Kiba na Diamond wagoma kuimba wimbo wa hamasa kwa Serengeti Boys

Kifurukutu

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2013
Posts
4,641
Reaction score
6,694
Wanabodi

Hapo awali kuliripotiwa habari za kuimba wimbo wa pamoja utakaowajumuisha wasanii wakuu wawili hapa nchini kwaajili ya kutoa "hamasa" kwa vijana wetu serengeti boys watakapoenda kutuwakilisha katika mashindano ya mpira wa miguu barani Africa kwa vijana chini ya miaka 17

Habari zilizopo sasa ni kwamba Alli Kiba na Diamond wamegoma kushiriki kuimba wimbo huo ili kuwajaza hamasa vijana wetu

Kiukweli hawa wasanii kitendo hiki si cha kiuzalendo kabisa!
kwani serengeti boys ni timu ya taifa na inahitaji kila mtanzania ajitoe kuisapo kwa namna yoyote ile!

moja kwa moja hawa wasanii wetu bado wanaendeshwa na bifu na timu zao zisizo hata na viwanja, "inasikitisha" kwa kweli

Watanzania tuungane pamoja tuwahamasishe vijana wetu watatutoa kimasomaso,
Shame on you Kiba
Shame on you Diamond
 
Hivi uzalendo ni nini hasa maana kwetu kufanya kitu free of charge au kufanya kazi muda wa ziada hata kama huna mood tunachukulia ndo uzalendo...
Uzalendo ni kujitoa kwaajili ya manufaa ya nchi yako!

kwani kutoa wimbo wataifa uwape vijana inacost bei gani?

Tuweke tofauti zetu pembeni tulisaidie taifa
 
Wanalipwa?

Kila mtu ana uhuru wa kuishi kwa ujira wa kazi yake.

Kila mtu ana uhuru wa kufanya kazi iliyo sawa na uwezo wake.

Hizi ni haki za kikatiba.

Unaelewa hilo?
 
hahaha, nchi ya kusadikika. mpira ni sanaa na ni sayansi pia hamna shortcut katika maisha lazima kupitia stages zote kufikia mafanikio. Sasa unahamasisha kwa wimbo then what😱😱😱
Wizara haina strategies haina exposure haitaki kujifunza vitu vipya, akitokea mtu kapaa nao wanadandia ju kwa juu refer yule mwanariadha India/UK
 
Uzalendo ni kujitoa kwaajili ya manufaa ya nchi yako!

kwani kutoa wimbo wataifa uwape vijana inacost bei gani?

Tuweke tofauti zetu pembeni tulisaidie taifa
Hivi Tanzania nani ni mzalendo? Nipe mtu mmoja tu anafanya kazi bure kwa ajili ya taifa, si jeshi, wanasiasa mpaka Rais kila mtu anachukua chake labda huyo Trump ndi hataka mshahara. Hata hao TFF ni pesa tu kama definition ya mzalendo ni free of charge then hakuna wazalendo.
 
mkuu tuwekee source ya hiyo news tafadhali!!!
 
Tuache kupangiana majukumu ya kufanya....wanaimba ili wapate pesa za kuendeshea mambo yao hawaimbi kumfurahisha mtu alafu wasipate kitu.
 
Wenzako wanaangalia maslahi yao kibiashara, wewe machinga unapiga domo tu hapo
 
Uzalendo ni kujitoa kwaajili ya manufaa ya nchi yako!

kwani kutoa wimbo wataifa uwape vijana inacost bei gani?

Tuweke tofauti zetu pembeni tulisaidie taifa
Usikariri manufaa ya nchi.

Hata wasanii kutoa mfano kwamba wananchi hawatakiwi kukubali kila kitu wanachopangiwa na serikali ni kitu chenye manufaa.

Hivyo ni uzalendo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…