Kevin Carter, Mwanahabari aliyejiua baada ya kupiga picha watoto waliokuwa wakifa kwa njaa sudan

najiuliza swali moja tu,HV kwann hakumchukua MTT? alikua anafikiria nn?
 
so sad! Basi na yeye nafsi ilimuuma ndo maana amejiua!
Baada ya habari kuifikia dunia kuwa yule mtoto aliliwa na yule Tai! Watu toka kote duniani wakaanza kumshutumu kuwa Tuzo na umaarufu wake aliupata kwa damu, na kwamba damu ya yule mtoto ipo mikononi mwake!
 
To be honestly hili tukio limenigusa sana japo lilitokea miaka kadhaa iliyopta. Ni dhahir nafs yake ilimuuma sana na ndo maana hakuona thaman ya ile tuzo wala uhai tena kwa kupoteza furaha maishan mwake.
 
najiuliza swali moja tu,HV kwann hakumchukua MTT? alikua anafikiria nn?
naweza nisiwe sahihi, ila huyu mpiga picha alizaliwa na kukulia afrika kusini ya enzi za ubaguzi sidhani kama alililelewa kuona thamani sawa ya binadamu wote, chukulia kwamba hiki kitoto kingekuwa kizungu naamini lazima angekibeba na hata kuanza kwa kukipa maji au maziwa kabla hajakifikisha kituoni. uzito wa dhambi YAKE ulimwingia kichwani pale dunia ilipohoji WHAT HAPPENED TO THE LITTLE GIRL. Gazeti la New York Times lilijitahidi kudanganya kuwa mtoto alifika kituoni lakini haikumsaidia Kevin
 
Mmmmh aisee alistahili kabsa kulAumiwa!!!na hta hicho kifo alistahili pia ni zaid ya ukatili alofanya,awekwe mahali panampofaa huko alipo mbavuuuukbsa!!!!!
 
Ki madili ya uwandishi huyu mpiga picha yuko sahihi kupiga picha hvyo ndivyo uwandishi unamtaka awe.
Ila hawa wa Tz wanopiga pic badala ya kusaidia ni kuingilia fani isiyo yao ya uandishia
 
Ki madili ya uwandishi huyu mpiga picha yuko sahihi kupiga picha hvyo ndivyo uwandishi unamtaka awe.
Ila hawa wa Tz wanopiga pic badala ya kusaidia ni kuingilia fani isiyo yao ya uandishia
Kwa hiyo haruhusiwi kutoa msaada wa uokozi?
 
Hii picha inanipandishaga hasira sana juu ya wazungu,ni bora alijiua mwenyewe kabla sijamkamata.
 
hii picha ilipigwa mwaka 1994 na mwandishi WA kimarekani aitwaye Kevin carter, huko sudani
Mwandishi huyu alivompiga picha huyu mtoto WA kike hakurudi nyuma kumsaidia na kumpeleka katika vituo vya misaada ya chakula.
Ijapo huyu mwandishi badae alikuja kupata tunzo katika picha hiyo miezi michache badae alijiua.
Moja ya sababu Ni lawama toka kwa watu kwamba kwanini hakumsaidia binti yule na kumwacha pale akifa na nja.

Tumsifu Yesu kristo
 
Baada ya habari kuifikia dunia kuwa yule mtoto aliliwa na yule Tai! Watu toka kote duniani wakaanza kumshutumu kuwa Tuzo na umaarufu wake aliupata kwa damu, na kwamba damu ya yule mtoto ipo mikononi mwake!
Maumivu makali sana haya
 
Kuna sehemu niliisoma hii habari, hakukua na maelezo yakua Kevin alimsaidia huyo mtoto baada ya kupiga picha
Ken alimfukuza Tai baada ya kupiga picha. Na mtoto aliishi miaka 14 zaidi. Alipona utapiamlo. Akafa kwa Homa. Jina la huyo mtoto ni long Nyong. Ken alietajwa kwenye uJumbe alouwacha ken ni mfanya kazi mwenzake aliefariki sio muda mrefu kipindi hicho. Ken oosterbroek
 
Jina la mtoto ni Kong Nyong*
 
She died already. Mpiga picha naye alipoona alipiga picha na kumuacha bila kumsaidia naye inasemekana alijiondoa duniani, maana ilizunguka sana na akaambia 'yule mtoto uliyempiga picha na kumuacha alikufa na kuliwa na tai' baada ya wewe kumuacha.
Hapana. Aliishi miaka 14 na hakuliwa na Tai. Na wala mpiga picha hakujiuwa kwa sababu ya huyo mtoto bali kwa sababu zake binafsi. Na Jina la mtoto lilikua Kong Nyong.
 
Not true. It was taken in Sudan. The child lived 14 years more and died of fever
 
Hakuna kazi ngumu kamakuwa mlinda amani au mpiga picha wa vitani..

utaona unyama wa kila aina ambao maishani mwako hukutegemea kama upo..
Ndio maana watu wanaoshuhudia hayo mambo Wanachanganyikiwaga,wanajiua maana hawawezi kuhimili walichoshuhudia... saikolojia yote inaharibika... ndio wajinyonga kwa kuandamwa na matukio mabaya waliyoona....

Mfano : Rwanda genocide walioshuhudia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…