Kiasi gani Wazungu wametuacha kiteknolojia

Kiasi gani Wazungu wametuacha kiteknolojia

Kosa kubwa walilofanya hawa wapigania uhuru mimi nawaita wapigaji ( kumfukuza mkoloni na kula wao) wangedai usawa yaani haki sawa ya kushiriki shughuli za uchumi wakawaacha tukashirikiana nao tungekuwa mbali sana
 
Katika technology wametuzidi, tujifunze kukubali baathi ya mambo, kuna mambo mengine tumewazidi

Hoja mezani ni teknolojia, kama unataka mambo mengine sijui utayapima kwa order ipi.... mfano useme tumewazidi uvivu wa kufikiri..!!
 
Cha ajabu Hadi Leo hii tunafundishwa namna ya kunawa mikono ili kujiepusha na kipindupindu....
Sisi waafrica tumeachwa zaidi ya miaka 1000

Mamamae unapishana na njemba inatoka chooni halafu inalipita sinki la kunawia kama haioni vile, hapo akitoka ni salamu za kushikana mikono smdh.... unajiuliza unaacha tu au mtu atanawa kwa mkumbo tu ila akiwa pekee yake hana muda kabisa.
 
Yani tunachokifanya kwenye huu uzi ndio kinazidi kutuweka mbali kuwakuta na kweli hatutowakuta milele
 
Kwenye mambo ya kugegedana, style mbalimbali, kukata viuno, umbea, uvivu, maneno mengi, nk huko tumewaacha mbali sana..

Jielekeze kwenye hoja, teknolojia.... ambayo hata hizo kugegedana mnashinda pornhub kujifua.
 
Tukipita njia walizopita wao tutahitaji miaka 500 kufika walipo leo.Tukiwaiga wao walivyofanya kamwe hatuta wafikia,kwani tutakuwa kuwa tunawafuata kwa nyuma.

Solution ni kutafuta njia yetu ya kufuata angalia nchi kama china na nchi za falme za kiarabu.
 
Kwanza kabisa nataka niweke bayana wazungu ambao nawazungumzia, hawa ni wazungu ambao walikuja huku kwetu Afrika na kututawala, kwa kesi yetu ya Tanzania nitawaongelea Wajerumani na Waingereza.
Kutokana na kufanyika mradi mkubwa wa reli SGR hapa tanzania nitatumia reli kama uwanja wa kutupima sisi watanzania na wazungu, haya ndo majibu yanayopatikana
WAMETUZIDI MIAKA >200+
Treni na reli kwa wazungu sio kitu kigeni kwani wanacho tokea miaka ya 1800, hivyo basi kutokana na sisi mpaka sasa kutokuwa na uwezo wa kutengeneza treni na reli yetu hivyo inatuonyesha ya kwamba ni miaka zaidi ya mia mbili wapo mbele.
Hii inamaanisha kama ni umri basi wao wapo mbele miaka mia mbili na zaidi hali hii inawafanya kuwa na uzoefu mkubwa sana kulinganisha na sisi, chukulia mfano mtu mwenye uzoefu wa miaka kumi alivyo kuwa mjuzi itakuwa vipi kwa mtu mwenye uzoefu miaka mia mbili na zaidi.
Kutokana na kuwa na jibu ambalo sio number kamili ( miaka mia mbili na Zzidi) nataka kutumia baathi ya nadharia ili kufanikisha adhimio langu la kupata miaka kamili ya kiasi ambacho tumepitwaa na wazungu hivyo natumia kigezo cha utambuzi wa majengo ya kihistoria ambapo kwa Tanzania jingo la utambuzi unaanzia miaka 1868 na kushuka chini, na ukiangalia Wajerumani nyumba zao za kihistoria zinanza miaka ya 1300 sasa kwa kufanya hesabu za kutoa. Tupapata tukitafutacho.
1868 – 1300 = 568
Hivyo basi napenda kuhitimisha mjadala wangu kwa kusema ya kwamba tumepitwa miaka mia tano na sitini nane.
Yale mambo ambayo bibi yako wa Namtumbo au mjomba wako wa Shinyanga angekatwa katwa mapanga kuitwa mchawi wenzio wameyafanya na wanafikiria pakubwa zaidi!.
Hujanielewa!?.
Namaanisha wazungu wana TRENI ZINAZOELEA!...yani wameweza fanya treni ikatembea kwa kutumia SUMAKU sio haya matakataka ya SGR!.. Sikufuru katafute/kagugo hii kitu MAGLEV TRAINS!!!..

(Bill Gate alijaribu kutuboost afrika labda tuwasogelee wao kiteknolojia kupitia mradi wake wa "LeapFrog" akaishia kugundua kusafisha maji ya choo yanyweke upya kizembezembe!, but seriously leo hii tutamfikia mjerumani ambaye anafunga smartphone traffic light ili kusaidia wale smartphone addict wasigongwe na magari!.
Nimekuacha tena!?.
Munich kuna hizi traffic light sasa badala ya kufungwa kwenye mataa kama Tazara wao wanafunga barabara za watembea kwa miguu, huitaji kuinua macho we tembea umeinamia simu yako bado utaziona taa kwa chini.
)

Tumeachwa MBINGU NA ARDHI jombaaa!!.
 
Tukipita njia walizopita wao tutahitaji miaka 500 kufika walipo leo.Tukiwaiga wao walivyofanya kamwe hatuta wafikia,kwani tutakuwa kuwa tunawafuata kwa nyuma.

Solution ni kutafuta njia yetu ya kufuata angalia nchi kama china na nchi za falme za kiarabu.
China na waarabu wapo mbele tangia enzi, cheki great wall of china, angalia arab numeral or name of stars utaelewa
 
Nakubaliana na wewe 100/% Huwa nikiiangalia hii meli kwenye picha ndio huwa naamini jinsi gani tulivyoachwa nyuma. Hii meli, MV Liemba, ililetwa na Mjerumani in 1915 (zaidi ya miaka 100). Yaani miaka miwili kabla ya kushindwa kwenye vita ya kwanza ya Dunia.

Mpaka leo hii tumeshindwa kupata replacement ya hii meli. Cha ajabu zaidi, MV Liemba bado inatoa huduma mpaka leo. Itatuchukua miaka mingine 500 kabla ya kuwafikia hawa watu.
Liemba1.jpeg
 
Hakuna mtu duniani anaeweza kukupa teknolojia.

Mzungu kakuweka kwenye dema. Unapowaona wanatangaza "scholarships" mbio mbio mnakimbulia kupeleka "vichwa" vyenu huko, vile vya uhakika wanahakikisha havirudi huku kabisa, labda vije kutembelea ndugu jamaa na marafiki, wiki mbili tu.

Mnafikiri "scholarships" ni msaada ule? Ile ni "investment" inayolipa sana.
 
Huku kwetu ndio kwanza tunawahimuza mjenge vyoo,maana hata vyoo tu hamna.
 
Hakuna mtu duniani anaeweza kukupata teknolojia.

Mzungu kakuweka kwenye dema. Unapowaona wanatangaza "scholarships" mbio mbio mnakimbulia kupeleka "vichwa" vyenu huko, vile vya uhakika wanahakikisha havirudi huku kabisa, labda vije kutembelea ndugu jamaa na marafiki, wiki mbili tu.

Mnafikiri "scholarships" ni msaada ule? Ile ni "investment" inayolipa sana.
Kumbe mda mwingine unaandika point
 
Back
Top Bottom