya zito kujijua. Ajira Hapa TZ ngumu, Zito katangaza dau kubwa wakili kasema twende mzigo. Ushauri wa kisheria haujazingatiwa zaidi ya panic na kukurupuka.
Naamini kesi hii itatupwa.
Kwa komenti hii tu, mtu makini atajua ni nini unatabiri kutokea, poleni sana.Mpaka hapa ilipo, Zitto kuzuwia tu leo Kamati Kuu isijadili kumfukuza uanachama ni ushindi mkubwa sana kwa Zitto. No matter Hakimu atoe uamuzi wowote ule mwingine, hata wa kuruhusu Kamati imjadili kumfukuza uanachama still ni ushindi kwa Zitto.
Siasa imeingiliwa na tamaa ya utajiri sio kutumikia watu. Uwezo wa kizazi cha sasa kuwa wavumilivu unapungua na kuondoa umakini. Hakuna kiongozi malaika na huwezi kukubaliana na kila mtu, ZZK, Msando, kinachowasumbua ni tamaa tu ya madaraka fedha, na utukufu.
Kwa komenti hii tu, mtu makini atajua ni nini unatabiri kutokea, poleni sana.
We mama acha kupoteza mantiki ya topic, umekubali sasa kuwa Tundu Antipas Mughwai Lissu hana mshindani katika ulingo wa sheria?Bado umeme Tanzania ni rahisi. Kama una hasira si uvumbuwe na wewe njia mbadala ya kuufanya uwe rahisi badala ya kulalamika.
We mama acha kupoteza mantiki ya topic, umekubali sasa kuwa Tundu Antipas Mughwai Lissu hana mshindani katika ulingo wa sheria?
hujitambui ama na wewe ni kondom, hoja ya Katiba ya Chama, Uchaguzi ndani ya Chama, Matumizi mabovu, kukopeshana fedha kinyemela, manunuzi yasiyozingatia sheria-mambo ambayo tunapigana na CCM kila siku-na kusafiri kwa ajili ya ngono ( ziara ya Slaa na Mshumbusi, Mbowe na viti maalum) bado unasema ZZK anatawaliwa na tamaa-au waraka fake ulikuwa wako nini-pole
Unaona eeeh! Kosa kubwa la zzk kutaka uenyekiti wakati wenye chama wamereserve cheo hicho kwa watu fulani. Sasa hiyo ndio demokrasia cdm? Katika zama hizi ni vigumu kuwa na chama kisichokua na makundi.... Kama mnabisha mtafukuzana hadi siku ya uchaguzi.Khaa!! Kweli hii kesi ni mauzauza tangu kuanza kwake hasa pale ZZK alipotaka kugombea nafasi ya Mkiti
Jana kamati kuu imesimamishwa kuongelea kumfukuza uanachama Zitto, leo uzi uleule mpaka Jumatatu. Mpaka sasa mshindi ni Zitto.
Huyo Tundu mpaka Rais kamponda kwa kubabia kwenye sheria tena mbele ya halaiki ya watu na mbele ya watazamaji wa TV mamilioni waliopo ndani na nje ya Tanzania wamejionea alivyopigwa madongo live. Na kimya, mpaka leo hajajibu, unajuwa kwanini? upigwe madongo na Mwenyekiti wa chama unachokipinga halafu ukae kimya? unajuwa kwanini?