Kheri James: Kumtukana Rais sasa basi

Kheri James: Kumtukana Rais sasa basi

Weka hapa list ya matusi aliyotukanwa rais wenu
Sikiliza hiyo video utaelewa kinachosemwa. Au kwako maana ya matusi ni yale ya nguoni? Kasome definition ya neno tusi kwenye kamusi. You can even just google. Hilo la nguoni wala siyo tusi.
 
Akina nani wanamtukana kiongozi wa malaika?
 
Mbona mgombea wenu anawatisha wananchi kwamba hawatajengewa barabara kama watachagua wagombea kutoka upinzani?
Hujui hata maana ya neno kutishwa. Mtu akikupa tahadhari wewe unaona umetishwa! Anakuambia usiende eneo fulani kwani huko kuna simba mla watu. Wewe kwa akili yako badala ya kumshukuru mtu huyo na kuzingatia tahadhari hiyo unamuona anakutisha! Kama si utahira ni kitu gani?
 
Huyo Rais katukanwa wapi? Na ametukanwa na nani? Nyie Mataga mmeishiwa hoja, mnatafuta chokochoko Chadema. Hapo lengo ni Chadema! Haooooooo tumewashtukia. Maana nashangaa na yule speaker anasema Lissu kamtusi yule mama.. lini Lissu alimtusi mtu (hasa yule mama)? Mbona mama katusiwa huko Twitter.. yule ni Lissu? Hawa Mataga vipi? Lissu anawachachafya sana aisee.

Hawa CCM Mpya wamebuni lugha na kamusi yao wanayoitumia mtaa wa Lumumba ambayo siyo Kiswahili.

Ndiyo maana kila neno la lugha ya kiswahili kwa kulinganisha na lugha yao ya mtaa wa Lumumba inatafsiriwa ni tusi katika lugha yao ya kiCCCM-Mpya.
 
Kuna mgombea moja anatoa lugha chafu ili aguswe akimbilie ubeligiji
Kawe Alumni , miaka yote UVCCM inakuwa na vijana werevu, wajibu hoja na wanaosaidia sana chama cha Mapinduzi, kuanzia akina Emmanuel Nchimbi, John Guninita, Nape Nnauye, Hussein Bashe, Masauni Yusuf na kadhalika, lakini sijaona kijana mpumbavu ambaye CCM imepata kuchagua kama huyu Heri James. Ni mpumbavu sana. Hakisaidii chama, zaidi ya kukiangamiza. Tangu amechaguliwa yeye ni kejeli na vitisho kwa wanaopishana naye kimawazo na mitazamo, hana constructive ideas kama hao niliowataja hapo juu. Ni shida sana. I am sorry to say that, lakini ndio mtazamo wangu.
 
Hujui hata maana ya neno kutishwa. Mtu akikupa tahadhari wewe unaona umetishwa! Anakuambia usiende eneo fulani kwani huko kuna simba mla watu. Wewe kwa akili yako badala ya kumshukuru mtu huyo na kuzingatia tahadhari hiyo unamuona anakutisha! Kama si utahira ni kitu gani?
Huna akili, acha kurukaruka kama maharage kikaangoni, orodhesha hayo matusi aliyotukanwa huyo kichaa!
 
Sijawahi kumsikia Mgombea wa Chadema akitukana zaidi ya kuelezea masuala na facts mbalimbali za yaliyofanywa na serikali ya awamu ya tano.Labda Mimi nitakuwa sijui matusi
 
Kwani huyo anayesema 'wakimugusa tu moto utakaowaka hamuna atakayeweza kuuzima' alikuwa anamtisha nani? Huyo anayesema 'mawakala wa chama chake watakapokuwa wanaenda kuapishwa kwa msimamizi wa uchaguzi wasindikizwe na umati wote uliohudhuria kwenye mkutano wake pale Ifakara' alikuwa anamtisha nani? Na kwamba umati wote huo utakapoenda kupiga kura hiyo tarehe 28 Oct 2020 ubaki hapo hapo kwenye kituo cha kupigia kura na kuhesabu kura hizo, alikuwa anamtisha nani? Na akasema maeneo yote nchi nzima wafanye hivyo, alikuwa anamtisha nani?

Arudi tu kwao Ubeligiji akapambane na covid 19, asituvurugie amani yetu. Tanzania ni kitovu cha amani Afrika.
Tuliza Munkari Mkuu, kwani hapo kuna shida gani? Tanzania ni kwake pia, hakuna mwenye hati miliki ya Tanzania. Kitovu cha amani tulikuwa tunaitambua hivyo nchi yetu lakini mpaka sasa hali iko hivyo? Mwanasiasa anapigwa risasi katika makazi ya viongozi wa kitaifa, mfanyabiashara wa kimataifa anatekwa karibu na makazi ya mawaziri na ofisi nyeti. Tuwe tu wa kweli kwa sasa hii sifa imepotea na inazidi kupotea kwa kasi kipindi hiki cha awamu ya 5
 
nanyi mshindeni kwa kuusema ukweli!
Hapo ndipo patamu. Ukweli wote utakaposemwa kuhusu yeye na chama chake hapatakalika. Siri zote za chama hicho zitakapowekwa hadharani itakuwa ni janga kubwa kwenye chama hicho. Sauti na video za waliopanga mashambulizi yake sept 2017 zikiwekwa hadharani itamlazimu asitishe hata hizo kampeni zake kwani ni watu alio nao karibu! Msitake tufike huko. Yaliyopita si ndwele tugange tu yajayo kwa ustaarabu na kuheshimiana. Tarehe 28 Okt 2020 yule wa kuchechemea ataendelea kuchechemea na yule wa kuzimiabataendelea tu kuzimia. Cha mhimu tujiepushe sote kuvuruga amani katika kipindi hichi cha silly season!
 
Wewe mpuuzi eti nawe unajiita Dr. Akili...huu udokta wenu huko CCM ni sawa na uhayawani! Kuna tusi zaidi ya kuwatishia raia wasio na hatia kwamba utawapiga wao, mama zao, shangazi zao na dada zao, huu si uhuni tu?

Hebu msikilize huyu mwingine anasema nini kuhusu kuwapelekea watu maendeleo...



Je wanaowakilishwa na wapinzani hawalipi kodi?
Mbona mgombea wenu anawatisha wananchi kwamba hawatajengewa barabara kama watachagua wagombea kutoka upinzani?
Shangazi zao na dada zao uwapige halafu kodi zao ukusanye lakini maendeleo uzuie huku wote ni Watanzania, kweli!​

huyu uvccm anahitaji msaada wa kisaikolojia
 
Tuliza Munkari Mkuu, kwani hapo kuna shida gani? Tanzania ni kwake pia, hakuna mwenye hati miliki ya Tanzania. Kitovu cha amani tulikuwa tunaitambua hivyo nchi yetu lakini mpaka sasa hali iko hivyo? Mwanasiasa anapigwa risasi katika makazi ya viongozo wa kitaifa, mfanyabiashara wa kimataifa anatekwa karibu na makazi ya mawazi na ofisi nyeti. Tuwe tu wa kweli kwa sasa hii sifa imepotea na inazidi kupotea kwa kasi kipindi hiki cha awamu ya 5
South Afrika ndiyo inaongoza kwenye matukio kama hayo kwa Afrika. Amerika inaongoza duniani kwa matukio ya aina hiyo. Sisi ni negligible. Kumbuka maendeleo ya nchi yanaambatana (direct propotional) na maongezeko ya uhalifu kama huo.
 
Back
Top Bottom