Khitma ya Saigon club ya Iddi Simba msikiti wa Mtoro

Kweli wewe umepata maradhi ya "kupenda kupigana bila kufikiri "!

Mie nakuonya kwa uandishi wangu wa aina yoyote ile, ili uache na ukome tabia ya kishetani ya kuchochea chuki ya kidini kwa kuchanganya uongo na ukweli!

Ukweli hata uwe mzuri vipi ukitia uongo kidogo kwa malengo ya kishetani ushaharibu. Inakuwa ni kitu cha hovyo tu kama maandishi yako hayo.

Hakuna mwenye akili timamu atakayekuona wa maana!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzizi...
Vitisho na lugha za "ukome" zinanisikitisha sana.

"Koma," ukimwambia mtu umemtukana.

Ikiwa unadhani nadanganya hebu wewe eleza ukweli.

Vitabu 12 na wachapaji mfano wa Oxford University Press Nairobi na New York na Minerva Press London ni wajinga kiasi kuchapa kazi zangu za uongo?

Basi ikiwa hivyo huyu Mohamed Said ni mtu mwenye akili sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kuweka kumbukumbu sawa, jaribu kuyaweka haya na mengineyo katika Vitabu.

Kuna mazito umeyazungumza kwa lugha nyepesi na ya kueleweka.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Salaam
Ustaadhi ningependa sana kukuona ukimsaidia Mzee Ali Hassan Mwinyi kuandika Historia yake, ingependeza sana,tena sana.
 
Mzee salaaam. Mie nimeifurahia sana makala hii. Basi ukijaaliwa siku ingine hebu tupatie na makala ya ndugu yetu Kigoma Malima enzi zile za vuguvugu la vyama vingi. Manake kwenye historia ya vyama vingi na siye mtu wa kuacha nyuma. Asante
 
Nilidhani anaelezewa Iddi Simba Marehemu kumbe Skyes... Huyu Sykes naanza ona alikuwa anawafanyia watu michezo ile mibaya maana sio kwa Kutajwa tajwa Huku kila issue hata zisizo mhusu...

Saigon ni kama ilishajifia siku nyingi tokea kijiwe kilipohama pale na kuhamia Nyumba ya Kina Hamisi Msukuma... Na Kumtukana na kumdharau Tarimo Mchaga mnywaji kama Laana iliwapata
 

Mlaleo,
Kuna historia nakuwekea hapa usome kisha tunaweza tukaendelea na mjadala:

Ndjabu...
Ondoa tu hayo matusi hayana maana lakini yote uliyoandika ni muhimu.
Obsession honestly...

Hakika kisa cha akina Sykes ni kisa mimi kimenikamata sana.

Achilia ule udugu lakini siku niliposoma kitabu, ''Modern Tanzanians,'' kitabu alichohariri John Iliffe na kusoma, ''The Townsman: The Life of Kleist Sykes,'' sura iliyoandikwa na mjukuu wa Kleist Sykes, Aisha ''Daisy'' Sykes Buruku historia hii ilikamata fikra zangu (Modern Tanzanians, (ed), East African Publishing House, Nairobi, 1973).

Nakumbuka kama vile jana nilikuwa katika Maktaba ya Taifa, Arusha ndipo nilipokikuta kitabu hiki.

Utafiti wangu wa kutaka kujua mengi ulianza siku ile.

Nikawauliza hawa ndugu zangu juu ya kitabu cha Iliffe.

Wakanifahamisha kuwa babu yao, Kleist Sykes kabla ya kufariki mwaka wa 1949 alikuwa ameandika ''kitabu,'' ambacho alimwachia mwanae Abdul Sykes.

Kwa hakika hakikuwa kitabu bali mswada wa kitabu.

Mwanae Abdu Sykes, Daisy alipoingia Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki mwaka wa 1967 kusoma Elimu na Historia ndipo alipokutana na John Iliffe na huyu mwalimu wake baada ya kufahamu historia ya akina Sykes na yeye kama mimi akakumbwa na hii ''obsession,'' akataka kujua mengi vipi walifika Tanganyika kutoka Afrika ya Kusini.

Hapo ndipo Daisy akawa anachukua nyaraka zilizokuwa katika familia na kumuonyesha Iliffe pamoja na mswada wa kitabu alichoandika babu yake.

Kutokana na nyaraka hizi Iliffe akaandika paper hii: '‘The Role of the African Association in the formation and Realisation of Territorial Conciousness in
Tanzania.’ Mimeo, Universityof East Africa Social Sciences Conference,'' 1968.
'
Iliffe kapatwa na homa ya ''obsession,'' ya akina Sykes anataka kujua mengi zaidi Daisy akipewa ''assignment,'' anakwenda kwa baba yake anauliza anapewa maelezo na ushahidi wa nyaraka.

Iliffe kila akielezwa hili ndani linazuka jingine akataka kujua ilikuwaje Abdul Sykes akawa General Secretary wa Dar es Salaam Dockworkers Union mwaka wa 1948.

