Khadija Kopa: Kuna kuzaa na kunya, mtoto hata akiwa anacho kidogo anakuona

Khadija Kopa: Kuna kuzaa na kunya, mtoto hata akiwa anacho kidogo anakuona

Mama Salma kikwete
Mama dangote
Na hadija kopa

Hao wanawake kwenye kuongea kama unasikiliza redio basi unazima maana wanaongeaga vitu vya ajabu sana kuongea mbele za watu ni mtihani sana kwao.
 
Riziki inatoka kwa Mungu ila inapitia kwenye mikono ya binadamu kuja kwako. Haishuki kama mvua Bali inapita kwenye mikono ya watu, kumbe basi ISHI NA WATU VIZURI
 
Khadija kamsifia bint yake lakini komenti zinawaponda watoto wa kiume tu
 
Alipoulizwa na mtangazaji wa Global kuhusu Zuchu kumnunulia gari, Khadija Kopa alisema kuna kuzaa na kunya na yeye ni miongoni mwa watu walio zaa, maneno hayo yametafsiliwa tofauti na watu wameenda mbali zaidi wakidai bi Khadija amewatukana wanawake wenzake ambao wamezaa watoto lakini hawajawapa magari na pengine nyumba kuwa hawakuzaa bali walikunya na watoto hao ni mavi wanatakiwa watupwe.
Hii kauli naomba tumkumbushe na yeye


Nini maoni yako?

=========
Mtangazaji: Na hii gari nadhani ndio aliyokununulia Zuchu

Khadija Kopa: Eeeh, ndiyo

Mtangazaji: Hii ndio fahari ya mtoto, unalizungumziaje pia?

Khadija Kopa: Kuna kuzaa na kuna kunya, ukinya unatupa mavi yote yanaondoka, anaetaka mbolea pengine yamshinde kuyabeba lakini kuna kuzaa, mtoto hata akiwa anacho kidogo anakuona, sio lazima akupe gari lakini anacho kidogo anakuona sio lazima akupe gari lakini hata kidogo.

Kapata laki mbili basi ishirini ya mama, huko ndio kuzaa na nawaombea wazazi wenzangu wote mwenyezi Mungu awajaalie watoto wao wawe na imani na waweze kuwasaidia wazee wao na wazee wa wenzao InshaAllah.



Labda neno "kunya" alilotumia ndilo lenye ukakasi tu lakini mantiki ya alichokisema ni swadaqta.🤣
 
Kuna kuzaa na kuya?[emoji23] mbona hivi viwili vinatoka matundu tofauti sasa[emoji23]
 
Kuna kuzaa na kuya?[emoji23] mbona hivi viwili vinatoka matundu tofauti sasa[emoji23]


Na wewe umeanza sasa!!!, angalia usiwe wewe ndie utukanaye kwani tunaweza kusema yeye kaongea msemo kwamba kuna "kunya na kuzaa", kwani unasemaje juu ya methali/mseno wa "nyani haoni kundu lake??" 🤣--- je hilo ni tusi??
 
Namuunga mkono KHADIJA, wewe kama hujali mzazi wako kutwa kucha Kitambaa cheupe na milupo una faida gani kwa mzazi?
Kuna wazazi wengine hawakuwajali watoto wao yaani walipowazaa kwao ikawa habari kwisha, hakuna cha malezi wala support yeyote, hawa pia tunawaweka kwenye kundi gani?
 
Ujumbe mzuri tatizo lugha.
Huwa nawashangaa wanaotumia neno kunya kwenye audience ya watu au kwenye mahojiano. Neno kunya halina tafsida. Angetumia busara kutumia maneno kujisaidia haja kubwa badala ya kunya
 
Back
Top Bottom