Iliffe akapewa maelezo na nyaraka akaandika paper hii:‘A History of Dockworkers of Dar es Salaam’ TNR, Dar es Salaam, 71, 1970.

Iliffe kama mimi miaka mingi baadae akawa Sykes, Sykes na Sykes.

Sijui kwa nini Iliffe hakuandika historia ya TANU kwa ukamilifu wake wala hakuwa na shauku ya kukutana na Abdul Sykes, baba wa mwanafunzi wake hodari Aisha ''Daisy,' Sykes ambae kamsaidia sana kuijua historia ya African Association na TANU.

Mohamed Said na yeye kwa kumsoma Iliffe gonjwa la Sykes likamkumba.

Mimi nikaamua kufanya kile Iliffe hakufanya nacho ni kuandika maisha ya Abdul Sykes lakini nikaamua pia kuweka mguu wangu pale unyayo wa Iliffe ulipokanyaga.

Hapa ndipo ilipoaanza safari yangu iliyonifikisha hadi Imhambane kijiji kinachoitwa Kwa Likunyi alipotoka Sykes Mbuwane kuelekea Laurenco Marquis akiwa ameongozana na Chief Mohosh na Wazulu wengine kupanda manowari ya Wajerumani kuja Pangani kuanza vita na Abushiri bin Salim na Mtwa Mkwawa mwishoni mwa miaka ya 1880.

Huyu Chief Mohosh ndiye akaja kujulikana kama Affande Plantan Tanganyika akiwa mkuu wa Germany Constabulary.

Prof. Emmanuel Achiempong wa Harvard na yeye gonjwa la Sykes likamkumba akaniandikia mwaka wa 2008 kuniomba anijumuishe katika mradi wa Dictionary of African Biography (DAB) anataka niandike mchango wa Kleist Sykes katika historia ya Afrika.

Mradi huu ulijumisha waandishi na watafiti takriban 500 kutoka kila pembe ya dunia.

Oxford University Press, New York wamechapa volumes sita ya kazi hii.

Bwana Ndjabu,
Yako mengi lakini kwa leo tuuishie hapa sitaki kuwachosha wasomaji.

NB:
Mwaka wa 2011 katika kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika serikali ikaamua kutunuku Medali ya Mwenge wa Uhuru kwa Ally na Abdul Sykes kwa kutambua mchango wao katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
Mzee salaaam. Mie nimeifurahia sana makala hii. Basi ukijaaliwa siku ingine hebu tupatie na makala ya ndugu yetu Kigoma Malima enzi zile za vuguvugu la vyama vingi. Manake kwenye historia ya vyama vingi na siye mtu wa kuacha nyuma. Asante
Blue Dog,
Nimeandika mengi kuhusu Malima.
Ingia na fanya search: mohamedsaidsalum.blogspot.com.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
 

Attachments

  • ISSA AUSI NA ALLY SYKES.JPG
    11.9 KB · Views: 8
  • IDDI SIMBA KHITMA YA MWISHO.jpg
    38.7 KB · Views: 9

Itabidi utuandikie pia hadithi ya The really Idd Simba. Amefanya mambo mengi sana. Ili tuwe waungwana yote yakae wazi. Na heshima ya Saigon iendelee kuenziwa
 
Itabidi utuandikie pia hadithi ya The really Idd Simba. Amefanya mambo mengi sana. Ili tuwe waungwana yote yakae wazi. Na heshima ya Saigon iendelee kuenziwa
Sl

Sent using Jamii Forums mobile app
Laki...
Wote wanataka kutambulika hii fikra kuwa kulikuwa na watu walitaka kutambulika wewe umeitoa wapi?

Watake kutambulika kwa kufanya nini?

Huenda wewe hujui yaliyopitika baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961.

Sijapata kusikia au kusoma popote kuwa katika waasisi wa TANU wako waliotaka kutambulika.

Mimi nililiona tatizo la historia ya TANU mwaka wa 1981 katika kitabu cha Chuo Cha CCM Kivukoni.

Historia ile waliyoandika haikuwa historia ya TANU niijuavyo mimi ndipo nikaandika hii historia mnayoisoma hivi sasa hapa barzani.

Ninachokiona kwenu ni nyinyi kutaabika na historia hii ya kweli kwa akili zenu kukataa kuamini ukweli wa mambo mkatamani kubakia na ile historia iliyowafuta wazalendo waliuounda TANU na waliopigania uhuru wa Tanganyika.


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Shida yako kubwa ni kutaka kuonyesha utakatifu wa kundi lenu na kwanini historia haiwatambui hivyo. Ila historia Mwalimu mzuri sana. Kuna siku tutayajua tote hata yale yanayofanywa gizani
 
Kwani kipi kibaya alichokisema hapa mwandishi? Acha kuleta udini ila ukitaka history sana ya nchi hii katika kutetea Uhuru wetu wallah!! Waislam walijitoa 100%
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…